Skip to main content

BENKI YA TADB YAKABIDHI NG'OMBE 153 KWA WAFUGAJI KASKAZINI PEMBA





IMEANDIKWA NA KHAULAT SULEIMAN, SUZA

 

BENKI ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB)  imekabidhi ngombe 153 wa maziwa kwa wafugaji 153 kisiwani Pemba, ambao wameletwa kutoka Afrika Kusini. 

 

Ngombe hao wamekabidhiwa wafugaji wa vikundi mbali mbali vya Mkoa wa Kaskazini Pemba kwa lengo la kuwawezesha wafugaji hao kufuga kibiashara na kuwaleta tija.  

 

Akikabidhi ngombe hao  Waziri wa Kilimo, Umwagiliaji Maliasili na Mifugo Zanzibar Shamata Shame Khamis aliishukuru benki hiyo kwa kushirikiana na mradi wa TI3P na Shirika la Heifer International Tanzania kwa juhudi zao za kumkwamua mfugaji wa kawaida kiuchumi na kumuwezesha kukuwa kibiashara zaidi.

 

Alisema kuwa, anaamini kuwa kupitia mkopo huo ng’ombe kwa wafugaji hao kutaweza kuwakwamua kiuchumi, kwani watazalisha maziwa mengi na kuuza, jambo ambalo litawapatia fedha zitakazowakwamua na maisha duni.

 

"Wafugaji nendeni mkafuge kwa tija ili kujiletea maendeleo wenyewe na Taifa kwa ujumla, kuweni mfano kwa wafugaji na wakulima wengine,’’ alieleza Waziri Shamata . 

 

Aidha Waziri huyo aliwataka wafugaji hao kushirikiana kulinda mifugo yao, ili kuepuka kupata maradhi, kuharibiwa, wizi na kusema kwamba ikitokea mtu yeyote akanajis mifugo hiyo atachukuliwa hatua za sheria. 

 

"Andaeni utaratibu mzuri kwa mifugo yenu kwani mwezi wa Oktoba watajifungua, hivyo wanahitaji mazingira ambayo hayatawaletea madhara wao na hata watoto wao, vifaa vya uzalishaji wa maziwa vitafuteni kwa wingi, ili tuweze kupata engezeko kubwa la uzalishaji wa maziwa nchini,” alieleza

 


Nae Meneja wa Benki hiyo Dames Damian alieleza kuwa, kwa kushirikiana na Shirika la Heifer international Tanzania, Serekali ya Mapinduzi ya Zanzibar kupitia Wizara ya Kilimo, Umwagiliaji na Mifugo, pamoja na chama Kikuu cha Wafugaji wa Ngombe cha pemba (PDCU), TADB imetoa mikopo ya ngombe wa kisasa wa maziwa (mitamba)  wenye mimba kati ya miez 3-6 kwa riba nafuu ya asilimia tisa (9%), ambapo mkopo huo umegharibu shilingi 877,608,000.

 

“TADB imetoa ruzuku ya asilimia 25 kwa wafugaji hao, hivyo wananchi ondoeni hofu kuhusu mikopo juu ya kuwawezesha kwani tayari benki yetu imeshatenga fedha za kuwawezesha miradi yenu, ili iweze kuleta tija kwenu na Serekali,” alieleza

 

Mapema Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo na Mifugo Pemba, Asha Zahran Mohamed alieleza, mradi huo utaweza kuwakomboa wafugaji kwa uzalishaji mwingi wa maziwa na kuachana na maziwa yenye kemikali.

 

"Wizara ipo tayar kutoa mashirikiano ya kutosha kwa kutoa elimu ya matibabu pamoja na kutoa mbegu za shindano bure kwa ajili ya upandishaji wa mbegu kwa ngombe hao, hivyo wawe tayari kushirikiana na wizara yetu,” alieleza

 

Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini Pemba Salama Mbarouk Khatib, aliwataka wafugaji hao na Wizara husika kushirikiana pamoja, ili lile lengo la Serekali liweze kufikiwa la uzalishaji wa maziwa mengi kisiwani Pemba.

 

 "Hatua hii tunategemea italeta tija kwa wananchi na Serekali, hivyo sasa ni jukumu lenu kuwajibika ipasavyo ili mradi huo uwe na ufanisi zaidi,” alifahamisha Mkuu huyo

  


Akiwasilisha risala fupi kwa niamba ya vikundi vilivyokabidhiwa ng’ombe hao, Meneja wa Ushirika Subira Talib Khamis alieleza kuwa, kwa kushirikiana na wadau mbali mbali wa maendeleo, tayari wameshapata mafunzo ambayo yatawawezesha kufuga na kuzalisha maziwa na nyama katika hali ya usalama zaidi, hivyo Serekali watarajie ongezeko la lita asilimia 15 kwa siku . 

 

Zaidi ya vikundi saba vimekabidhiwa ng’ombe hao, miongoni mwa hivyo ni kikundi kutoka Kifundi Konde, Tundwa Piki, kikundi cha Mola Kinyasini, Tumeridhika kutoka Finya, Tuko Imara Kiungoni, Kiuyu  na Kinyasini Jiamishe.

 

                                                  MWISHO.

 













Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

…….SUZA WATOA USHAURI WA ADHABU YA KUNYONGWA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WANAFUNZI wanaosomea uwalimu Chuo cha taifa cha Zanzibar ‘SUZA’ kampasi ya Benjamin Wiliam Mkapa Wete Pemba, wamependekeza adhabu ya kunyongwa hadi kufa, kwa mtu atakaetiwa hatiani, kwa kosa la dawa za kulevya. Walisema, haiingii akili kuona, mahkama imeshamtia hatiani mtu kwa kukutwa na dawa za kulevya, ambazo huathiri nguvu kazi ya taifa na kisha, kupewa hukumu ya kifungo pekee. Wakizungumza leo Juni 26, 2024 kwenye kongamano la vyuo vikuu, juu ya masuala ya msaada wa kisheria, kuelekea wiki ya msaada wa kisheria Zanzibar, lililofanyika Chuoni hapo, walisema wakati umefika sasa kutolewa kwa hukumu hiyo. Walipendekeza kuwa, ni vyema kwa mtu anayetiwa hatiani asibakie chuo cha Mafunzo pekee kuitia tena hasara serikali kwa chakula na wakati mwingine matibabu, wakati tayari ameshasababisha madhara, kwa vijana. Mshiriki Juma Nafasi Juma, alifafanua kuwa kama mtu ameamua kuliumiza taifa kwa kuingiza, kusafirisha, kusambaaza dawa za kulevya, hivyo ni vy

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan