Skip to main content

DPP: ‘CHONGA ITAKUWA SALAMA KIUHALIFU WANANCHI MKIAMUA’

 

NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

AFISI ya Mkurugenzi wa Mashtaka Zanzibar afisi ya Pemba, imewahakikishia wananchi wa shehia ya Chonga wilaya ya Chake chake, kuwa kama wako tayari kushirikiana na vyombo vya sheria, shehia yao itakuwa salama na vitendo vya kihalifu.

Hayo yameelezwa  leo Septemba 6, 2024 na Mwendesha Mashtaka Dhamana wa mkoa wa kusini Pemba, kutoka afisi hiyo, Seif Mohamed Khamis, wakati akijibu hoja za wananchi hao, waliooneshwa kushindwa na vitendo vya kihalifu vinavyofanywa na watoto wao, kwenye mkutano wa kuwajengea uwezo wananchi hao.



Alisema, kama kweli wananchi hao wameshakua tayari kuviondoa vitendo vya kihalifu kama wizi, utumiaji wa dawa za kulevya, wajitayarishe kuona mabadiliko muda mfupi ujao.

Alieleza kuwa, atahakikisha ofisi yake, kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi na kitengo cha dawa za kulevya, wataunda timu ambayo wanawategemea wazazi na walezi, ili kuiweka Kipapo salama.

Alisema, hata wao watafurahishwa mno, ikiwa wazazi sasa wako tayari, kuhakikisha wanashirikiana na vyombo vya ulinzi na usalama, kwani uhalifu hauathiri tu shehia hiyo pekee.

‘’Sisi baada ya maelezo yenu, tumeona ipo haja ya kuhakikisha tunaunda timu kati yetu na Jeshi la Polisi na kitengo cha kupambana na dawa za kulevya, ili kuisafisha shehia ya Chonga na vitendo vya kihalifu,’’alieleza.

Katika hatua nyingine, Wakili huyo wa serikali, aliwakumbusha wananchi hao, kuhakikisha wanawaibua wahalifu waliomo katika shehia yao, ili wakati ukifika wa operesheni iwe rahisi kuwakamata.

Kwa upande wake, Wakili wa serikali kutoka Afisi hiyo Zubeir Awam Zubeir, alisema hakuna hatia yoyote mahakamani, pasi na wananchi kutoa ushahidi.



Akizungumzia mkutano huo maalum, alisema lengo lake hasa ni kuwafuata wananchi walipo, ili kusikiliza maoni yao, kama sehemu ya kutokomeza vitendo vya ukatili na udhalilishaji.

‘’Tunapokuwa afisini, huwa tunaona majalada tu ya watuhumiwa, lakini sasa tumeamua kufika kwa wananchi wenyewe, ili watuhadithie na kutupa ushauri wa kuondoa matendo hayo,’’alieleza.

Hata hivyo amewakumbusha wananchi hao, kutozifanyia sulhu kesi za udhalilishaji, na badala yake zikitokezea tu, wananchi waziripoti katika vyombo vya sheria.

Mkuu wa dawati la jinsia la Jeshi la Polisi mkoa wa kusini Pemba Habiba Ali Said, alisema bado wapo wananchi wamekuwa wakizichelewesha kuziripoti kesi za udhalilishaji.




‘’Tumebaini, baada ya mtoto kubakwa, mzazi anamtafuta aliyembaka mtoto wake, na baada ya siku tatu hadi nne, ndio anaamua kufika Polisi kulalamika, kitendo cha kuchelewa kwake, ameshapoteza asilimia kubwa ya ushahidi,’’alieleza.

Akijibu baadhi ya maswali ya wananchi hao, alisema kama watashirikiana vilivyo na Jeshi la Polisi, hasa katika eneo la ushahidi, vitendo vya kihalifiu vitamalizika katika jamii.

Akifungua mkutano huo, sheha wa Chonga Ali Juma Nte, alisema elimu hiyo kwa wananchi wake ni muhimu, kwani shehia yao, imekuwa ikiongoza kwa uhalifu.



Baadhi ya wananchi, walisema kasoro kubwa bado iko ndani ya Jeshi la Polisi, kwa kutofuatilia vilivyo, baadhi ya kesi wanazoziripoti kituoni.

Abdalla Omar Ali na mwenzake Said Omar Ali, walisema bado ndani ya Jeshi la Polisi, wapo baadhi ya askari wanafanyakazi kinyume na kanuni zao, jambo linalowafanya kutokuwa na hamu ya kushirikiana nao.

Kwa upande wake, Salim Mbarouk Ali na Mohamed Shaib Kombo, walisema kwa sasa shehia yao, inatishia kwa kuwepo kwa matukio ya kihalifu, kama mauwaji na wizi.

‘’Kwa sasa haipiti wiki moja, shehia ya Kipapo usisikie kuna mtu kauliwa, kupigwa, wizi wa kuku, uvunjaji nyumba au watoto kudhalilishwa, hili sasa linatuchosha,’’walieleza.







Miongoni wa majukumu makuu ya Afisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka, ambayo imeanzishwa mwaka 2002, kufuatia marekesbisho ya nane ya Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984, ni kuendesha mashtaka, kusimamia vyombo vya dola ili kusiweko na matumizi makubwa ya nguvu.

                                     Mwisho

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

…….SUZA WATOA USHAURI WA ADHABU YA KUNYONGWA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WANAFUNZI wanaosomea uwalimu Chuo cha taifa cha Zanzibar ‘SUZA’ kampasi ya Benjamin Wiliam Mkapa Wete Pemba, wamependekeza adhabu ya kunyongwa hadi kufa, kwa mtu atakaetiwa hatiani, kwa kosa la dawa za kulevya. Walisema, haiingii akili kuona, mahkama imeshamtia hatiani mtu kwa kukutwa na dawa za kulevya, ambazo huathiri nguvu kazi ya taifa na kisha, kupewa hukumu ya kifungo pekee. Wakizungumza leo Juni 26, 2024 kwenye kongamano la vyuo vikuu, juu ya masuala ya msaada wa kisheria, kuelekea wiki ya msaada wa kisheria Zanzibar, lililofanyika Chuoni hapo, walisema wakati umefika sasa kutolewa kwa hukumu hiyo. Walipendekeza kuwa, ni vyema kwa mtu anayetiwa hatiani asibakie chuo cha Mafunzo pekee kuitia tena hasara serikali kwa chakula na wakati mwingine matibabu, wakati tayari ameshasababisha madhara, kwa vijana. Mshiriki Juma Nafasi Juma, alifafanua kuwa kama mtu ameamua kuliumiza taifa kwa kuingiza, kusafirisha, kusambaaza dawa za kulevya, hivyo ni vy

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan