Skip to main content

WANAUME WANAOPIGWA NA WANAWAKE CHAKE CHAKE WATAKA DAWATI KUTOA MALALAMIKO

 

NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

WANAUME wa shehia za Kibokoni na Vitongoji wialaya ya Chake chake, wamesema wakati umefika sasa, wa kuanzishwa kwa dawati la siri la kundi lao, ili kutoa malalamiko, wanapopewa kichapo na wanawake.

Ushauri huo wameutoa Septemba 5, 2024 kwenye kongamano la kujadili njia za kutokomeza ukatili na udhalilishahaji wa kijinsia, lililoandaliwa na Mwemvuli wa asasi za kiraia Pemba ‘PACSO’ na kufanyika skuli ya sekondari ya Vitongoji wilayani humo.

Walisema wapo baadhi yao, wanaopokea vipigo kutoka kwa wake zao, ingawa wamekuwa hawajui wapi wakaripoti madhila hayo.

Walieleza kuwa, wapo wanawake wamekuwa wakatili kwa waume zao, ingawa wanapokumbumbwa na changamoto hizo, hushindwa wapi wakaripoti.



Mmoja kati ya wanaume hao, Salim Ayoub, alisema wanaoa aibu kwenda moja kwa moja kituo cha Polisi kuripoti matukio hayo, hivyo kama wataanzishiwa dawati lao, watejenga uthubutu wa kuziripoti kesi hizo.

Alifahamisha kuwa, kama serikali inataka kujua njia sahihi ya kupunguza matendo wanayofanyiwa, kwa sasa ni kwepo kwa dawati la wanaume, la kushughulikia malalamiko yao.

"Wakati umefika sasa kuwapa haki ya faragha wanaume wanaopigwa na wanawake, ili nao kuwa huru kuziripoti kesi za udhalilishaji ikiwemo kipigo,’’alishauri.

Nae Haji Yussuf Khamis, alisema sio sahihi panapozungumziwa ukatili na udhalilishaji, wanaume kuachwa nyuma, kama vile hawakumbani na changamoto hizo.



‘’Hata sisi wanaume tunadhalilishwa na wanawake, sasa lazima sheria ituangalie na ikiwezekana ituwekee mahakama ya siri, ili kufikisha malalamiko yetu,’’alisema.

Kwa upande wake Jokha Abdalla Ali, alishauri kuwa, watoto wanaofanyiana udhalilishaji, lazima kwe na adhabu mbadala, ili waingie woga.

Mwanasheria Aziza Suleiman Mohamed, alisema rushwa muhali ni miongoni mwa sababu, inayochangia kuendelea kwa metendo hayo.




‘’Sheria ziko wazi, kuwa hawezi kutiwa hatiani mtu yeyote, pasi na ushahidi usio kuwa na shaka, lakini kama hatutoshirikiana na vyombo vya sheria, tusitegemee mabadiliko,’’alifafanua.

Akizungumza kwenye kongamano hilo, Mratibu wa miradi kutoka ‘PACSO’ Mohamed Najim Omar, alisema lengo la kongamano hilo, ni kuwapa nafasi wanajamii kutoa mawazo yao, nini kifanyike ili kutokomeza udhalilishaji.

Alisema, PACSO imeona kutumia njia hiyo, kwa vile wakosaji wa makosa hayo, wanatoka ndani ya jamii yenyewe.



‘’Makongamano haya ya wazi, yatakuwa endelevu kila tunapopata nafasi, na lengo lake hasa ni jamii kutoa fikiria zao ni namna gani, matendo haya yatakoma ndani ya vijiji vyetu,’’alifafanua.

Akifunga kongamano hilo, sheha wa Kobokoni Khalef Othman Khamis, alisema hata tafsiri ya umri wa mtoto, kwa sasa ni shangamoto.




‘’Kisheria hadi miaka17 bado ni mtoto na anakinga, lakini makosa anayoyafanya ni makubwa, ni zaidi ya mtu mzima, na huu umri napendekeza upunguzwe,’’alifafanua.

Katibu Mkuu wa ‘PACSO’ Sifuni Ali Haji, alisema kinachofuata kwa sasa ni kuanzisha kamati za maadili zenye mfumo wa polisi jamii, ili kuwakinga watoto na udhalilishaji.

‘’PACSO kama muungano wa asasi za kiraia, imefanya wajibu wake, kilichobakia sasa ni jamii kukaa chini na kuwa na sheria ndogo ndogo, ili kuwalea watoto wetu,’’alifafanua.





Katika hatua nyingine, amwataka watoto kutoa taarifa za haraka kwa wazazi, waalimu, masheha na watu wingine watapoona dalili za kufanyiwa ukatili.

                                   MWISHO

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

Vikausha damu vya mjamzito hivi hapa, umo mchele, udongo, mkaa, chaki Uwezekano wa kuzaliwa watoto wenye udumavu, utapiamlo ni mkubwa

  NA ZUHURA JUMA, PEMBA@@@@ ‘’KILA ninapobeba mimba nimezoea kula mchele kwa wingi naweza kusamehe pilau au biriani,’’ ndio maneno ya mwanzao ya Bahati Mohamed Ali (sio jina lake halisi). Nilimfuma akiwa barazani kwake, mjini Ole wilaya ya Chake chake, pembeni yake akiwa na kibakuli cha mwazi, kwa umbali utaona amejaza chakula aina ya pepe, kumbe ni mchele wa Mbeya. Hujichotea kidogo kidogo na kuushindilia mdomoni mwake, huku akiendela kupiga storia na wenzake, bila ya kujali kuwa ujauzito alionayo na mchele huo hauna mwisho mwema. Kawaida yake akiwa mjamzito, kila anapoamka asubuhi anaroweka mchele upatao robo kilo hivi…na baada ya kumaliza kupika, yeye huchukua mchele wake kutafuna (kula). Wakati mwenza wake na watoto wao, wanakula chakula cha mchana, Bahati yeye hukaa pembeni na kibakuli chake cha mchele akiendelea kubahatisha afya yake. ‘’Mimba nyengine hupenda sana kutafuna mchele wa Mbea na nyengine hupenda mchele wa mapembe, kwa kweli huwa nina hamu (kileo), kwan...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...