Skip to main content

VIKUNDI VYA KUHIFADHI MAZINGIRA VYAOMBA KUUNGWA MKONO




IMEANDIKWA NA ZUHURA JUMA, PEMBA

WANAKIKUNDI cha kuhifadhi mazingira cha ‘Nyange Cooperative’ waliopo shehia ya Mjiniole wilaya ya Chake Chake wameiomba Serikali kuviunga mkono vikundi vyote vinavyojishughulisha na uhifadhi wa mazingira kwa kuwachukulia hatua za kisheria wananchi wanaokata miti ambayo hupandwa na vikundi hivyo kwa lengo la kuzuia maji ya bahari yasipande juu kwenye mashamba yao.

Walisema kuwa, wamekuwa wakipoteza nguvu nyingi kupanda miti ya mikoko kwa ajili ya kurudisha uoto asili na kuzuia mabadiliko ya tabianchi, ingawa wamekuwa wakirudi nyuma kutokana na wananchi kuikata huku wakiendelea kuachwa bila ya kuchukuliwa hatua.

Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi wanakikundi hao walieleza kuwa, hakuna siku hata moja waliyoona watu wanaokata miti hiyo wakichukuliwa hatua za kisheria licha ya kuzifikisha kesi hizo sehemu husika.

‘’Kilichotushanga ni kwamba, siku moja tulikata miti kidogo ili tupate pesa angalau ya kununulia vifaa tunavyotumia lakini wananchi walikwenda kutushtaki na tulichukuliwa, sasa kwa nini tunapopeleka kesi za wizi tunapuuzwa?, kwa kweli inauma,’’ walisema.

Mmoja wa wanakindi hicho Hamad Khatib Hamad alisema, wao ndio waliopanda miti hiyo ingawa walipoikata walichukuliwa kwenda kujielezea lakini hawakupatikana na hatia, hivyo waliiomba mamlaka husika wanapowafikishia kesi wasipuuze.

Alieleza kuwa, itafika mahala na wao watachoka kupanda miti, hali ambayo itasababisha maji ya bahari kupanda juu na kuingia kwenye mashamba ya wananchi na kuharibu vipando vyao.

Mwanakikundi Hadia Ali Hamad alieleza kuwa, ili waendelee kuotesha miti hiyo ipo haja kwa Serikali kuwawekea udhibiti ili miti isikatwe kwa sababu wanapoteza nguvu nyingi kupanda bila mafanikio yeyote.

‘’Hatujawahi kunufaika na miti hiyo kwa kujipatia kipato, bali tumeona kwamba manufaa makubwa ni kuhifadhi mazingira yetu, ili kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi, hivyo tunaomba tuungwe mkono,’’ alifahamisha.

Nae mwanakikundi Khadija Henock Maziku alieleza kuwa, zaidi ya miti ya mikoko 5000 imeibiwa katika shamba hilo tangu walipoanza kupanda, jambo ambalo linawafanya wakose nguvu ya upandaji.

‘’Wanajamii na wakulima wa tungule nao wanatuharibia sana, hivyo elimu itolewe kwa vijana juu ya umuhimu wa kuhifadhi mazingira, ili tudhibiti hali hii, kinyume chake, maji yatapanda juu tu kwenye makaazi ya watu,’’ alifafanua.

Alieleza kuwa, anaweza kuwakuta wizi ingawa hawezi kuwakamata kwani wanakuwa na silaha, hivyo huwaacha tu licha ya kuwa anaumia moyoni.

Aliishauri Serikali kuwaelimisha wananchi juu ya kuhifadhi mazingira na kuwatoza faini kwa wale wanakamatwa kwa wizi wa miti hiyo, ili eneo libaki katika hali salama.

Kwa upande wake sheha wa shehia hiyo Hamad Said Mgau alisema kuwa, wanajitahidi kuwaelimisha wanajamii juu ya suala ya uhifadhi wa mazingira ingawa binadamu hawezekani.

‘’Kila siku tunawakataza na tunawaeleza na athari zake lakini bado wanaendelea kuikata miti na hawa wanaopanda wanasema wamechoka kushtaki, kwa hiyo wanawaacha tu, jambo ambalo ni hatari kwetu,’’ alieleza.

Afisa Mkuu Idara ya Misitu Pemba Samira Makame Juma aliwataka wanakikundi hao kushirikiana pamoja katika ulinzi na kutoa taarifa Idara ya Misitu ili watendaji wao wafike kuangalia athari iliyotokea na kuchukua hatua ya kuwaita walioharibu au wa pande zote mbili kusikiliza malalamiko yao kwa ajili ya hatua stahiki.

 ‘’Tushirikiane, wanakikundi wajiwekee taratibu na wajulikane na uongozi wa shehia, wajue wanafanya nini, wakifanya hivyo wanaweza kuungana na sheha pamoja na Idara ya misitu kuhakikisha eneo hilo linahifadhiwa kwa taratibu maalumu,’’ alifafanua.

Mkuu huyo aliwataka wananchi kuhifadhi misitu ya juu na ya baharini (mikoko) na kutumia sheria pale ambapo patatokea athari ya uharibifu, ambapo wanatakiwa kujua kuwa miti hiyo sio mali ya mtu mmoja bali ni ya wote kwani yanayawanufaisha wote katika kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi.

Shehia hiyo ina wananchi 2,800 ambapo wanajishughulisha na kilimo cha mazao mbali mbali, uvuvi pamoja na uhifadhi wa mazingira.

                                            MWISHO.                                                             

                                

 








Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

…….SUZA WATOA USHAURI WA ADHABU YA KUNYONGWA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WANAFUNZI wanaosomea uwalimu Chuo cha taifa cha Zanzibar ‘SUZA’ kampasi ya Benjamin Wiliam Mkapa Wete Pemba, wamependekeza adhabu ya kunyongwa hadi kufa, kwa mtu atakaetiwa hatiani, kwa kosa la dawa za kulevya. Walisema, haiingii akili kuona, mahkama imeshamtia hatiani mtu kwa kukutwa na dawa za kulevya, ambazo huathiri nguvu kazi ya taifa na kisha, kupewa hukumu ya kifungo pekee. Wakizungumza leo Juni 26, 2024 kwenye kongamano la vyuo vikuu, juu ya masuala ya msaada wa kisheria, kuelekea wiki ya msaada wa kisheria Zanzibar, lililofanyika Chuoni hapo, walisema wakati umefika sasa kutolewa kwa hukumu hiyo. Walipendekeza kuwa, ni vyema kwa mtu anayetiwa hatiani asibakie chuo cha Mafunzo pekee kuitia tena hasara serikali kwa chakula na wakati mwingine matibabu, wakati tayari ameshasababisha madhara, kwa vijana. Mshiriki Juma Nafasi Juma, alifafanua kuwa kama mtu ameamua kuliumiza taifa kwa kuingiza, kusafirisha, kusambaaza dawa za kulevya, hivyo ni vy

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan