Skip to main content

WAZIRI PEMBE: 'POLISI HARAKISHENI UPELELEZI KESI ZA UDHALILISHAJI'



 Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Riziki Pembe Juma

amelitaka Jeshi la Polisi Zanzibar kuharakisha masuala ya upelelezi kwa kesi za

vitendo vya ukatili na udhalilishaji ili kuona zinamaliza ndani ya muda mfupi.

Kauli hiyo aliitoa jana katika kilele cha maadhimisho ya kufunga siku 16 za

harakati za kupinga vitendo vya ukatili na udhalilishaji kwa wanawake na watoto

yaliyofanyika katika kijiji cha Muyuni Wilaya ya Kusini Unguja.


Mhe. Riziki alisema taarifa za Mtakwimu Mkuu wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar

zinaonesha hali inatisha kwani katika kipindi cha mwezi Januari hadi Octoba 2023

jumla ya matukio 1,620 yameripotiwa ambapo matukio 1,360 yanahusu watoto,

194 wanawake na wanaume 77.

Alisema pamoja na kazi kubwa inayofanywa na Jeshi la Polisi lakini bado

ucheleweshwaji wa upelelezi wa matukio hayo umekuwa mkubwa hali ambayo

inapelekea kesi nyingi kukaa muda mrefu katika vituo vya Polisi Zanzibar.

Alisema kuendelea kwa hali hiyo itaweza kuathiri malengo ya Serikali katika

mapambano ya kuondoa vitendo hivyo pamoja na kuwatia hatiani watu

wanaothibitika kutenda vitendo vya ukatili na kudhalilisha ndani ya nchi.

Aidha alisema ipo haja ya kutambua na kuweka kampeni maalum za kuyakabili

matendo ya udhalilishaji wa Kijinsia kwa kuweka nguvu kazi na kampeni isemayo

“Wekeza katika Kuzuwia Ukatili Dhidi ya Watu Wenye Ulemavu” na “Nijuze

Nijilinde Dhidi ya Ukatili wa Kijinsia”.

Alieleza kwamba kundi hilo la watu wenye ulemavu limekuwa na changamoto

kadhaa ambazo zimekuwa zikiwakabili na hivyo haja ya tafakuri ya kina

inahitajika katika kumkomboa mtu mwenye ulemavu dhidi ya vitendo vya ukatili

wa Kijinsia.



Mapema Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Abeida Rashid Abdalla, alisema bado

matukio ya udhalilishaji yanaongezeka ikiwemo matukio ya kubaka, kunajisi

ambapo Wilaya ya Mjini na Magharibi ‘A’ na ‘B’ zinaongoza kwa kesi hizo

nyingi.

Alieleza kwamba wakiwa wanahitimisha kilele cha siku 16 lakini bado

mapambano yanaendelea hivyo ni lazima jamii kwa pamoja wanaumme na


wanawake wote wanalazimika kupambana na matendo hayo kwani bado kuna kazi

kubwa ya kufanya ili kuhakikisha matendo hayo yanaondoka nchini.

Naye Katibu Tawala Mkoa wa Kusini Unguja, bi Radhia Rashid Haroub,

aliipongeza Wizara hiyo kwa kuadhimisha siku 16 za kupinga vitendo vya Ukatili

na Udhalilishaji katika mkoa huyo. Alisema bado nguvu za mapambano

zinahitajika kwani Mkoa wa Kusini matukio hayo yameongezeka mwaka jana

2022 kulikua na jumla ya matukio 1,320 ambapo kwa mwaka huu yamefikia

matukio 1,620 sawa na ongezeko la asilimia 16.

Kwa upande wa wanaharakati wa kupinga vitendo vya ukatili na udhalilishaji

akizungumza kwa niaba bi Amina Yussuf Ramadhani alisema jamii wameshapat

uwelewa wa kuripoti matokeo hayo lakini bado tatizo la muhali linaendelea

kujitokeza na kusababisha baadhi ya kesi kusuluhishwa katika ngazi ya familia.

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch