Skip to main content

MASHEHA WAWI, WESHA WANG'AKA WANAOHARIBU NGUZO ZA MAJINA YA MITAA

 



NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

MASHEHA wa shehia za Wawi na Wesha wilaya ya Chake chake Pemba, wameahidi kuwa watakula sahani moja kisheria, na mtu yeyote atakaekamatwa akihujumu nguzo zenye majina ya mitaa katika shehia hizo.

Walisema, baadhi ya wananchi wamekuwa wakijaribu kuzing’oa nguzo hizo kwa maksudi, na kuwataka waache mara moja tabia hiyo, kwani atakaekamatwa, sheria itachukua mkondo wake.

Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi kwa nyakati tofauti, kufuatia katika baadhi ya vijiji kung’olewa nguzo hizo, walisema yeyote hatovumiliwa.

Sheha wa shehia ya Wesha Haji Mohamed Ali, alisema tayari katika moja ya vijiji vyake nguzo iliyokuwa na jina la kijiji imeshang’olewa na kuwataka wananchi, wairejeshwe mara moja.

Alieleza kuwa, kwa vile serikali imetumia gharama kubwa kutengeneza nguzo hizo kwa ajili ya kurahisisha shughuli mbali mbali, hatokaa kimnya hadi itakaporejeshwa.



‘’Niwaombe kama kuna mwananchi anajua taarifa za kuibiwa kwa nguzo hizo, aje anipe kwa kina, kwani jambo hilo halitokuwa dogo kama haijarejeshwa,’’alisema.

Katika hatua nyingine, sheha huyo wa shehia ya Wesha Haji Mohamed Ali, alielezea kusikitishwa kwake na tabia ya baadhi ya wananchi kuzitikisa tikisa nguzo hizo.

Sheha wa shehia ya Wawi Sharifa Waziri Abdalla, alisema wapo wananchi wamekuwa wakizitumia nguzo hizo hata kufungia wanyama wao, jambo ambalo sio sahihi.

Alisema, anazo taarifa kuwa zipo baadhi ya nguzo huangushwa kwa makusdi, na nyingine kuchukuliwa, ambapo mwananchi huyo atakayebainika atafikishwa Polisi kujibu.



‘’Ukiharibu nguzo yenye jina la mtaa, ama ukiiba itakuwa umeiba mali ya serikali, hivyo lazima kwa kuhujumu huko mali hizo, ufikishwe mbele ya vyombo vya sheria,’’alifafanua.

Aidha sheha huyo aliwataka wananchi kila mmoja, kuwa mlinzi wa mwenzake, kwani nguzo hizo zenye majina ya mitaa ni kwa manufaa ya watu wote wakiwemo wageni.

‘’Tuelewe kuwa, majina haya ya mitaa yapo kwenye mtandao wa serikali na faida yake kubwa ni kuwarahisishia wageni kwa kufuata nguzo za mitaa hadi anakokwenda,’’alifafanua.

Baadhi ya wananchi wa shehia hizo, walielezea kusikitishwa kwao, na baadhi ya wananchi wenzao, kuihujumu miundo mbinu ya mitaa na vijiji.


Khadija Issa Msellem wa Wesha, alisema hakuna haja kwa wananchi wenzao, kuzing’oa nguzo hizo, kwani moja ya faida kubwa ni mitaa kuwa na majina ya kudumu.

Amina Omar Mzale wa shehia ya Wesha, alisema ni vyema atakaebainika kuihujumu miundombinu hayo, kuchukuliwa sheria kali, ili iwe funzo kwa wengine.

Askari shehia ya Wawi Issa Ahmad, alisema kimsingi nguzo ni mali ya wananchi, wanayohaki ya kuzilinda na kuhakikisha hakuna anaeziharibu, kwani athari yake ni kubwa.




Nassor Khamis Mohamed, alisema wakati umefika sasa wa wananchi kuelimishwa juu ya umuhimu wa nguzo hizo, kwani wengi wanafikiria ni kama urembo.

Akizundua zoezi hilo, Mkuu wa Mkoa wa kusini Pemba Mattar Zahor Massoud, aliwataka wananchi kujali gharama iliyotumika katika kutengeneza nguzo hizo.

                                          Mwisho

 

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch