Skip to main content

DC: MICHEWENI ATOA RAI ULEZI WA MAYATIMA

 


NA ASHA ABDALLA , PEMBA @@@@   

MKUU wa wilaya ya Micheweni Mgeni Khatibu Yahya, ame wataka wazazi na walezi, kuwa makini katika kuwalinda watoto ili waweze kuepukana na vitendo vya udhalilishaji,  ambavyo vimeshamiri nakuongezeka siku hadi siku. 

Hayo aliyasema wakati alipokuwa akikabidhi misaada kwa Mayatima  kwaniaba ya Mwenyekiti wa Nuru Foundation Zainab Kombo Shaib, ambae ni Mke wa Makamo wa Kwanza wa Rais wa  zanzibar katika Mahafali ya 11 yaliyofanyika Madrassatu _ Nnisai iliopo Machomane Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba. 

Alieleza kuwa  watoto Mayatima  wanatakiwa kutunzwa vizuri na kulelewa kama Watoto wengine bila ya kubaguliwa  kwani nao wana haki ya kupata Elimu ili  waweze kufarajika katika maisha yao ya kila siku. 

"Watoto Mayatima tuwapeni  Misaada kwani nawao wanahitaji upendo nafuraha ili  weweze kutimiza ndoto zao ambazo wamejiwekea kuwa viongozi wa nchi hapo baadae", alieleza. 

Aidha alisema kuwa Wazazi wajitahidi kuwahimiza Watoto wao  kwenda Skuli  ili waweze kujipatia Elimu nakuondokana na umaskini Nchini. 



Hata hivyo aliwaomba akina mama wasijiweke nyuma katika kugombea Uongozi jambo ambalo lina wasababishia kutopewa kipaumbele katika kutoa uamuzi ili waweze kuwatetea  Wanawake  wenzao.   

"Tunamuona Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanazania ambae ni Dk. Samia Suliuhu Hassan  anavoiongoza Nchi nakuwatetea wanawake wenzake juu  yasuala zima la maendelo", alisema.  

Kwa upande wake Katibu wa taasisi ya Nuru Foundation Zanzibar , iliyopo Gombani Biubwa Yahya Othman alisema kuwa nivyema wananchi wajitolee katika kutoa misaada kuwapa mayatima kwani kufanya hivo ni kwaajili ya Allah  SWT na malipo yake watakwenda yaona kesho Akhera.  

Nae Mwalimu kutoka Madrast_Nnisai Bimkubwa Habibu Sultan alisema kuwa Wazazi wawe karibu na Watoto wao ili kuwafahamisha kuhusu Udhalilishaji wa Watoto ulivo zidi kuenea. 

"Watoto wanadanganywa ni watu kwa kuwapa Pipi au kitu chochote ili watimize lengo lao ambalo wamejiwekea la kuwadhalilisha watoto wetu , " alieleza .  



Nae mtoa nasaha kutoka Madrasatu -Nnisai Maryam Juma Hatibu alisema kuwa ni jambo zuri kupewa misaada  Mayatima wale wote waliondokewa nawazazi wao kwani mtu hajui muda gani yeye ataondoka kwa sabubu kifo kitamgusa kila binadamu.  

"Tutoweni kile ambacho tumeruzukiwa na Allah  SWT kwani hivyo vyote Allah ana habari navyo kama tumeviweka kwenye kibubu au benki" alifafanua  

Aidha alisema kuwa kila mwenye uwezo wakutowa na akafanya ubakhili kwa kuwapa misaada Mayatima kwa ajili ya Allah huyo anajifanyia nafsi yake. 

  Nae msoma Risala kutoka Mdrassa hiyo Khadijja Muhammed Mussa alisema kuwa Mahafali hayo yametayarishwa  na Kamati ya Wanawake kutoka Madarassat -Nnisai ambayo ilianzisha mfuko wa Mayatima kwa kuwapa sare na vifaa ambavyo vitawasaidia katika masomo yao mwaka  ujao.  




Hata hivyo  alieleza kuwa  changa moto kubwa inayojitokeza ni  pale wanapotowa misaada hiyo kwa mayatima kuwa niwengi mfuko wao ukawa haukidhi haja . 

Mfuko huo ulianzishwa Mwaka 2013 wakiwa namayatima 16 hadi kufikia mwaka huu wametowa kwa mayatima 100 Wakiwa Wanawake ni 47 na Wanaume 53.

                                                          MWISHO 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch