Skip to main content

UCHUMI MDOGO ULIMFANYA MWANAMKE AWE KIONGOZI

 



NA AMRAT KOMBO, ZANZIBAR@@@

Binaadamu siku zote hutakiwa ajuwe alipo na wapi anataka kwenda. Katika maisha hii huwa ni ndoto ambayo humpelekea mtu kupitia mengi, baadhi yao yakiwa ni mtihani mmoja baada ya mwengine.

Jambo muhimu ni kutokata tamaa na kuendelea kupambana na pale unapoteleza au kuanguka unapaswa kuinuka na kuendelea na safari huku ukiwa na matumaini ya siku moja utafika huko unapokusudia kwenda.

Bi Huzaima  Ali Hamdani, miaka 51, ambae ni mjasiria mali wa uchoraji piko  na biashara ya vyakula, ni mmoja wa wanawake aliyekabiliana na mithani mingi katika safari yake ya uchoraji aliyoianza 1997.

Kila alipokutana na kikwazo hakukata tamaa, bali aliendelea kupambanana na  kuanza biashara nyengine, ikiwemo ya kuuza urojo, maandazi na chapati, ili kuhakikisha anajipatia kipato cha halali cha kujiendesha kimaisha.

"Kila siku asubuhi nauza urojo, mandazi chapati na juisi na ikifika jioni nauza supu ya utumbo na chapati,"alisema.

Alipomsikia Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Ali Mwinyi, akisema wachoraji watapewa mfuko wa kuendeleza biashara zao hakusita kufuatilia kwa kwenda halimashauri kujaza fomu ambayo imeshafikishwa benki na anayo matumaini  ya kupata mkopo utakaomsaidia kuimarisha biashara yake.

Wakati akiendesha biashara zake alikuwa ameshajiunga katika Chama cha Democrasia na Maendeleo ( Chadema) akiwa mwanachama katika mwaka 1996 na baada ya muda alichaguliwa kuwa kiongozi katika tawi.

Wazazi wake walimuwekea pingamizi hapo awali, lakini hilo halikumkatisha tamaa kwa vile alikuwa na ndoto ya kuwa kiongozi na alifarajika alipoona mume wake hakuwa na pingamizi na akawa karibu naye.

Alipokuwa kiongozi katika tawi akawa bado hakuridhika na nafasi hio na akaingia katika kinyang’anyiro cha kugombea ubunge katika mwaka 2020 na ingawa hakubahatika kuipata nafasi hio hakukata tamaa na kuamini ipo siku ndoto yake itatimia.

"Nilifanikiwa  kuweka mikutano kutokana na biashara zangu,na nikafanya kampeni ya kugombania ubunge katika mwaka 2020, nikabahatika kupata kura 400, japo hazikutosheleza lakini sikuanguka sana na jambo ambalo linanifanya mwakani nigombanie tena ." anasema

SABABU ZA KUINGIA KATIKA SIASA

 Miongoni mwa mambo yaliyomsukuma kuingia katika siasa ni kutaka kusaidia kutataua matatizo wanayokutana nayo wanawanawake katika maisha ya kila siku. Hii ni pamoja na huduma duni za matibabu.

"Hadi leo ukienda katika hosptali kitanda cha wajawazito kimoja wanakaa watu watatu. Hili jambo linanikera na nimeamua nikiwa kiongozi mwenye nafasi ya kusaidia kulitatua nitasimama kidete kuhakikisha usumbufu huu unaondoka’’, alieleza.

Licha ya kutopata nafasi ya kuwa mbunge mwana mama huyu anaendelea kuongoza wenzake kwa kutoa elimu kwa wanawake wenzake ya kujitambua na kujuwa kwamba wanayo haki ya kuwa viongozi.

Pamoja na hayo anashirikiana na vijana na kuwasaidia anapokuwa na uwezo. Mfano mmoja ni wa kuona vijana wanashiriki katika michezo na aliwashaijisha vijana wa jimbo l la Welezo shehia ya Mchokichini, Tumbatu, kwa kuwapelekea mipira na kuwafahamisha umuhimu wa kujihusisha na siasa kwa vile ndio msingi wa maisha yao ya kila siku.



Miongoni mwa mafanikio ya harakati zake za kuongoza wenzake Bi Huzaima ameweza kuwashawishi  wanawake 10 kuingia katika uongozi.

"Nilipoenda Tumbatu waliniomba niwapatie ofsi na kwa vile uwezo wangu bado ni mdogo, nilichanga na kuwapelekea shilingi 300,000 zilizosaidia matengenezo ya ofsi hiyo, ingawa mwisho wa siku hawakunishika mkono katika safari yangu ya kutaka kusonga mbele kwenye uongozi. Hata hivyo sijakata tamaa," aliongeza.

Alisema uzoefu alioupata ni unapofanya kazi kwa bidi wanatokea wenzako wanaokuwa hawafurahii na hukuona kuwa ni mtu unayejiona badala ya kuthamini kile unachokifanya.

Alieleze kusikitishwa kwake na kuona bado jamii inatawaliwa na mifumo dume ambayo humtenga mwanamke na hata kumuona hana haki ya kuingia kwenye safu ya uongozi na miongoni mwa wenye kufanya hivyo ni wanandoa.

"Lakini pia wapo wanawake ambao wamejijengea hofu ya kuingia kwenye siasa kutokana na kuwa na uelewa mdogo na kuona siasa ni kwa ajili ya wanaume pekee yao,’’alieleza.

MAFANIKIO

Miongoni mwa mafanaikio aliyoyapata ni kujifunza mengi kupitia siasa na kuwa mtu anayejiamini na kuwa na ujasiri wa kuweza kuzungumza pahala popote.

Neema Said Mwishehe ambae ni mjumbe wa Baraza kuu la  Taifa kupitia Chadema alikuwa mjasiria mali wa vyakula na kabla ya kuingia katika siasa alikuwa anauza urojo na wakati huo aliwaona wanachama wa Chadema walivyokuwa wanawahamasisha watu. Hapo ndipo  alipohamasika na kujikuta anaingia kwenye siasa katika mwaka 2018 wakati akiwa kijana mbichi wa miaka 18.

Alipojiunga na chama hicho alianza kutumikia nafasi mbalimbali, ikiwemo ya Mwenyekiti wa Shehia ya Kijitoupele na Mwenyekiti wa jimbo kwa upande wa vijana na baaadaye Mwenyekiti wa Wilaya hadi kufikia mjumbe wa Baraza Kuu la Taifa la chama hicho.

Akiwa katika nafasi hizo aliamua kuachana na biashara zake kutokana na a majukumu kuongezeka huku akiwa na shauku ya kujiendeleza kwenye  elimu na siasa.

Alisema miongoni mwa  watu waliomshajihisha kuingia katika siasa ni Huzaima ambae alimuelewa kuwa ni mwanamke mwanamke jasiri, anaejiamni na kuwajibika katika uongozi wake na hali hio ilimpeleeka  kumfanya mmoja wa watu waliokuwa wanampa ushauri.

Hata hivyo,  safari yake ya uongozi haikuwa nyepesi kwani alikumbana na  vikwazo ambavyo wanawake wengi hukutana navyo katika siasa, hasa wale wenye umri mdogo na alipata shida kuwaongoza watu waliomzidi umri.

Alisema miongoni mwa faida aliyoipata katika  chama chake ni elimu ya kupiga vita vitendo vya ukatili na udhalilishaji kwa wananchi na kumepelekea kuwa mstari wa mbele katika mapambano ya kutokomeza vitendo hivyo.

Hivi sasa anajitayarisha kugombania uwakilishi katika jimbo la Kijitoupele kupitia tiketi ya chama chake.

Asiata Said Abdallah ambae ni mueka hazina wa Kanda ya Unguja katika CHADEMA alisema  aligombea nafasi mbalimbali baada ya kushawishiwa na Huzaima ambaye alimuona kuwa ni mwanamke anayependelea maendeleo kwa wanawake wenzake.

Mchungaji wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Shukuru Malonda, alisema mwanamke ana nafasi ya uongozi katika kanisa na kijamii na kutoa mfano wa viongozi wa kike, waliongoza na kuwasimamia watu katika dini ya Kikirsto. Miongoni mwao ni Esta ambae alikuwa Malkia na Debora alikuwa Nabii.

"Katika kanisa letu tumewachaguwa wanawake wawili   na wanaume wanne ambao  ni wachungaji na Wainjilist 12,  wanawake watano na wanaume saba, ndio wanaoongoza kanisa," alisema.

Mratibu  wa kuinua wanawake katika uongozi katika Chama Cha Wandishi wa Habari Wanawake Tanzania  (TAMWA Zanzibar),  Maryam  Ame, alisema wanatoa elimu  kwa wanawake wanaotaka  kuwa viongozi ili wajitambua na kutatua changamoto za kiuongozi.

Alisema hadi wanawake 172 Unguja na Pemba  wamepatiwa mafunzo ya uwongozi ambayo yamewasaidia kutambua vikwazo wanavyoweza kukutana navyo na namna ya kukabiliana navyo.

Aliwanasihi wanawake wanaotaka kuingia kwenye uongozi kutokuwa na hofu kwani hio ni haki yao iliyoainishwa katika katiba na mikataba mbali mbali ya kikanda na kimataifa ambayo nchi yetu imeiridhia na kuamua kuitekeleza.

MWISHO

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch