Skip to main content

TAMWA yajadili na kutathmini maendeleo ya 2023 na kuunda mikakati imara ya 2024


Na Nafda Hindi, Zanzibar @@@@

Chama cha waandishi wahabari wanawake Tanzania TAMWA ZNZ, wamekutana katika mkutano wao wa kila mwaka kutathmini utekelezaji wa shughuli zake kwa mwaka unaokwisha  2023, kujadili maendeleo, changamoto pamoja na kupanga mikakati imara ya utekelezaji wa mwaka ujao 2024.

Mkutano huo wa siku mbili uliofanyika katika ukumbi wa TAMWA uliowashirikisha wafanyakazi wa TAMWA ZNZ akiwemo Mwenyekiti, Wajumbe na wadau kutoka  Asasi  mbali mbali za kiraia.

Mapema akifunguwa mkutano huo Mkurugenzi wa Chama cha waandishi wahabari wanawake TAMWA ZNZ Dk Mzuri Issa amesema udhalilishaji ni janga katika jamii hivyo wanaharakati wa kupinga vitendo hivyo wasichoke na waendelee kujitoa kwa lengo la kuwalinda watoto.

“Udhalilishaji bado upo unaendelea hivyo wanaharakati wasichoke kupambana ili kuwasaidia watoto na wanawake kuhakikisha wanaondokana na vitendo hivyo,” Dk Mzuri Issa.

 Nae Afisa mradi wa kupinga vitendo vya ukatili na udhalilishaji kutoka TAMWA Zaina Salum amesema wanakumbana na changamoto kadhaa katika kupiga vita vitendo hivyo ikiwemo uwajibikaji kwa watendaji wanaosimamia vitendo hivyo hasa katika eneo la utoaji wa hukumu Mahakamani.

“Mahakama bado hawajawa na mfumo bora wa kutoa hukumu katika kesi za udhalilishaji kwa mfano utasikia mashahidi hawakufika mahakamani au mtuhumiwa katoroka ni vitu ambavyo kwa kweli vinarudisha nyuma wanaharakati na jamii kwa ujumla,” Zaina Salum.

Mkufunzi kutoka Idara ya Mawasiliano na Mafunzo ya Habari Chuo Kikuu cha Taifa (SUZA) Imane Duwe amesema vyombo vya habari vitimize wajibu wake kwa kuripoti kwa kutowajibika kwa vyombo vya sheria kuhusiana na vitendo vya udhalilishaji ili wajirekebishe na kufanya ipasavyo.



“ Vyombo vya habari vinajitahidi kuripoti vitendo hivyo lakini bado vitendo vinaendelea hivyo wachukuwe jukumu la kuwakumbusha wajibu wa watendaji kutoka vyombo vya sheria,” Imane Duwe.

Wadau kutoka Asasi za Kiraia wakitoa mchango wao wameipongeza TAMWA kwa kazi nzuri wanayoifanya ya kuisadia jamii kupambana na vitendo vya udhalilishaji na kuziomba Taasisi nyengine kuiga mfano huo kwa lengo la kuisaidia jamii.

“TAMWA ina inafanya vizuri katika kazi zake za kuisaidia jamii na kuonesha njia juu ya mambo mbali mbali ikiwemo vitendo vya ukatili kwa wanawake na watoto,” Wadau.

Aidha Afisa Mradi wa kuwawezesha wanawake kugombea nafasi za Uongozi (SWIL) Maryam Ame Chuom amesema wanatoa mafunzo mbali mbali ya kuwajengea uwezo wanawake kushiriki katika nafasi za maamuzi na tayari wanawake mia moja sabiini, ikiwa Unguja ni mia moja na sabiini kwa Pemba na wameahidi wanawake kujitokeza kwa wingi katika Uchaguzi mkuu wa mwaka 2025.

“Tumetowa mafunzo kwa awamu mbili, awamu ya kwanza ni wanawake 45 kwa Unguja na 35 kwa Pemba na awamu ya pili ni wanawake 55 kwa Unguja na 35 Pemba,” Maryam Ame.

Kwa upande wa Mradi wa haki ya Afya ya uzazi kwa wanawake na wasichana Afisa Mradi huo Zaina Mzee amesema wametowa mafunzo kwa waandishi wahabari hamsini na nane kwa Unguja na Pemba, wanawake ni arubaini na sita na wanaume ni kumi na mbili.

 “Mafanikio tumeyapata kwa waandishi kuibuwa changamoto mbali mbali zinazoikumba sekta ya Afya na wanawake pamoja na wasichana na baadhi yao zimepatiwa ufumbuzi kama kituo cha Afya Wesha Pemba kupatiwa huduma ya maji ambapo awali haikuwepo kabla ya ziara ya waandishi.” Zaina Mzee.

Kwa upande wa Mradi wa KIJALUBA ISAVE, Nayrat Abdula ambae ni Afisa Uwezeshaji wanawake Kiuchumi wakishirikiana na Shirikisho la Jumuiya ya Watu wenye Ulemavu Zanzibar (SHIJIWAZA) Amesema mradi huo umekuja kuwasaidia wanawake wenye ulemavu ambao wameonekana kutengwa kwa muda mrefu

Aidha Sabrina Mwinjuma Meneger mradi wa VIUNGO amesema wamesaidia wanawake wapatao …kwa lengo la kuwawezesha kujiajiri kupitia mradi huo kuondokana na utegemezi hasa kwa vijana na wanawke kwa Unguja na Pemba.

Katika mradi wa VIUNGO umewafikia wanawake elfu tatu mia tisa na tisini na nne  kwa Unguja na Pemba elfu sita mia moja na nane.

Tatu Mtumwa ambae ni Afisa mradi wa kuwajengea uwezo waandishi vijana kuripoti na kuandika habari za wanawake kugombea nafasi za Uongozi amesema wametoa mafunzo kwa waandishi wahabari wapatao ishirini na nne, wanawake ni kumi na tisa na wanaume ni sita, Unguja ni kumi na nane na Pemba sita.

Hata hivyo kitengo cha Habari na Mawasiliano kutoka TAMWA wamesema wamejipanga vyema katika mwaka ujao kuhakikisha wanaitumia fursa ya mitandao ya kijamii ipasavyo kwa lengo la kuboresha utendaji wa Taasisi hiyo na jamii kupata ujumbe wa haraka kwa kile wanachokifanya.

 Kwa mujibu wa Mkuu wa Utawala na Fedha Mohammed Khalid amesema TAMWA imeteleza miradi tisa kwa mwaka 2023 ikiwemo Mradi wa Kuwajengea Uwezo wanawake kugombea nafasi za Uongozi, VIUNGO, Haki ya Afya ya Uzazi kwa wasichana na wanawake,Mradi wa kuwawezesha wanawake wenye ulemavu (ISAVE KIJALUBA), Tumia jukwaa la habari kumaliza Udhalilishaji, Uhuru wa habari, Shajihisha hatua za kitaifa kumaliza Udhalilishaji, Mafunzo kwa waandishi wahabari kumaliza Udhalilishaji na Mafunzo kwa waandishi wahabari vijana juu ya kuandika habari za wanawake na Uongozi.

 TAMWA  ni Jumuiya isiyo ya Serikali ilioanzishwa mwaka 1987, yenye lengo la kujenga Tanzania yenye Amani inayoheshimu haki za kibinadamu inayofanya kazi zake kwa mujibu wa sheria na TAMWA ZNZ ilianza rasmi 2004 hapa Zanzibar kufanya kazi zake za kuisaidia jamii.

 



Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch