Skip to main content

USHAURI WA KISHERIA WA 'CHAPO' WAZAA MAKAAZI YA KUDUMU KWA MJANE

 


HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

ZAKIA Rashid Baraka (36) wa Chanjamjawiri wilaya ya Chake chake, anaetgemewa na watoto sita, sasa amejengewa makaazi ya kudumu na aliyekuwa muume wake, baada ya kunufaika na ushauri wa kisheria, aliyopewa na wasaidizi wa sheri wilaya ya Chake chake.

Mjane huyo, alisema baada ya kuachika na aliyekuwa muume wake na kisha kumtaka ahame ndani ya nyumba waliokuwa wamejenga pamoja kijiji cha Tundaua shehia ya Kilindi wilayani humo, alimua kufuatilia haki yake kwa wasaidizi wa sheria.

Alisema, kisha mwanamme huyo alikutanishwa nae, na kutakiwa kunijenga chumba kimoja, kwa vile alishakataa kumpa chumba kimoja katika nyumba walipokuwa pamoja kindoa.





Akizungumza na mwandishi wa habari hizi, nyumbani kwake Chanjamjawiri, alisema katika ujenzi wa nyumba hiyo anayoishi muume wake kwa sasa alitumia nguvu kazi na fedha taslimu zaidi ya shilingi milioni 1.

Alisema kuwa, alitegemea sana baada ya kuchwa aidha engerejeshewa fedha ama kupewa haki yake ya chumba kimoja, ingawa yote hayo hayakufanyika.

‘’Baada ya kufuatilia haki zangu kuanzia kwa sheha na ofisi ya Mufti Mkuu Pemba, mote nilikwama, lakini nilipopewa ushauri wa kisheria, nilifanikiwa na sasa naishi ndani ya chumba kimoja,’’alieleza.

Zakia alifafanua kuwa, kwa vile mama yake mazazi alishapiga fondesheni kwa ajili ya ujenzi wa nyumba ya familia, ilikuwa rahisi kusimamisha matofali na kuezeka chumba chake kimoja, alichokubaliana na aliyekuwa muume wake.

‘’Ijapokuwa nilizaa nae mtoto mmoja, kati ya sita nilionao, lakini nilihitaji nipate haki yangu, na kwa sasa ameshanikabidhi chumba kimoja kikiwa kimeezekwa,’’alifafanua.

Hata hivyo amewashukuru wasaidizi hao wa sheria, kwa umakini wao wa kufuatilia lalamikoa lake, hadi kulipatia ufumbuzi, ambao ulishindikana katika taasisi nyingine.

Wakati huo huo Zakia, amewataka wanawake wenzake, wasikubali kuchangia wa nyumba au kununua kitu cha thamani pasi na kuandikiana na waume zao.

Sheha wa shehia ya Kilindi Nassor Mohamed Khamis, alisema anaifahamu vyema kesi ya mjane, ambayo anasema hata kamati ya shehia, ilishindwa kumnasihi na kukubaliana na ushauri wa aliyekuwa muume wake.

‘’Baada ya kumuona Mohamed Mohamed (muume), ni mzito wa kutuelewa, nilimataka Zakia (mjane), awasiliane na ofisi ya Mufti Mkuu, ingawa alirudi tena, kwamba hajafanikiwa na kumuelekeza kwa wasaidizi wa sheria,’’alieleza.

Mkurugenzi wa Jumuiya ya Wasaidizi wa sheria wilaya ya Chake chake Pemba ‘CHAPO’ ambae ndie aliyempa msaada wa kisheria mjane huyo, Nassor Bilali Ali, alisema awali, muume huyo alitaka kuwa mzito wa kufahamu, ingawa baadae alikiri na alihadi kumjengea.



‘’Huu unaweza ukawa mfano wa kwanza na mkubwa ndani ya wilaya ya Chake chake, lakini walionufaika na msaada wa kisheria katika maeneo mingine, wapo zaidi ya watu 7,000 kwa mwaka 2023,’’alifafanua.

Hata hivyo, alisema CHAPO inaendelea kumuangalia mjane huyo kwa karibu, na inatarajia kumsaidia zaidi, kumuwekea saruji chini na kumsaidia fikra ya kujenga banda ya vyumba viwili, kando ya chumba hicho, ili kutanua makaazi yake.

Mratibu wa LSF zoni ya Pemba, Hamisa Bakar alisema, LFS ikishirikiana na Idara ya Katiba na Msaada wa Kisheria Zanzibar, imekuwa ikiwawezesha kimafunzo na mbinu, wasaidizi wa sheria, ili kukabiliana na changamoto kama hizo.

Mkurugenzi wa Idara ya Katiba na Msaada wa Kisheria Zanzibar Hanifa Ramadhan Said, alisisitiza kuwa kusema kuwa, ni vyema wasaidizi wa sheria, wanapoibua changamoto, kuzifuatilia hadi upatikane ufumbuzi.

Sheria ya Msaada wa Kisheria Zanzibar nambari 13 ya mwaka 2018, ambayo imekuja kuanzisha Idara ya Katiba na Msaada wa Kisheria, moja ya majukumu yake, ni kumtaka mtoa msaada wa kisheria, kutoa huduma ya msaada wa kisheria, kwa mtu asiyekuwa na uwezo.

                      Mwisho

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch