Skip to main content

WADAU HAKI ZA BINAADAMU PEMBA:' UTEKELEZAJI SHERIA ZA WATU WENYE ULEMAVU BADO KITENDAWILI’

 



NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

WADAU wa haki za binaadamu kisiwani Pemba, wamegundua kuwa Zanzibar inazosheria, kanuni na sera nzuri kwa ajili ya watu wa wenye ulemavu, ingawa changamoto kubwa ni utekelezaji wake kwa vitendo.

Walisema, kwa mfano ipo sheria na sera, inayotaka kila jengo la umma, liwe ni njia maalum kwa ajili ya watu wenye ulemavu, ingawa changamoto ni kutotekelezwa na mamlaka wakati wa ujenzi.

Wakizungumza kwenye kikao kazi, kilichoandaliwa na Mwemvuli wa asasi za kiraia Pemba ‘PACSO’ chenye lengo la kupitisha changamoto za kisheria kwa wanawake, watu wenye ulemavu na vijana, kilichofanyika leo Disemba 16, 2023 skuli ya maandalizi Madungu Chake chake.

Walisema, hata suala la ajira kwa kundi hilo, limewekwa katika sheria kama ilivyo suala la haki nyingine za kibinaadamu, ingawa shida ni utekelezaji wake.

Mmoja kati ya wadau hao, Khalfan Amour Mohamed kutoka Jumuiya kwa ajili ya watu wenye ulemavu wa akili ‘ZAPDD’ Pemba, alisema inashangaaza kuona majengo ya umma, hayana njia za kutembea kwa watu wenye ulemavu.




‘’Hii bado ni changamoto, utakuta jengo la ghorofa la serikali, chini imewekwa njia maaluma ‘rams’ kwa ajili ya watu wenye ulemavu, lakini haikuzingatia ofisi zilizoko juu,’’alisema.

Nae Salim Abdalla Salim, alisema kwa mfano waliandikia barua kadhaa wakati wa ujenzi wa soko jipya la Machomane Chake chake, ingawa hakuna lililozingatiwa.

‘’Leo soko la Machomane limemalizika, kakini bado kwa mtu mwenye ulemavu hasa wa viungo, hawezi kuyatembelea maduka yote yliomo humo, hii sio sababu ya sheria, ni utekelezaji tu,’’alisema.


Kwa upande wake Mwache Juma Abdalla, alisema kama sheria zitatekelezwa kama zilivyo, kundi la watu wenye ulemavu wataneemeka na haki zao.

‘’Sheria zipo nzuri, ikiwemo kuwekwa kwa alama za barabarani, adhabu kwa atakaemuigiza au kumkebehi mtu mwenye ulemavu na hata masuala ya ajira, ingawa shida ni kwenye utekelezaji,’’alieleza.



Nae mshiriki Khadija Sultan, alieleza kuwa, wakati umefika sasa kwa wadau wa haki za watu wenye ulemavu, kuungana pamoja, ili kuhakikisha, vifungu vya sheria vilivyopitishwa vinatekelezwa.

Akifungua kikao hicho, Makamu Mwenyekiti wa ‘PACSO’ Nassor Suleiman, alisema wamekuwa wakizichambua changamoto za kisheria na kisera, zinazowakwaza watu wenye ulemavu, vijana na wanawake.




‘’Lengo ni kuona makundi hayo ambayo ni sehemu ya jamii, wanafaidi haki na fursa zao, kama ilivyo kwa makundi mbali mbali, yaliopo katika jamii husika,’’alifafanua.

Mratibu wa miradi kutoka ‘PACSO’ Mohamed Najim Omar, alisema katika kikao cha kwanza, makundi ya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu, waliibua changamoto za kisheria, ambazo kupitia kikao kitaangaliwa kwa kina.

‘’Kikao cha leo ‘jana’ kitachambua na kuona kwa kina, ikiwa yale yliyoibuliwa hapo awali, ni kweli ni changamoto za kisheria, kisera ama kikanuni,’’alifafanua.



Akielezea yaliojiri yatokanyo na kikao cha kwanza, Mratibu huyo alisema ni pamoja na kifungu cha 116 cha Sheria ya Adhabu nambari 6 ya mwaka 2018, juu ya kupewa dhamana aliyemlawiti mtu mwenye ulemavu wa akili.

Jingine alisema ni kutotekelezwa kwa uwekwaji wa miundombinu rafiki kwenye majengo ya umma, kwa ajili ya watu wenye ulemavu na hasa wa viungo.

Aidha lieleza kuwa, kwa upande wa wanawake ni kutokuwepo kwa sheria maalum, inayozungumzia masuala mbali mbali ya wanawake, ikiwemo suala la uongozi katika taasisi.

‘’Lakini hata kundi la vijana, walitaka kanuni ya kuwa na uzoefu, kama sharti la kuajiriwa hasa kwenye sekta za umma, liondolewe ili kuwe haki, wanaotoka vyuoni moja kwa moja waajirike,’’alieleza.

Mwanasheria Ali Hamad, alisema, hakuna kifungu kinachooelezea uzoefu kama sharti la kupata ajira, ama kukosa ajira na hasa katika sekta za umma.



Aidha alifafanua, hakuna mgongano wa hukumu unaotolewa tofauti ikiwa mtu atapatikana na hatia ya kumdhalilisha mtu mwenye ulemavu, kwani makosa kadhaa ya jinai yanafasiriwa kwenye sheri ya Adhabu.

Akifunga kikao hicho, Mwenyekiti wa PACSO Mohamed Ali Khamis, alisema kuwa, maoni ambayo yatapatikana katika kikao hicho, watayaandika vyema na kuyasilisha kwa Jumuiya ya wanawake wanawake wenye ulemavu Zanzibar, ambao nao watakeleza mradi kama huo, ngazi ya kitaifa.



‘’Kwenye mradi huu PASCO, inatekeleza ngazi ya kanda (zone), ingawa wenzetu wa ‘JUWAUZA’ wanatekeleza ngazi ya kitaifa na kisha maoni hayo, watayafikisha kwa viongozi wa kitaifa,’’alieleza.

Mwisho

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch