Skip to main content

UWT TAIFA, WAMPA KONGOLE MBUNGE ASYA SHARIF PEMBA

 



NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

MWENYEKITI wa Umoja wa Wanawake Tanzania ‘UWT’ taifa Mery Pius Chatanda, amesema aina ya Mbunge wa viti maalum mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, katika kuwakomboa wanawake kiuchumi, ndio mfano unaofaa kuigwa, na wabunge wengine Tanzania.

Alisema, Mbunge huyo ameendelea kutekeleza kwa vitendo maagizo ya UWT taifa, ya kuwakomboa wanawake kiuchumi, kufuatia kukabidhi mashine ya kuzalisha mikate na tosi na fedha taslim, kwa wanawake wa mkoa wake, yenye thamani ya shilingi million 10.5

Mwenyekiti huyo wa UWT taifa, aliyasema hayo leo Oktoba 25, 2023, Micheweni mara baada ya kukabidhi mashine hiyo, kuweke jiwe la msingi ofisi ya ushoni wa nguo na kukabidhi shilingi milioni 1, zilizotolewa na Mbunge huyo.

Alieleza kuwa, anaamini kupitia uwekezaji wa Mbunge huyo, wanawake wa CCM mkoa wa kaskazini Pemba, watapiga hatua kubwa ya kimaendeleo, kupitia njia ya kujiinua kiuchumi.

Alifahamisha kuwa, wakati umefika kwa wabunge wengine wa mikoa ya Tanzania, kufuata nyao za utekelezaji wa Ilani, kama alivyofanywa Mbunge wa viti maalum, mkoa wa kaskazini Pemba.



‘’Kwa hakika Mbunge wetu huyu wa mkoa wa kaskazini Pemba Asya Sharif Omar, ametekeleza kwa vitendo, dhana ya kuwakomboa wanawake kiuchumi, kwani uwekezaji aliyoufanya, umenifurahisha mno,’’alieleza.

Aidha Mwenyekiti huyo wa UWT taifa Mery Pius Chatanda, alisema, Mbunge Asiya Sharif, ni aina ya wabunge wachache Tanzania, wanaotekeleza kwa vitendo, yale waliowaahidi wananchi.



Katika hatua nyingine, amwataka wanawake wa CCM mkoani humo, kuzienzi mashine hizo na ziende moja kwa moja, kuwanufaisha na kupunguza ukali wa umaskini wa kipato.

Alieleza kuwa, hataki kusikia, misuguano, malumbano na ugomvi kupitia uwekezaji huo mkubwa, na badala yake wafanyake kazi, kwa ushirikiano.

Wakati huo huo Mwenyekiti huyo wa UWT taifa, amemtaka Mbunge huyo, kuendelea na kasi yake hiyo, kwani bado wanawake waliowengi, wanakabiliwa na hali ngumu ya kipato.

‘’Mbunge wetu Asya Sharif, endelea kuwakomboa wanawake kiuchumi, ili ile dhana ya wanawake jeshi kubwa, izae matunda kwa kujiongezea kipato,’’alieleza.

Akizungumza kabla ya kukabidhi mashine hizo, Mbunge huyo wa viti maalum mkoa wa kaskazini Pemba, Asya Sharif Omar, alisema, ameamua kuyafanya hayo, ili wanawake wanachama wa UWT wainuke kiuchumi.



Alieleza kuwa, kwa vile aliaminiwa kwa kushika nafasi hiyo, hana budi, kurejesha imani ya kweli kwa wananchi, kwa njia ya kuwaekeza miradi mikubwa na yenye tija kwao.

Alifahamisha kuwa, UWT daima imekuwa ikiwahimiza wao wabunge mara baada ya kumalizika kwa uchaguzi, kurudi kwa wananchi, katika kufikishia miradi mikubwa.

‘’Mheshimiwa Mwenyekiti, huu sio mwanzo, nimeshachangia na kutoa vifaa mbali mbali vya ujenzi, katika ofisi na matawi yetu ya UWT na CCM, kama njia ya kurejesha imani, kwa wananchi,’’alifafanua.



Hata hivyo, Mbunge huyo alisema amechangia shilingi milioni 1, kwa ajili ya uunganishaji huduma ya umeme na ununuzi wa mafeni, kwenye kituo cha ushoni cha UWT kilichopo Micheweni.



Mapema Mbunge huyo, aliwataka wanafunzi wanawake wa skuli ya sekondari ya Chasasa Wete, kusoma kwa bidi, ili kufikia malengo waliojiwekea.

Akizungumza na wanafunzi hao, mara baada ya kukabidhi mchele paketi tano, taula za kike boksi 10, soda boksi 10 na sukari paketi moja vyenye thamani ya shilingi million 1.3, alisema kila mmoja, kwa vile amejiwekea malengo, hana budi kuyafikia.

Hata hivyo, amewataka wanafunzi hao, kuendelea kujilinda na kutoa taarifa, wanapoona viashiria vya udhalilishaji dhidi yao, kutoka kwa mtu yeyote.



Kwa upande wake Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Zanzibar, Riziki Pemba Juma amempongeza Mbunge huyo, kwa uamuzi wake, wa kuwasaidia chakula wanafunzi hao.

Alisema, alichokifanya ni njia moja wapo ya kuwaweka mazingira mazuri wanafunzi hao, kwani suala la chakula na taula za kike, ni mambo muhimu kwao.

‘’Hizi taula zikikosekana, mwanafunzi wa kike huanza kujiskia aibu na wakati mwingine, anaweza kukatisha masomo japo kipindi kimoja au zaidi,’’alieleza.

Nae Mwenyekiti wa UWT wilaya ya Micheweni Mkitu Hassan Mwalimu, amempongeza Mbunge huyo, kwa kutekeleza ahadi yake ya kuwapatia kitega uchumi hicho, ambacho ameahidi kukisimamia.

                          Mwisho

 

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch