Skip to main content

MRADI WA VIUNGO WALETA MAPINDUZI YA KIUCHUMI ZANZIBAR

 



Na Nafda Hindi, Zanzibar @@@@

Uwepo wa mradi wa VIUNGO, mbogamboga na matunda  Zanzibar umesaidia wananchi  kujikita katika sekta ya  kilimo hali iliyoleta mapinduzi ya kiuchumi katika familia zao.

Hayo yamebainishwa na wanufaika wa mradi huo mara baada ya kutembelewa na Kikosi Kazi cha ufundi kwa Taasisi zinazotekeleza mradi huo kwa  lengo la kugunduwa Mafanikio  pamoja na changamoto zinazowakabili wakulima na kuzitafutia ufumbuzi.

Wamesena kuna mafanikio waliyoyapata kupitia kilimo ikiwemo kuimarisha Afya za familia kwa lishe bora kwa kula mboga mboga na kuongeza kipato kupitia mfumo wa biashara.

Ali Shauri ni katibu wa uhirika wa kilimo hai kiitwacho TUMAINI LA KIJANI uliopo Chuini Zanzibar, amesema wao wanatengeneza bustani za nyumbani ambazo zinajumuisha mbogamgoga pamoja na mimea ya dawa lengo likiwa kukibadilisha kijiji kuwa  cha kijani na wananchi kurudi katika uasili wa kutumia dawa za mitishamba jambo linalotoweka kwa vizazi vijavyo.

Amesema  sababu zilizowapelekea kujiingiza katika kilimo hicho ni kuona jamii inakuwa na afya bora kwa kutumia vyakula wanavyovizalisha wenyewe kupitia kilimo hicho sambamba na kupunguza matumizi ya fedha.

“Sababu ambazo zimetufanya kuingia katika kilimo hichi ni kuzingatia suala ziama la afya bora kwa jamii kwa kutumia chakula walichokizalisha wenyewe ambacho ni salama ukizingatia kimezalishwa kwa kutumia teknolojia ya kilimo hai” amesema Ali Shauri

Amesema jamii ya kijiji hicho imeanza kuelewa dhamira ya kilimo hai katika kupunguza matumizi ya fedha na sasa wameondoa dhana ya kuliba bustani za maua na kuanza kulima bustani za mbogamboga.

“kabla hatujaanza mradi huu kulikuwa kuna watu wameweka bustani za maua lakini baada ya kuuelezea mradi huu katika kijiji chetu  wenyi wamepunguza maua na kuanza kulima kilimo cha mbogamboga” Ameongezea

Akiyataja moja ya mafanikio waliyoyapata kupitia kilimo hicho amesema kwa sasa kumekuwa na uhakika ya upatikanaji wa chukula kwenye familia zinazojishughulisha na kilimo hicho.

“Familia zimeanza kuhakikisha upatikanaji wa chakula chao pamoja na kupunguza gharama za matumizi ya mbogamboga” Aliendelea kufafanua

Kwa upande wake Bi. Aviwe Ali Songoro ambaye anajishughulisha na kilimo cha Vanila, Migomba, Pensheni na viungo vingine amesema awali alikuwa akijishughulisha na kilimo cha pilipili lakini mwanga kwake ulianza kung’aa baada ya kunufaika na mradi wa Viungo mboga na Matunda chini ya programu ya Agri-Connect.

“Nilianza kulima pilipili lakini baada ya kukutana na maafisa wa mradi wa VIUNGO, mbogamboga na matunda wakanipatia mafunzo nilianza kujibadilisha na kuingia kwenye mazao mengine” Amesema Bi. Aviwe



Amesema alianza na ukulima wa vanila akiwa na mashina 200, uwezeshi wa mradio huo kwa kumpatia mbegu kwa sasa ana mashina 1,000 na tayar yameshaanza kutoa maua huku kwa upande wa migomba kwasasa anamiliki mashina 2,800.

“Nilianza na mashina 200 ya vanila ila mradi umeniwezesha na kwa sasa nina mashima 1,000 ambayo tayari imeshatoa Maua” Aliongezea

Amesema amekuwa na mafanikio makubwa kupitia shughuli zake hizo za kilimo ambapo zinamsaidia kuendeshea maisha yake ikiwemo suala zima la mahitaji yake ya msingi pamoja na kuwasomesha watoto wake.

“Kwsasa nina uhakika wa mahitaji yangu na hivi sasa nawasomesha watoto wangu mmoja akiwa yupo Chuo Kikuu na namlipia kila kitu” Alisisitiza

Kama inavyofahamika kila penye mafanikio hapakosi changamoto ndio ilivyo pia kwa Bi. Aviwe ambapo yeye amesema uhaba wa maji wa kumwagilia mazao yake imekuwa ndioo kikwazo kikubwa kwake.

Akizungumza kwa niaba ya  Wizara ya Kilimo, Umwagiliaji Mali Asili na Mifugo Afisa Mdhamini  wa Wizara hiyo Pemba Muhandisi, Idriss Hassan Abdulla amepongeza juhudi zinazofanywa kwa pamoja na watekelezaji wa mradi wa viungo Zanzibar na ameahidi kuwa Wizara itaendelea kutoa mashirikiano ya kina ili kuona lengo la kuwawezesha wananchi kwenye kilimo linafikiwa.

“Tumeona umuhimu wa sisi Wizara kuwa na ushirikiano na washirika hawa wa miradi na tumejiridhisha kuwa ni kazi nzuri ambayo inalenga kutoa ajira pamoja na kuimarisha lishe bora kwa wananchi” Alisema Afisa huyo



Nae Meneja Mkuu wa Mradi wa VIUNGO, Simon Makobe amesema wamefurahishwa kuona yale ambayo walikuwa wakiwafundisha wakulima hao wamekuwa wakiyazingatia na kuyafanyia kazi hali iliyoleta mabadiliko kutoka walipokuwa na walipo sasa.

“Tumefurahishwa kuona wakulima wameanza kuwa na mabadiliko kwenye utekelezaji wao mafanikio yameanza kuonekana hasa kwa akina mama” Amesema  Simon Makobe

Vicent Akulumbuka kutoka timu wa washauri mradi wa VIUNGO  Wizara ya Kilimo  Tanzania Bara kutoka   Dodoma amesema katika mradi huo wako katika hatua ya kujitathmini na kuangalia maendeleo ya mradi na changamoto zinazowkabili wakulima ili kuzipatia ufumbuzi.

“Tumeona wakulima wanajisaidia wenyewe kupata masoko lakini ikitokea kuna changamoto ya masoko sisi ndio kazi yetu kutatua changamoto hiyo”  Amesem Akulumbuka

Ziara hiyo imejumuisha  Ushirika wa kilimo cha bustani  (TUMAINI LA KIJANI) kilichopo Chuini, Wilaya ya Magharibi “A”, Mkulima wa zao la Vanila Kizimbani na Kiwanda cha Uchakataji na Usindikaji wa Viungo unaozalisha kiungo cha  majani ya chai (ZANZIBAR ORGANIC PROCESSOR) kilichopo Amani viwanda vidogo vidogo Mkoa wa Mjini Magharibi.

Mradi hua wa Viugmgo unaotekelezwa kwa pamoja na TAMWA,  People Developmend Forum (PDF) na Community Forest in Pemba (CFP) unadhaminiwa na Jumuiya ya Umija wa Ulaya.

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch