Skip to main content

KASORO ZA KISHERIA ZAWAWEKA NJIA PANDA WATU WENYE ULEMAVU KUPATA HAKI ZAO

 



HABIBA ZARALI, PEMBA@@@@

KATIBA ya Zanzibar ya 1984 kifungu 11 (1) imeeleza kuwa binadamu wote ni huru, na wote ni sawa na kila mtu anastahiki heshima ya kutambuliwa  na kuthaminiwa utu wake.

Ikafafanuliwa tena kifungu cha 12 (1) kuwa watu wote ni sawa mbele ya sheria  na wanayo haki  bila ya ubaguzi  wowote , kulindwa na kupata haki sawa mbele ya sheria.

Katiba ya Jamuhuri ya Muungano ibara ya 12 (1) nayo imeelezea kuwa binadamu wote huzaliwa huru na wote ni sawa, na kila mtu anastahiki heshima ya kutambuliwa na kuthaminiwa utu wake.

Tena kwenye Ibara ya 13 (4) ikaweka marufuku kwa mtu yoyote kutobaguliwa na mtu au mamlaka yoyote inayotekeleza madaraka yake chini ya sheria yoyote au katika utekelezaji  wa kazi au shughuli yoyote ya nchi.

Kimataifa upo Mkataba wa haki za watu wenye ulemavu  katika ibara ya 5, imeeleza kutokuwepo ubaguzi, na kwamba watu wote ni sawa mbele ya sheria.

 Mkataba huo pia unapinga aina zote za ubaguzi zilizojengeka katika misingi ya ulemavu, ambapo katika masuala yanayohusu watoto wenye ulemavu maslahi yao yatazingatiwa na yatapewa kipaumbele.

Wakati huohuo, kwenye sheria ya watu wenye ulemavu ya Zanzibar nambari 8 ya mwaka 2022, kifungu cha 30 kinasisitiza wajibu wa kila mtu kulinda, kutetea haki za watu wenye ulemavu, ikiwemo pale wanapovunjiwa haki zao za msingi.

Nacho kifungu cha 31 kikaelezea zaidi huku kikifafanua kuwa, watu wenye ulemavu hawatobaguliwa au kudhalilishwa kwa namna yote kwa sababu tu ya ulemavu wao.



 

KASORO ZA SHERIA

Kifungu cha 151 (1) cha sheria nambari 7 ya mwaka 2018 Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai Zanzibar, imeweka wazi makosa yasio na dhamana.

 

Kati ya hayo limo kosa la ubakaji, kuingilia kinyume na maumbile, kuingilia maharimu, kubakwa kwa kundi, kunajisi mtoto wa kiume, ingawa kasoro ipo kwenye kifungu cha 116.

 

Uzuri wa Kifungu hicho  namba 116 ni kuwa,  kimekataa dhamana kwa kosa la kunajisi mtu mwenye ulemavu wa akili, hata kama mtuhumiwa huyo alikuwa anajua kuwa aliyemnajisi ana ulemavu huo.

Je! Sheria hizi, Katiba na mikataba ya kimataifa inazingatiwa kwa vitendo au hali ikojo!  hapa kisiwani kwetu Pemba?. 

 

KESI ZA WATU WENYE ULEMAVU ZILIZOFUTWA

Mahakama ya Mkoa Chake Chake, Juni 21, mwaka 2022 iliifuta kesi ya Abdalla Khatib, aliyedaiwa kumbaka mtu mwenye ulemavu wa akili, baada ya kutofautiana ushahidi wake alioutoa mlemavu huo wa akili.

 

‘’Ilinibidi kuondoa  kesi maana, muathirika (mwenye ulamevu wa akili), ametofautiana na mashahidi wa upande wa mashataka, juu eneo alilobakwa,’’alisema Hakimu Muumini.

 

Mama mwenye mtoto wake alobakwa, mwanzoni mwa mwaka 2018, kesi hiyo ilichukua muda hadi mwaka 2020 kufutwa kwake sababu ikiwa ni mkanganyiko wa maneno.

 

“Nenda rudi kuanzia kituo cha Polisi hadi mahakamani huku kukiwa na ushirikiano mdogo na kukosekana kwa mkalimani ilibidi mwanangu akose haki yake hata kama kabakwa.” anasema.

 

“Kwa vile mtoto wangu ana tabia ya kupoteza kumbukumbu  siku aliyotoa ushahidi wake, alisema alifanyiwa tendo hilo ndani ya nyumba, ingawa Polisi alitaja kwenye kichaka na kuachiwa huru mtuhumiwa kwa sababu ya mkanyiko wa maneno,’’anasimulia mama huyo.

 

Lakini hata dada wa mtoto wa miaka 16 mwenye ulemavu wa matamshi, wa Wawi Chake chake, anasema baada ya mdogo wake kutoa taarifa za kubakwa na kijana Shaaban Mohamed Issa miaka 35, mtuhumiwa hakukamatwa na baada ya wiki tatu  alikuwa anatembea mitaani.

 


 

WADAU WA KUPINGA UDHALILISHAJI

Ofisa ustawi Wilaya ya Mkoani Aisha Abdi, anasema changamoto kubwa kwa wenye ulemavu mbalimbali baada ya kudhalilishwa, ni kukosa taaluma ya kuyaripoti matendo hayo.

 

Anasema wakati mwengine huwa hawawezi kukumbuka walilosema mara ya kwanza ambapo napo ni sababu ya kukosa haki zao.

 

Hakimu wa mahakama maalum ya kupambana na udhalilishaji  mkoa wa kaskazini Pemba, Muumini Ali  Juma, anasema changamoto inayojitokeza hadi kesi za watoto wenye ulemavu, kutofikia pazuri ni changamoto ya ushahidi.

 

“Wanapohojiwa kituo cha Polisi huwa na ndugu ama jamaa zao huwasaidia kukamilisha maelezo ya mwanzo, lakini kisheria hawaruhusiwi kufika tena mahakamani,’’anafafanua.

 

Anabainisha, kuwa sheria haimtambui mkalimani wa awali aliyesaidia kutoa maelezo kituo cha Polisi, na kisha kufika mahakamani, ikihofiwa kuegemea upande mmoja.

 

Haji Shoka Khamis mwana mtandao wa kupinga udhalilishaji wilaya ya Mkoani anasema, miongoni mwa sababu  ya watu waliobakwa kutovifikia vyombo vya sheria, ni kuwepo kwa  rushwa kwa baadhi ya vyombo vya sheria.

 

Anasema katika kuzifikia suluhu kesi za udhalilishaji hasa za watu wenye ulemavu ni lazima kuwe na utayari kwa jamii na wazazi wenyewe.

 

Mwanaharakati wa msaada wa kisheria na haki za binadamu Siti Habib anasema wanatowa elimu kwa jamii pamoja na kupitia vifungu vya sheria ambavyo havijazingatia usawa wa haki za watu wenye ulemavu.

 

Mohamed Ali Abdalla afisa mtakwimu Wilaya ya Mkoani anasema,dana dana  ya kwenda na kurudi ya kila siku kwenye vyombo husika ikiwemo polisi ni kikwazo kinachoviza kesi za udhalilishaji.

 

Mratibu wa Chama cha waandishi wa habari wanawake Tanzania, Zanzibar (TAMWA-ZNZ) ofisi ya Pemba Fat-hya Mussa Said, anasema ndio maana TAMWA Zanzibar inaendelea kuziibua kasoro za sheria hizo, ili ziangaliwe upya.

 

‘’Sisi baada ya kugunduwa kasoro ya sheria basi hushirikiana na wadau mbalimbali, wakiwemo waandishi wa habari ikiwemo kuwapa mafunzo mbalimbali ili waweze kuzitangaza na  kushajihisha kufanyiwa marekebisho ”anasema.

 

Tatu Abdalla Msellem  kutoka  jumuiya ya Tumaini jipya Pemba, anasema watoto wengi wanaofanyiwa udhalilishaji wakiwemo wenye ulemavu  ni wale ambao wazazi wao tayari wameshatengana.

Anasema watoto wenye ulemavu wanahitaji malezi madhubuti ya kuhakikisha wanalindwa ingawa kwa wazazi waliotengana  ni vigumu kufanikiwa.

“Wako baadhi ya wanaume wanapoona mwanamke kazaa mtoto mwenye ulemavu basi humwacha ama  kumtelekeza hilo hukosesha mtoto haki yake ikiwemo ya elimu,ambayo humsaidia anapofikwa na changamoto za udhalilishaji.

 

 VIONGOZI WA WATU WENYE ULEMAVU

Afisa wa watu wenye ulemavu Wilaya ya Chake Chake chake Mwadini Juma Ali anasema mtu mwenye ulemavu wa akili  ama wasioona  apewe nafasi maalum.

Anasema sheria inaeleza kuwa watu wote ni sawa ingawa inawapa ugumu maradufu watu wenye ulemavu, na kuhimiza watu kutowa ushahidi kwani wasipofanya hivyo hupelekea kesi kufutwa na kuwakoseshwa haki zao.

“Kuna kesi nyingi hufutwa kutokana na watu wenye ulemavu kutokana na mkanganyiko wa ushahidi kwani wengine hukosa kumbukumbu na kupelekea maelezo kutofautiana hivyo ni vyema jamii kutowa ushahidi wa kesi hizo ,”anasema.

Akitoa mfano wa kesi ambazo ilikuwa na tatizo la ushahidi ni ile ya Mtuhaliwa, dereva wa daladala Wesha  ambayo baba mzazi alikataa kutowa ushahidi anasema ingawa zipo nyingi kama hizo.

Mratibu Baraza la Taifa la watu wenye ulemavu Pemba Mashavu Juma Mabruk anasema kinachorejesha nyuma ni rushwa muhali na rushwa fedha.

“Mara nyingi wanaochangia kuharibu ushahidi ni wahanga au familia zao ambao hupewa mbinu za kuharibu ushahidi na watuhumiwa wa kesi hizo na kupelekea kufutwa kwa kesi”, anasema.

Naibu katibu wa jumuiya ya watu wenye Ualbino Pemba Mudathir Sharif Khamis anasema elimu ni kitu pekee kitakachowawezesha watu wenye ulemavu.

Anasema kama watu wenye ulemavu watasomeshwa wataweza kukabiliana na changamoto kadhaa zinazowakabili katika maisha yao ikiwemo kujuwa kueleza kwa kusoma na kuandika wanapofikwa na vitendo vya udhalilishaji.

Mwenyekiti wa jumuiya ya wasioona Zanzibar 'ZANAB' wilaya ya Mkoani Ali Hemed Khalifa aliitaka jamii kuwasimamia watu wenye ulemavu badala ya kuwakandamiza kwani nao wana haki sawa kama wengine.

Anasema hata vyombo vya sheria navyo vitende haki na  viangalie watu wenye ulemavu kwa jinsi ya hali zao na kwasaidia kupata haki zao kwa mujibu wa sheria pale wanapodhalilishwa.

WAZAZI WA WATOTO WENYE ULEMAVU

Mzazi Asha Ahmed wa Mtambile anasema serikali iwawekee adhabu kali wanaowadhalilisha watu wenye ulemavu kwani wanapoachiwa ndio huzidi kufanya matendo hayo.

“Bado sheria inawapa nafasi ya kujipenyeza penyeza wanaowadhalilisha watu wenye ulemavu lakini ni wakati sasa wa kufanyiwa marekebisho sehemu hizo”,anasema.

Kassim Ali wa Mkoani wanasema hawezi kuwa sawa mtu mwenye ulemavu wa akili ama wasiosema na mtu asiye na ulemavu hasa katika kutowa ushahidi.

“Asiye na ulemavu hata aitwe mara kumi atatowa ushahidi lakini mwenye ulemavu kama wa akili ni ngumu hivyo achukuliwe pale aliposema awali”,anasema.

ATHARI YAKE

 Mzazi wa mtoto mwenye ulemavu anasema ni vyema sheria ingewatazama watu wenye ulemavu ili wakaweza kuchukuliwa ushahidi wa awali kwani wengine hawana kumbukumbu za muda mrefu na hatimae hukosa haki zao.

Hakimu wa mahakama maalum ya kupambana na udhalilishaji  wilaya ya Wete Muumini Ali  Juma anasema wanafanya hatuwa mbalimbali ikiwemo kupeleka mapendekezo kwa uongozi husika ya kuhakikisha yanafanyika mabadiliko ya sheria na kuweka mazingira rafiki ili watu wenye ulemavu hasa wa akili waweze kupata haki sawa pale wanapofanyiwa dhalilishaji.

 NINI KIFANYIKE

Wazazi na walezi wasiwe rahisi kuharibu kesi za watoto wenye ulemavu na badala yake wasimamie hadi kupata haki zao.

Sheria  iruhusu na kuwekwe wakalimani wa kutosha ambao watasimamia kesi za watu wenye ulemavu sambamba na  kuwepo sheria ambayo itakuwa na usawa kwa watu wote.

Ingetungwa sheria moja tu ambayo itajumuisha makosa yote ya udhalilishaji, badala ya sasa kuwepo kwenye sheria mbali mbali.

Polisi na Mahakama zisimamie kesi bila kujali huyu ni nani kuanzia uendeshaji mrefu wa kesi, ukusanyaji  na uchunguzi.

Kila kesi iamuliwe na mazingira husika iangalie kufanyika kwa kosa na kuachana na tofauti zinazojitokeza kwenye ushahidi.

Huwenda watunga sheria hawakuwaki kufikiria katika utelekezaji  wa majukumu yao itakuja kutokea kukutana na  kesi ngumu za udhalilishaji ambazo hufanyiwa watu wenye ulemavu.

Hata hivyo kwa dunia ya sasa ambayo inachangamoto ya mmongonyoko wa maadili kila jambo baya ambalo huwezi hata kulifikiria basi hutokea.

Kinachohitajika ni kwenda na wakati kulingana na uhitaji kwa sasa suala la kubadilisha sheria ili kupambana na majanga ya udhalilishaji  na changamoto nyenginezo linapaswa kuzingatiwa kwa umakini na kimkakati mahususi.

  mwisho

 

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch