Skip to main content

USHIRIKA MWANZO MGUMU FURAHA, TUNDA ADHIMU LA MRADI WA KIJALUBA PEMBA

 



NA HAJI NASSSOR, PEMBA@@@@

SHERIA ya watu wenye Ulemavu Zanzibar nambari 8 ya mwaka 2022, kifungu cha 28 (e) kimeweka wazi, haki ya watu wenye ulemavu, kujumuishwa kwenye harakati za uchumi.

Ikaelezwa kuwa, mtu mwenye ulemavu ana haki ya kujitegemea na kujumuishwa katika shughuli za kijamii, kiuchumi na siasa.

Kifungu chingine ni kile cha 30, kinachotoa wajibu wa kila mmoja, kulinda na kutetea haki za watu wenye ulemavu, zikiwemo cha kiuchumi.

Hata kifungu cha 31, kimepiga marufuku, mtu yeyote kumbagua mtu mwenye ulemavu, kwa namna yoyote ile, tena kwa sababu ya ulemavu wake.

Kwenye kifungu cha 42 cha sheria hiyo, kimekataa kumficha mtu mwenye ulemavu, kwa lengo la kumzuia asishiriki katika moja ya haki zake, zikiwemo za kiuchumi.

Mkataba wa kimataifa wa haki za watu wenye ulemavu, Ibara ya 27, ikasisitiza nchi zilizoridhia mkataba huo, lazima ziweke mazingira sawa na wasiokuwa na ulemavu, katika ajira na kujiajiri.

Haya yalikuja kulindwa na Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984, kuanzia kifungu cha 12 (2), kikisisitiza hakutakuwa na sheria itakayokuwa na kifungu, kinachoonesha ubaguzi.

Tena hata kifungu cha 22 (1) (a) kimeainisha kuwa, ni wajibu wa kila mmoja, kujituma katika kazi za halali na zile za uzalishaji mali, ambapo hapa watu wenye ulemavu wakiwemo.



Na ndio maana, Jumuia ya Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania TAMWA-Zanzibar, kwa kuyaona hayo, ikaja na mradi jumuisha wa kijaluba iSAVE ZANZIBAR.

NINI KIJALUBA iSAVE ZAZNIBAR?

Ni mradi jumuishi, unaolenga kuwawezesha watu wenye ulemavu kiuchumi na kijiamini.

Kupitia mradi huu, watu hao wenye ulemavu kwa sasa wameshajengewa uwezo, kuhusu maisha yao wenyewe, na jamii zao.

Maana, lengo kuu hasa la mradi huu wa Kijaluba iSAVE Zanzibar, unaangazia zaidi, kukuza uwezo wa watu hao, kwa kujenga mitazamo chanya, juu ya ushiriki wao, na kujiingiza katika shughuli za kujipatia kipato.





Mratibu wa mradi huo kutoka TAMWA -Zanzibar ofisi ya Pemba, Mohamed Salim Khamis, anasema kipato hicho, hasa kwa aina ya maradi huo ulivyo, ni kupitia katika vikundi vyao vya kuweka na kukopa ‘saccos’.

Mbiznu za utekelezaji wa mradi huo, anasema moja wapo ni kuwawezesha watu hao, kupata kipato, jambo ambalo tayari kwa sasa limeshafanyika.

‘’Jingine ni kuwezeshwa, ili wawe na ushiriki kamili, katika miradi na maendeleo ya jamii, kutokana na mazingira yao,’’anasema.

Mbinu nyingine aliyoitaja, ni kuangalia vikwazo vinavyowakatisha tamaa watu hao hasa katika jamii zao.



‘’Kwa mfano, kama jamii wanamitazamo kuwa, watu wenye ulemavu hawawezi, tutoa elimu, au kama tutagundua wanatengwa, tutaelezea haki zao kwa jamii,’’ anaeleza.

Kwa sasa tayari watu hao wenye ulemavu kupitia mradi huo, wameshaanzishiwa vikundi vya kuweka na kukopa (iSAVE groups).

Baada ya kupewa mbinu za kisasa kwenye vikundi vyao vya kuweka na kukopa, kisha wataunganishwa na tasisi za kifedha kama benki, ili waweza kuomba mikopo.

Walishasema wahenga kuwa, mgagaa na upwa.. wala hali ugali mkavu, hapa msemo huu utasadifu, kwa kundi la watu wenye ulemavu, maana wanagaa gaa kwenye ufukwe wa Kijaluba.

Na hili linaingia akilia, maana walengwa wakuu wa mradi huu, ni watu wenye ulemavu wakiwemo watoto, wanawake, wanaume, kwamba kila 60 kwenye 100 wahusika watakuwa wao.

Akimaanisha kuwa, kwa mfano kila watu 10 wataokanufaika na mradi, basi sita wawe watu wenye ulemavu na wanne wale wasiokuwa na ulemavu.

‘’Kwa hiyo, wanajamii wa wilaya ya Chake chake kwa Pemba na wilaya ya Kusini kwa Unguja, ndio ambao watafikiwa na mradi huu, kwa njia ya majaribio,’’anafafanua.



WATEKELEZAJI MRADI

Mratibu wa Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania TAMWA-Zanzibar ofisi ya Pemba, Fat-hya Mussa Said, anasema, mradi unatekelezwa kwa ushirikiano kati ya shirikisho la Jumuiya za watu wenye ulemavu Zanzibar ‘SHIJUWAZA’ pamoja na TAMWA-Zanzibar.

TAMWA kazi yao kubwa, ni kuhakikisha kila kitakachofanywa ndani ya mradi, jamii inapata taarifa kwa, kuwatumia waandishi wa habari.

‘’TAMWA tunaguswa na haki za watu wenye ulemavu, na ndio maana tukawa washirika wa utekelezaji wa mradi huu, ambao unafadhiliwa na Chama cha watu wenye ulemavu cha Norway ‘NAD’, anafafanua.

Anaona kama jamii ya wilaya ya Chake chake itajali kwa kiasi kikubwa haki za watu wenye ulemavu, mradi huo utatekelezwa kwa mafanikio.

USHIRIKA ‘MWANZO MGUMU’

Ushirika huu wa ‘Mwanzo mgumu’ wenye wanachama 30 jumuishi ambao umaenzishwa Mei 28, mwaka huu lengo likiwa lilelile la kuwakomboa watu wenye ulemavu.

Hapa Mwenyekiti wa ushirika huo, wa kuweka na kukopa, Mayasa Hamad Salim, anasema ushirika huo pamoja na uchanga wake, umeshapiga hatua.



‘’Kwa sasa, pamoja na kuwa kuanza kutoa mikopo kati ya shilingi 100,000 hadi shilingi 400,000 kwa wanachama jumuishi, lakini tayari biashara zimeanza kufanyika,’’anasema.

Anafafanua kuwa, watu wenye ulemavu hawakufikiria kuwa kupitia ushirika wao huo, wengeweza kuwa na uhakika wa kipato, kupitia njia ya kukopeshana.

Katibu wa ushirika wa mwanzao mgumu Khamis Said Massoud, anasema sasa wameanza kukopeshana bidhaa ya sabuni na wameshafanya hivyo mara tano mfululizo.

‘’Unajua kabla ya kujiunga na mpango huu, unaosimamiwa na mradi wa kijaluba, ilikuwa hata sabuni ya kufulia kwa sisi watu wenye ulemavu, haikuwa ya uhakika, lakini sasa ni kawaida mno,’’anaeleza.

Anasema hata wameshatoa mikopo mitatu, yenye thamani ya shilingi 650,000, maana mwanachama mmoja amekopa shilingi 400,000, mwengine shilingi 200,000 na mmoja shilingi 50,000.




Mwanachama wa ushirika huo Fatma Najim Omara, anasema tayari ameshakopa shilingi 200,000 na kununua bidhaa za njugu nyasa, kwa ajili ya kuendelezea biashara yake.

‘’Naamini, kama sio kuwepo wa ushirika huu, leo hii ningehitaji kiasi hicho cha fedha, ningemaliza kijiji chote bila ya kufanikiwa,’’anaeleza.

Malengo yake ya baadae, kwanza ni kukuza biashara yake ya genge yenye viungo vya mchuzi, ili kuhakikisha kuwa na duka kubwa la chakula.

Sahera Mbarouk Suleiman, anasema uwepo wa ushirika huo jumuishi wa kuweka na kukopa, sasa maisha yake ana hakika wa kipato.

Kwa sasa nna hisa 70, zenye thamani ya shilingi 35,000 fedha hizo sio kidogo, maana zinaniwezesha kukopa hadi shilingi 400,000.

‘’Mimi naona mradi wa Kijaluba iSAVE, umechelewa kunifikia, laiti wengekuwepo tokea zamani, ningeshakuwa na uwezo wa kuajiri wengine,’’anaeleza.

Anasema wanaosema watu wenye ulemavu hawawezi kufikia ndoto zao, huyo anaota ndoto za mchana, na akitaka ushahidi wa hilo, wanamkaribisha kijiji cha Furaha Mbuyuni shehia ya Mvumoni.




Kwake biashara yake ya kuuza nguzo za mtumba, anaiona kuelekea kupata mafanikio, kwani licha ya muda mfupi tokea kujiunga na ushirika huo, sasa ameanza kunawirika.

‘’Kwa sasa hata muume wangu akiondoka miezi miwili hadi minne, sina wasiwasi wa huduma za lazima, maana najua kwanza wapi nikakope,’’anaeleza.

Kabla ya kuingia kwenye ushirika huo, anasema hakuwa na uhakika hata wa shilingi 100 kwa siku kuipata, ingawa kwa sasa anaishi kwa amani.

‘’Mimi ni mgonjwa wa sukari na presha, sasa wakati mwengine nilikuwa nahitaji walau shilingi 50,000 kwa ajili ya safari, na kwa wakati huo haikuwa rahisi kupata,’’anaeleza.

Anakumbuka vyema kuwa, hata fedha za michango, ada ya masomo kwa wakati huo, kwake ilikuwa ni mzito kuipata kwa uhakika, licha ya kuwa anae msaidizi katika hilo.

‘’Hata michango kama ya harusi, matibabu, ufiwa, nguo za sikukuu kwa ajili ya watoto, ilikuwa kazi kubwa, ikilinganishwa na sasa,’’anaeleza.

Mshika fedha wa ushirikia huo Amina Said Ali, anasema wanachama hao 30, kwa sasa wamekubaliana kuanzisha biashara ya sabuni.

‘’Kwa hatua za awali, tulijikopa shilingi 34,000 na kununua sabuni paketi 30 na kila mmoja alinunua na kijiingizia faida wastani wa shilingi 13,000, lakini mara ya pili, ya tatu na ya nne faida ilingezeka shilingi 100, ingawa kwa msimu wa tano tumepasta shilingi 15,000,’’anaeleza.

Anasema pamoja na uwepo wa mradhi huo wenye sura ya biashara, ushirika pia umeanzisha kilimo cha mboga za mriba, bamia, bilingani ili kuongeza pato.

‘’Kwa hakika ujio wa mradi huu, sisi watu wenye ulemavu na wengine, tunaowawakilisha watoto wenye ulemavu, tunaona TAMWA na wafadhili wao, hawakukosea,’’anaeleza.




Mzazi Juma Maasoud Said anaemwakilisha mtoto wake mwenye ulemavu, anasema sasa watu wa kundi hilo, wamekuja kukombolewa kwa vitendo.

‘’Nilikuwa nishamkatia tamaa mtoto wangu wenye ulemavu mchanganyiko, juu ya hatma ya Maisha yake, lakini leo sasa nna hakika kupitia mpango huu, maisha yake yameanza  kuimarika,’’anasema.

Kwa sasa ana hakika ya kupata sabuni na huduma nyingine kama mboga mboga, wakati wote, kufuatia mpango ulioandaliwa ndani ya ushirika wao.

Kupitia ushirika huo anasema sasa ameshajua njia za kujikwamua na umaskini wa kipato, ikiwemo kufuga, kupanda mboga kwa ajili ya biashara na Kuanzisha biashara ndogo ndogo.

‘’Unajua elimu waliotupa wenzetu TAMWA, kupitia mradi huu wa iSAVE Zanzibar sasa, haikuniongoza kwenye ushirika pekee, lakini hata, nikiwa peke yangu sasa najiamini,’’anaeleza.   









HATUA ILIYOFIKIWA

Tayari waalimu wasimamizi wa vikundi vya kuweka na kukopa wameshapewa mbinu za kwenda kuihamasisha jamii, na hasa kundi la watu wenye ulemavu, kuanzisha vikundi vya kuweka na kukopa.

Mwalimu wa mafunzo hayo Bakar Haji Bakar kutoka TAMWA-Pemba, aliwaeleza wasimamizi hao ngazi ya shehia, wahakikishe, hata kwenye uongozi wa vikundi kipaumbele ni watu wenye ulemavu, jambo ambalo kwa sasa lipo.

‘’Kwa mfano wale viongozi sita wa mwanzo, katika kila kikundi, watu wanne, wawe ni watu wenye ulemavu, maana pia mradl huu unalenga kutoa fursa za uongozi kwao,’’anasema.

Kumbe mradi huu utakapotia nanga Disemba 2024, kutoka pale ulipoanza Novemba 2022, watu wenye ulemavu kwa wilaya ya Chake chake, wewe wameshaiva kiuongozi.

Kupitia mradi huu wa majaribio, utaona kuna wananchi 1876, wakiwemo wanawake 1,122 na wanaume 750, kutoka wilaya za Chake chake Pemba na Kuisni Unguja, ndio wanaonufaika.

Chakuzingatia tu ni kuwa, kila watu 60, kati ya 100, watakuwa ni wenye ulemavu mchanganyiko, tena waliomo kwenye shehia za wilaya ya Chake chake kwa Pemba na au wilaya ya Kusini Unguja.

Watu hao, watawezeshwa kupitia vikundi maalum vitakavyoanzishwa katika kila shehia ya wilayani humo, ambapo kila kikundi, kitakuwa na wastani wa wanachama kati ya 25 na wasiozidi 30.

Afisa Utawala kutoka Shirikisho la jumuiya za watu wenye ulemavu Zanzibar ‘SHIJUWAZA’ kisiwani Pemba Aisha Abdalla Juma, yeye amefurahishwa, na ujio wa mradi huo.

Upande mwengine Mwezeshaji wa vikundi vya watu wenye ulemavu ‘CRP’ Fatma Abrahman Ali wa shehia ya Ole wilaya ya Chake chake, anaesimamia vikundi tisa, vyenye wanachama wastani wa 25 hadi 30 kwa kila kimoja.

Aidha mradi huo ulioanza mwaka 2022, ukitarajiwa kumalizika mwaka 2024, utakwenda kushughulikia vikwazo vinavyowarudisha nyuma, watu wenye ulemavu.

Kwa sasa mradi huu, anatekeleza wilaya ya Kusini Unguja na Chake chake kwa Pemba, kama eneo la majaribio, ambapo walengwa wakuu ni watu wenye ulemavu wakiwemo vijana, watoto kwa asilimia 60 na 40 na watu wengine.

                               Mwisho      

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch