Skip to main content

WANANCHI TUMBE PEMBA WAKATA TAMAA FIDIA ZAO

 



NA HAJI NASSOR, PEMBA::

WANANCHI wa shehia za Tumbe Magharibi na Mashariki wilaya ya Micheweni Pemba, wamesema wameshakata tamaa, juu ya kulipwa fidia za vipando vyao, vilivyoharibiwa na Shirika la Umeme la Zanzibar ‘ZECO’ wakati lilipokuwa likipelekea huduma ya umeme soko la samaki Tumbe.

 

Walisema uharivu huo ambao umefanywa tokea mwaka juzi, na kufanyia uhakiki mara mbili, lakini kutokana na muda kuwa mrefu, hawana tena tamaa juu ya kulipwa fidia zao.

 

Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi kwa nyakati tofuati, walisema wamekuwa wakipewa ahadi zisizotekeleza na mlipaji, ambae ni wizara ya Uchumi wa Buluu zaidia ya mwaka mmoja na nusu sasa.

 

Mmoja kati ya wananchi hao Halima Haji Khalid (90), alisema aliharibiwa Miembe, Mibirimbi, Mifenesi, mihogo na migomba ingawa hadi sasa alichopewa ni ahadi.

 

‘’Mimi mmoja kati ya waathirika wa kuharibiwa vipando vyangu, wakati ZECO linasafisha njia kwa ajili ya kupeleka huduma ya umeme soko la samaki Tumbe, lakini hadi leo sijalipwa.’’alieleza.

Nae Ali Kale alisema, pamoja na kuharibiwa kwa vipando vyake alivyokuwa akivitegemea mfano minazi na mifenesi, lakini hadi sasa hajapata fidia zake.

 


Nae Khadija Makame Shamata, alisema haamini tena kuwa kuna siku atalipwa fidia yake, kutokana na kupewa ahadi hewa kila muda kutoka wizara ya Uchumi wa buluu.

 

‘’Tupo zaidi ya wananchi 35 ambao tuliharibiwa vipando vyetu vichanga wakati ZECO inapeleka huduma ya umeme soko la samaki Tumbe, lakini hadi sasa hatujalipwa,’’alieleza.

 

Kwa upande wake Aisha Issa Mjaka, alisema alielezwa kuwa watalipwa fidia zao wakati wowote, ingawa kutokana na muda kuwa mkubwa, kwa sasa hana tena tamaa.

 

Kaimu sheha wa shehia ya Tumbe Mashariki Omar Ali Omar alikiri kuwepo kwa shida hiyo, na kusema mara ya mwisho uongozi wa uchumi wa Buluu Zanzibar uliwaahidi kuwalipa fidia wananchi hao mwezi Mei mwaka huu.

 

‘’Kikao cha mwisho kilifanyika mwezi Aprili mwaka huu, ndani ya soko la samaki la Tumbe, baina ya waathirika na uongozi wa wizara ya Uchumi wa Buluu na Uvuvi, na ahadi ikatolewa kuwa mwezi Mei watalipwa, lakini hadi sasa bado,’’alieleza.

Alisema taarifa za kuwa wananchi wa shehua yake hawajalipwa fididi hizo ameshazifikisha kwa uongozi wa wilaya ya Micheweni, kwa muda mrefu sasa.

 

Mkuu wa wilaya ya Micheweni Mgeni Khatib Yahya, alikiri kuwepo kwa taarifa hiyo, na kusema tayari ameifikisha shirika la umeme la Zanzibar ‘ZECO’ ofisi ya Pemba.

 


Alisema, mara ya mwisho aliahidiwa kuwa, mpango wa kulipwa kwa fidia hizo umeshawekwa sawa na wakati wowote wananchi hao watalipwa.

 

‘’Ni kweli wananchi wa shehia za Tumbe Mashariki na Magharibi walioharibiwa vipando vyao, wakati wa upelekaji umeme soko la samaki Tumbe hawajalipwa, na taarifa hizi nshazifikisha ZECO,’’alieleza.

 

Meneja wa shirika la Umeme la Zanzibar ZECO tawi la Pemba Mohamed Juma, alikiri kuwa deni hilo kwa wananchi hao halijalipwa, ingawa wao sio wahusika.

 

‘’Sisi ZECO tulipewa kazi ya kufikisha huduma ya umeme soko la samakini Tumbe na wizara ya Uchumi wa Buluu na Uvuvi, na hao ndio tuliokubaliana kuwa walipe fidia,’’alieleza.

 

Meneja huyo alieleza kuwa hata wananchi wanalijua hilo, kuwa walipaji sio ‘ZECO ‘bali na wizara ya Uchumi wa Buluu na Uvuvi, kama makubaliano yalivyofikiwa.

 

Afisa Mdhamini wizara ya Uchumi wa Buluu Pemba Dk. Salum Mohamed Hamza, alikiri kuwa hadi sasa fidia hiyo haijalipwa, ingawa nia bado ipo.

 

Alisema kwa sasa wanaisubiri wizara ya Fedha na Mipango Zanzibar, maana ndio walipaji wakuu wa madeni yote ya serikali, kwa mujibu wa maelekezo ya ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali.

 

‘’Sisi tunaisubiri wizara ya fedha, baada ya kumaliza taratibu zao, kama watutingizia sisi fedha tutawalipa fidia zao wananchi, na kama watalipa wenyewe pia sawa,’’alieleza.

 

Aidha alieleza kuwa, wastani wa shilingi milioni 60 hadi 70 ndio ambazo zikadiriwa kulipwa na hasa baada ya kufanya tathmini ya mara ya pili, ambayo ya mara kwanza ilikuwa na makosa kadhaa.

 

‘’Wamo baadhi ya wananchi watalipwa katia ya shilingi milioni 4, wengine hadi 6, na hii itawashangaaza wananchi, maana wao walitarajia kupata kidogo, lakini kwa tathimini ya mtathimini mkuu kutoka wizara ya Ardhi fidia zimeongezeka,’’alieleza.

 

Sehemu eneo la kuuzia samaki la soko hilo lilifunguliwa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi Julai 26, mwaka huu.

                        Mwisho

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch