Skip to main content

KILANGI: MCHAKATO MAREKEBISHO SERA YA MAJI WAIVA



NA SALMA LUSANGI::

KATIBU  Mkuu Wizara ya Maji, Nishati na Madini ( WMNM) Joseph Kilangi amesema Wizara yake ipo katika mchakato wa kuifanyia marekebisho sera ya maji ili iendane na wakati uliyopo sasa.  

 

Akizungumza  katika kikao cha pamoja   nilichofanyika jana katika ofisi ya Mamlaka ya Maji safi na Mazingira Dodoma (DUWASA)  ambapo kikao hicho amekusudia kujitambulisha kwa viongozi wa Wizara ya Maji ya SMT baada ya uteuzi wa makatibu wa wakuu uliyofanyika June 30, 2022 .      

 

Alisema wizara ya MNM inaendelea na kazi ya kupitia sera ya maji ili Sekta ya maji iweze kuleta tija kwa Serikali angalau wananchi wachangie huduma ya  maji.   


Alifahamisha kwamba  lengo kuu, la wizara yake  kuwataka wananchi wachangie maji ni kuipunguzia Serikali ya Mapinduzi Zanzibar ( SMZ) mzigo mkubwa wa kuendesha bure sekta hiyo kutokana gharama ziliyopo.  


Katibu mkuu huyo alifafanua  kwamba gharama za kuendesha huduma ya maji ni kubwa ikiwemo, uchimbaji wa visima, ulazaji wa mabomba, ujenzi wa matangi pamoja na huduma ya umeme hivyo uchangiaji wa wananchi utasaidia kuleta ufanisi katika kuendesha huduma hiyo.       


Alisema hata hivyo SMZ bado inaendesha huduma zingene bure, ikiwemo  afya na elimu hivyo amewaomba wananchi wa Zanzibar kuunga mkono katika kuchangia huduma ya maji.      


Aidha katibu Mkuu Kilangi aliwashukuru viongozi wa Wizara ya Maji ya SMT  kwa mapokezi mazuri pamoja na kuendeleza mashirikiano  kupitia sekta hiyo. Alisema  vikao vya pamoja vinaonesha inshara njema katika kulipatia ufumbuzi tatizo la maji Zanzibar.    

  


" Najua vikao vingi, vimefanyika, hadi tumepata fedha za Uviko 19, zimetusaidia katika uchimbaji wa visima, mmetupa mtaalamu Dkt Subira ameweza kutusaidia kuhusu Groundwater,  Naibu Katibu Mkuu msituache mkono, kwani tukiendeleza mashirikiano, Muungano tutakua tumeutendea haki" Alisema Kilangi.  

 Naye Naibu katibu Mkuu Wizara ya Maji    ( SMT) Nadhifa Kemikimba  alimshukuru Katibu Mkuu Kilangi kwa uamuzi wake huo wa kufunga safari ya kutoka Zanzibar na kwenda Dodoma kwaajili ya kujitambulisha kwa lengo la kuendeleza mashirikiano baina Wizara bili hizo.        


 Aidha alishauri kwamba kupitia vikao vyao vya mashirikiano wawe na jitathimini kwa kulinganisha kabla  ya masharikiano walikuaje na baada ya mashirikiano ufanisi umeongezeka kwa kiasi gani! ili hata wakiandika ripoti kwa viongozi wa juu ioneshe uhalisia .    


Kwa upande wa wakurugenzi wamependekeza katika   vikao vya pamoja kuwe na utaratibu wa kuwaalika maafisa manunuzi wa pande zote mbili ( SMZ na SMT) ili waweze kuwasilisha changamoto zinazowakabili katika vitengo hivyo. Alisema kwani bado  kuna changamoto kwa upande wa manunuzi na zinahitaji kupatiwa ufumbuzi.   

 Katibu Mkuu WMNM Joseph Kilangi katika safari yake hiyo aliambatana na watendaji wake akiwemo Mkurugenzi Mipango,  Sera na Utafiti Dkt Maryam Issa,  Afisa, Mipango,  Afisa Utumishi na Afisa Uhusiano, na  alikaribishwa na Naibu Katibu Mkuu, Mhandishi Nadhifa, wakurugenzi na maafisa wengine wa wizara ya Maji ( SMT). 

                    MWISHO 


Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch