Skip to main content

WAANDISHI PEMBA WAPEWA MBINU KUILINDA MITANDAO YAO

 

 



AMINA AHMED MOH'D-PEMBA.

Waandishi wa Habari Kisiwani Pemba wameaswa kuzidisha umakini katika utumiaji wa mitandao ya kijamii  ikiwa ni pamoja na kuweka ulinzi katika utumaji  wa taarifa zao ili zisiweze  kudukuliwa.

Ushauri huo ulitolewa Oktoba 27, mwaka 2022 na  Mwenyekiti wa Klabu ya waandishi wa Habari kisiwani Pemba (Pemba Press Club)  Bakar Mussa   Juma  alipokuwa akifungua mafunzo ya siku moja ya  Usalama wa Mitandao (Digital Security) kwa waandishi wa habari wanaotumia zaidi  mitandao ya kijamii   katika kazi zao  yaliofanyika  katika ukumbi wa  Ofisi hizo Misufini Chake Chake.

Alisema   mitandao imekuwa ikipeleka ujumbe  kwa haraka  zaidi  kwa jamii   ukilinganisha na vyombo vyengine vya habari  vilivyopo nchini lakini kumekuwa na changamoto mbali mbali ambazo kama hawakuwa makini wanaweza kujiingiza katika matatizo wasio yategemea kwa vile kunaweza kukatokea wahalifu wakaharibu dhamira zao.



Alieleza kuwa watumiaji wa mitandao wanawajibu wa kujifunza na kuelewa namna ya kujilinda kwenye  mitandao yao ili isiingiliwe na wahalifu   ambapo kunaweza kupelekea kutokuwepo kwa   usalama  kwa  waandishi wa habari   kutokana na baadhi ya wahalifu kutumia  mitandao  hiyo  kudukua taarifa  pamoja  kufanya uhalifu .

"Kudukuliwa  taarifa kwenye mitandao ya kijamii  aidha za mwandishi mwenyewe lakini hata kazi za kihabari zinazofanywa na kutumwa katika mitandao , kunaweza kukajitokeza upotoshaji kwa kupata taarifa nyingi zisizo sahihi ( Fakenews) ambazo hazijafanyiwa uchunguzi wa kina  na hivyo kuwa ni chanzo cha matatizo hata usalama wa nchi “, alisema.

Aidha Mwenyekiti huyo wa Pemba Press Klab aliwataka  waandishi hao  kuyafanyia kazi mafunzo watakayopatiwa  juu  ya  suala hilo la usalama wa mitandao ili kuweza  kujiweka salama  katika utumiaji wao ambao kwa sasa umekuwa ni changamoto kwa waandishi wa habari.

"Kujiepusha na  mitandao ambayo haiko salama  na kutofautisha fake news, kutasaidia kuwaepusha kujiingiza kwenye matatizo musioyatarajia ,ambapo mutafunzwa namna ya kuweza kulinda taarifa zako na mitandao yenu munayofanyia kazi na hapo mutaweza kufanyakazi bila ya wasi wasi wowote”, alisisitiza.



Kwa upande wake  Mratibu  wa Klabu  hiyo ( Pemba Press Club) Mgeni Kombo  Khamis aliwataka washiriki wa mafunzo hayo kufikisha elimu watakayopatiwa  kwa waandishi wengine ambao wamekosa fursa hiyo  kutokana na sababu mbali mbali.

Alisema kuwa utumiaji wa mitandao umekuwa na kasi kubwa kutokana na uharaka wake, lakini hakuna mafanikio yasiokuwa na changamoto zake hivyo ni lazima wasiwe wachoyo kuyapeleka mafunzo hayo kwa waandishi wengi zaidi.

“ Klabu haina uwezo wa kuwakusanya waandishi nyote munaotumia mitandao ya Kijamii ,lakini kwa umuhimu wake tumeona tuwaite nyinyi muliohudhuria ili muwe mabalozi kwa wengine  hivyo itumieno fursa hii mulioipata”, alisema Mgeni.

Mratibu huyo aliwataka Waandishi wa habari ambao hadi sasa hawajaamuwa kujiunga kuwa wanachama wa Pemba Press Club, kufanya hivyo ili kuweza kupata fursa mbali mbali za mafunzo hususan yanayotolewa na UTPC na Klabu wenyewe.

Akitoa  Elimu ya Usalama wa mtandao   kwa waandishi hao mkufunzi  aliepatiwa  Mafunzo hayo na Umoja wa Klab za Waandishi wa Habari Tanzania (UTPC) Haji Nassor Mohamed pamoja  na mambo mengine   alisema kuwa usalama wa mtandao ni kujikinga  na hatari zinazoweza kujitokeza kwa watumiaji   sambamba na kujilinda na hatari zilizokusudiwa na wahalifu na zisizokusudiwa kusambazwa.



"Kuna uhalifu katika mitandao ambao umepangwa na ule uliokuwa haukupangwa  yapo mambo  mbali mbali usioyahitaji unaweza ukayakuta katika simu au Komputa yako  , masuala ya kuingilia email ya mtu kumuazima mtu mwengine, afungue, yote hayo ni hatari na ili ujikinge ni lazima ujue usalama na ulinzi wake "alisema.

Aliwataka waandishi hao kujiengeza zaidi katika kujifunza mambo mbali mbali yanayoweza kuwa kinga ya kujilinda na udukuzi wa taarifa zao kwani kumekuwepo na wahalifu wanaotumia mitandao hiyo kwa maslahi yao ama kwa dhamira ya kumchafuwa mwandishi ama mtumiaji wa mtandao fulani.

Haji Nassor ambae pia ni Mwandishi wa habari wa Shirika la Magazeti ya Serikali aliwasisitiza waandishi hao kutumia mitandao yao kwa ajili ya kuihabarisha jamii mambo mbali mbali na sio kwa matumizi ambayo hayana tija kwa jamii na taifa kwa ujumla ikuchukuliwa kuwa wananchi waliowengi wanafuatilia kusoma habari za mitandao kila wakati.

“ Waandishi wenzangu ni wambie sio kila anaemiliki Mtandao ni mjuzi wa matandao hivyo zitumieni simu  ama Komputa zenu kujifunza zaidi mambo ambayo yanaweza kukuweka katika hatari hata ya maisha yako binafsi”, alieleza.




Waandishi hao walipata fursa ya kujifundisha  mambo mbalimbali   ikiwemo ya usalama wa mitandao ikiwa ni pamoja  na  kujikinga dhidi ya hatari  (Safety) kujikinga  binafsi   ili kuweza kuwa salama katika matumizi ya mitandao kwa vyombo vya mitandao (Security) .

Hata hivyo walifunzwa juu ya tathmini ya hali ya hatari pamoja na mbinu za kujua  program  hatarishi na zisizo hatarishi zinazotokana na matumizi mabaya ya Mitandao.

 

                               MWISHO.    

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch