Skip to main content

VIFARANGA VYA SAMAKI VYAWACHELEWESHEA WAFUGAJI PEMBA NDOTO ZA UCHUMI WA BULUU

 




NA HANIFA SALIM, PEMBA

UCHUMI wa buluu ni shughuli za kiuchumi zinazohusu matumizi bora ya rasilimali za bahari kwa ajili ya kuimarisha au kukuza pato la wavuvi na taifa.

Kuna nafasi kubwa na nzuri ya kuifanya Zanzibar na Tanzania kwa ujumla kuwa na uchumi mzuri zaidi kwa kuifanyia maarifa zaidi ‘Blue Economy’.

 

Elimu na mafunzo katika uchumi buluu inapaswa kuratibiwa vizuri ili kukuza ukuaji wa sekta ya bahari, kwa hivyo unaweza kutoa moja ya fursa kubwa zaidi kwa mafanikio ya biashara.

Sio kitu cha ajabu kwa Zanzibar kusikia neno uchumi wa buluu, ambapo ikiwa na maana kuwa ni shughuli zote za uendelezaji na ukuzaji wa uchumi kupitia matumizi bora ya rasilimali zote muhimu za bahari.

Dhana nzima ya uchumi wa buluu ni pana, ambayo imebeba shughuli zote za msingi zinazofanywa katika bahari kama vile, uvuvi wa aina mbali mbali ikiwemo raslimali zote zitokanazo na bahari.

Ikiwemo uvuvi wa kibiashara na usio wa kibiashara katika kina kirefu na kifupi cha maji, shughuli za usafirishaji baharini, shughuli za utafutaji na uchimbaji wa maadini na mafuta baharini.

Makala hii itazungumzia namna ya upatikanaji wa vifaranga vya samaki Zanzibar utakavyoimarisha sekta ya uchumi wa buluu kwa wafugaji wa samaki kwa kuongeza pato la taifa.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi amesema, kutokana na juhudi kubwa zinazochukuliwa na wafugaji wa samaki Serikali ina kila sababu ya kuwasaidia kwa kuwapatia mitaji wanayoitaka.



Akiwa kwenye ziara yake aliyoifanya mwezi Julai mwaka huu, ambapo alipata fursa ya kutembelea kilimo cha ufugaji wa samaki kwa kikundi cha “Siri fish Farm” Pujini Kibaridi Chake Chake Kisiwani Pemba.

Dk. Hussein anasema, bado kunahitajika nguvu za ziada kutoka Serikalini kuwasaidia wafugaji wa samaki, hivyo aliitaka wizara inayohusika kuhakikisha wanawapatia vifaranga kwa muda mfupi ujao.

Iwapo wananchi wataitumia bahari vizuri itawapatia kipato wataondokana na umaskini kwani kuna shughuli nyingi za kufanya ikiwemo uvuvi, kilimo cha mwani, ufugaji wa samaki, kamba, majongoo bahari na mengineyo.

“Changamoto zenu ni nyingi tumezichukuwa na kuzifanyia kazi, tumeambiwa kuna vikundi nane ni vyema tukavisaidia vikundi hivi kuliko kuanzisha wengine,”anasema.

Anasema, Serikali imekuwa ikiwawezesha wavuvi kwa kuwapatia maboti na zana za kisasa ili wavue vizuri sambamba na wakulima wa mwani kuwapatia boti za kubeba mwani wao pamoja na mitaji.

‘’Wananchi wa Zanzibar watakapowezeshwa vizuri katika suala la uchumi wa buluu, wataweza kuondokana na umasikini, na sasa anaona ulazima wa kusaidiwa upo,’’.

WIZARA YA UCHUMI WA BULUU NA UVUVI ZANZIBAR

Waziri wa wizara ya Uchumi wa Buluu na uvuvi Zanzibar Suleiman Masoud Makame anasema, wizara imeshafikia makubaliano na mwekezaji, ambae ataekeza uzalishaji wa vifaranga.

Aliwaaminisha wafugaji wa samaki wa Zanzibar, kuwa wamekubaliana awali mwa mwezi Agost watakuwa wameshasaini mkataba wa utekelezaji.

Baada ya kusaini mkataba huo wa utekelezaji, wanategemea kwamba changamoto ya vifaranga inayowakabili wafugaji wa samaki kuondoka kabisa.

Anaeleza, wao kama wizara jitihada zao ni kuzalisha vifaranga, jambo ambalo ndio kipaumbele chao cha kwanza ambavyo vitawawezesha wafugaji kuzalisha fedha nyingi kupitia shughuli zao wanazozifanya.

IDARA YA MAENDELEO YA UVUVI PEMBA

Mtaalamu kutoka Idara ya Maendeleo ya uvuvi Pemba Haji Omar Haji, anasema katika kutengeneza ajira za wananchi imeona ni vyema kuziendeleza jitihada ambazo wanazifanya siku hadi siku.

Aliwahakikishia wafugaji kwamba, serikali imeshaandaa mpango wa kuzalisha vifaranga vya samaki utakaosaidia kufikia malengo ya wafugaji hao ambayo wamejiwekea.

“Niwatoe hofu kuhusu suala la upatikanaji wa vifaranga wafugaji wa samaki karibuni tatizo hili, linaelekea kutatuka kwani serikali yetu imeshatenga fedha za mradi huo ambao utakua ni chachu ya mabadiliko kupitia sekta yetu hii,” anasema.

KIKUNDI CHA “KICHAKAA SI CHANGI”

Katibu wa Kikundi hicho cha ufugaji wa samaki kilichopo Kiuyu Minungwini wilaya ya Wete Othman Bakar Shehe anasema, kikundi chao ndio cha mwanzo kilichoanzisha wazo la ufugaji wa samaki kwa Zanzibar, kikiwa na wanachama 26.

Upatikanaji wa vifaranga umekua ni tatizo kwao, jambo ambalo awali walikua wakisaidia kuwapatia hata wenzao ambao waliamua kufanya shughuli hizo kwa kuwauzia na hata kuwagaia.

Mahitaji yao ya sasa ni kupata vifaranga vya aina tofauti ikiwemo Sato, Kambare na Mwatiko, ambapo mwanzo walianza na samaki aina moja ya Mwatiko, ingawa kwa sasa wanalengo la kupiga hatua nyengine kubwa za kiufugaji.

Miongoni mwa changamoto nyengine zinazowakabili ni kufanyiwa matengenezo makubwa ya shamba lao la kufugia samaki wakati ikiwa hali ya uchumi walionao kwa sasa ni dhaifu.

Anasema serikali imewaunga mkono sana wafugaji wa samaki lakini bado wanahitaji elimu ili wafuge kwa kuendana teknolojia ya sasa pamoja na kuwapatia vifaranga vya aina mbali mbali.

“Tuliamua sisi wenyewe kufuga samaki tulikaa kuwaza wazo tukakubaliana, tulikwenda serikalini kuomba ruhusa tukaruhusiwa hatukua tumeona sehemu yoyote ni ubunifu wetu wenyewe,” anasema.

 

Mabwawa yao ni nane yana ukubwa wa kiwanja kimoja cha mpira, nusu kiwanja na mengine yana ukubwa mita 25 ambayo yanauwezo wa kuchukua samaki zaidi ya 8,000 hadi 50,000 kwa wakati mmoja.

KIKUNDI CHA ‘SIRI FISH FARM’ PUJINI

Mwenyekiti wa kikundi cha ufugaji samaki ‘Siri Fish Farm’ kilichopo Pujini Kibaridi Ahmed Salum Issa anasema, moja ya malengo yao ni kujiajiri, kujipatia kipato halali.

Anasema, walijenga matumaini makubwa ya kuengeza mabwawa mapya 12 ya samaki pamoja na kufanya ukarabati wa kujenga miondombinu, ingawa kwa sasa wanakabiliwa na ukosefu wa vifaranga.

“Jambo hili lina tunavunjika moyo kwani tunalazimika kufuga samaki aina ya Mwatiko, ambao vifaranga vyake ni vya kubahatisha jambo linalopelekea kuwa na idadi ndogo ya samaki na kushindwa kufikia malengo,” anasema.

Mahitaji yao ya sasa ni kupata vifaranga zaidi ya milioni 1, ambavyo vitakidhi mahitaji yao, kutokana na changamoto hiyo inawavunja moyo kwani idadi ya samaki walionao ni ndogo ukilinganisha na ukubwa wa shamba lao.

KIKUNDI CHA ‘MAPAMBANO’ SIZINI

Mwenyekiti wa kikundi cha ufugaji wa samaki cha Mapambano shehia ya Sizini wilaya ya Micheweni Pemba Khalfan Hamad Khalfan anasema, zaidi ya shilingi 15 zimetumika kwa ujenzi wa mabwawa yao ya kufugia samaki.

Mpango wao ni kuzalisha samaki wengi kwa ajili ya biashara ingawa wanakabiliwa na changamoto ya upatikanaji wa vifaranga vya samaki ambavyo vinarejesha nyuma juhudi zao.

“Tuliingiza samaki zaidi ya 3,500 tuliwachanganya na kamba lakini tulijikuta tunapata hasara kubwa wakati wa mvua, samaki wengi walipotea kwani hatukua na taaluma kwamba mvua inaweza kupoteza rasilimali zetu,” anasema.

Mabwawa yao ni 14 ambayo ya uwezo wa kuchukua samaki 40,000 lakini kinachowarejesha nyuma ni upatikanaji wa vifaranga vya samaki kwa upande wa Zanzibar nzima.

“Bei yetu kwa kilo moja ya samaki ni shilingi 1000 tunapovua samaki wetu soko letu linakua kubwa tunaingiza fedha nyingi, faida nzuri na wala hatupati hasara kwa hii bei,” anasema.

SOKO



Wenyeviti na Makatibu wa vikundi hivyo amesema, suala la soko halina changamoto kwao kama ilivyo kwa upatikanaji wa vifaranga vya samaki.

Wanasema, endapo serikali itawapatia vifaranga vya samaki ambavyo vitakidhi mahitaji yao watapiga hatua kubwa kwenye sekta ya uchumi wa buluu kwao na kwa taifa.

                                     MWISHO.

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch