Skip to main content

RC KUSINI PEMBA AIKOLEZA 'SPEED' KAMATI MAANDALIZI SIKU 16 ZA KUPINGA UKATILI

 



NA HAJI NASSOR, PEMBA:::

MKUU wa mkoa wa kusini Pemba, Mattar Zahor Massoud, amesema ana imani na kuiamini kamati maalum ya maandalizi ya kuelekea kilele cha siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia kisiwani Pemba.

 

Alisema, kamati hiyo imejipanga vyema na kutokana na shughuli ambazo wamezipanga kuzifanya zinaweza kuwa chanzo kizuri kwa kufikisha ujumbe kwa jamii husika.

 

Mkuu huyo wa mkoa ameyasema hayo mbele ya kamati hiyo ofisini kwake mjini Chake chake, wakati akizungumza na kamati hiyo, kuwasilisha mapendekezo ya shughuli zinazotarajiwa ndani ya siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia.

 

Alisema, shughuli zilizopangwa ikiwa ni pamoja na matembezi, makongamano, elimu kwa jamii, vipindi vye redio na tv ni dhahiri kuwa elimu hiyo itasambaa na kuwafikia walengwa.

 

Alieleza kuwa, kamati hiyo imelenga hasa kule ambako serikali imekuwa ikitilia mkazo kila siku, juu ya elimu na kujadili changamoto katika kutokomeza matendo hayo kwa wanawake na watoto.

 

‘’Kwanza nichukue nafasi hii kuipongeza kamati hii ya maandalizi kutokana na maono yenu, ambayo yametoa dira ya namna ambavyo mtaifikia jamii, tukiwa kwenye shamra shamra za kuelekea siku 16 za kupinga ukatili wa kujinsia,’’alieleza.

 

Katika hatua nyingine Mkuu huyo wa mkoa wa kusini Pemba Mattar Zahor Massoud, ameridhia baadhi ya shughuli ambazo zilipendekezwa kufanywa na kamati hiyo, ikiwa ni pamoja na kuzungumza na vyombo vya habari na matembezi kama eneo moja la uzinduzi.

 

Hata hivyo, ameitaka kamati hiyo kuwasiliana na mkuu wa mkoa wa kaskazini Pemba, ili nae atoe ushauri na mapendekezo yake, katika kuona shughuli hiyo inanoga.

 

Mapema Katibu wa kamati hiyo Khalfan Amour Mohamed, mara baada ya kuwasilisha mpango kazi wa kamati hiyo, alisema hayo ni mapendekezo ya awali ya kamati.

 


Alisema, mara baada ya kamati kukutana, iliamua kumpelekea mapendekezo hayo, ili kwanza ayapate na kisha atoe ushauri wake katika kufanikisha shughuli nzima.

 

Hata hivyo Katibu huyo alisema wameyachukua na kuyafanyia kazi mapendekezo yote yaliotolewa na Mkuu wa mkoa ikiwa ni pamoja na kuangalia uwezekano wa kupunguza shughuli.

 

‘’ Ni kweli katika jambo ambalo mkuu wetu wa mkoa alitushauri na tunaona ni sahihi ni kupunguza shughuli, na hizo chache ambazo tumezipanga kuzifanya, tuchaguwe wawasilishaji wanaokubalika,’’alisema.

 

Mjumbe wa kamati hiyo Tatu Abdalla Msellem, alisema mapendekezo waliyopewa na Mkuu wa mkoa watayafanyiakazi, maana yanalengo la kuimarisha shughuli hiyo.

 

Nae mjumbe wa kamati hiyo Asha Mussa Omar, alisema watajipanga vyema ili kuona shughuli hiyo inafanikisha kama walivyokusudia.

 

‘’Kwanza tunampongeza mkuu wa mkoa kwa ushauri ambao ametupa katika kuona tunaendeleza shughuli za kuelekea siku16 za ukatili wa kujinsia,’’alieleza.

 

Siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia ni kampeni ya kimataifa ya kupinga ukatili dhidi ya wanawake, ambapo kampeni hii hufanyika kuanzia tarehe 25 Novemba na kumalizika tarehe 10 Desemba ya kila mwaka.

 

Siku hiyo ilianza kuadhimishwa rasmi mwaka 1991, siku hii inaongozwa na Kituo cha kimataifa cha Wanawake tarehe 10 ilichaguliwa rasmi kuwa siku ya kilele cha maadhimisho haya ikiambatana na siku ya haki za binadamu duniani.

 

                           MWISHO  

      

 

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch