Skip to main content

WANANCHI PEMBA WAWAPA USHAURI WA BURE VIONGOZI WA UMMA

 



NA HAJI NASSOR, PEMBA

WANANCHI kisiwani Pemba, wamewaomba viongozi wa ofisi za umma, kupunguza mikutano ya ndani ya nje ya ofisi, kwa siku ambazo wamezitenga wenyewe, kwa ajili ya kukutana na wananchi, kusikiliza malalamiko yao.

 

Walisema zipo ofisi za umma, zimejiwekea utaratibu wa kukutana na wananchi kila wiki mara moja au mbili, ingawa hata kwa siku hizo, imekuwa shida kuwapata.

 

Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi, walipofika ofisini kulalamika, walisema viongozi wa ofisi za umma, wamejiwekea utaratibu wa kukutana nao, ingawa kwa baadhi yao imekuwa changamoto.

 

Mmoja kati ya wananchi hao Nassor Salim, alisema wamekuwa wakiitumia siku ya Jumanne na Alhamis, kumfuata mkuu wa wilaya ya Chake chake, ingwa changamoto ni mikutano isiyokwisha.

 

‘’Wakati mwengine, anaingia kiongozi mwenzake anatumia zaidi ya saa mbili au tatu na sisi tunaendelea kusubiri bila ya kujua wakati gani tutampata,’’alieleza.

 

Nae Asha Issa Nassor, alisema tatizo hilo lilimkumba wiki mbili zilizopita, baada kufika ofisi ya mkuu wa wilaya ya Chake chake, bila ya kukutana nae.

 

‘’Bahati mbaya hata tulipomuuliza katibu wake muhutasi, alisema Mkuu wa wilaya ametoka kidogo, ingawa alitimiza saa nne, bila ya kurudi na mimi nikarudi Ndagoni,’’alieleza.

 

Nao Is-mail Ali Khamis na Rukia Mohamed Hamad, walisema njia pekee kwa viongozi hao, ni kupunguza safari, mikutano na vikao na kutumia siku hiyo, kwa ajili ya kuwasikiliza.

 

Hata hivyo alisema, hata ofisi ya mkuu wa mkoa kuna siku maalum ya kukutana nae ingawa, mara nyinyi unaonana na Katibu tawala wake.

 

‘’Sisi wananchi shida yetu ni kukutana na mkuu wa Mkoa, lakini utaulizwa mara mia moja, na mwisho unaambiwa leo mkuu wa mkoa hayupo, unakutana na Katibu tawala,’’alilamikia.

 

Mkuu wa mkoa wa kusini Pemba Mattar Zahor Massoud, alikiri kuwepo kwa changamoto hiyo, na kusema hawapendi kuwakimbia wananchi, lakini wakati mwengine majukumu huingiliana.

Alieleza kuwa, ni kweli wakati mwengine viongozi hao wakiwemo wakuu wa wilaya, wamekuwa hawapo ofisini kwa siku ambazo wamewatengea wananchi, lakini hakuna mwananchi anarejeshwa.

 


‘’Nimekuwa nikiwaambia viongozi wenzangu, kuwa hata siku ambayo sio iliyoko kwenye ratiba, kama wananchi wapo wawasikilize, na mimi kwenye ofisi yangu, nimetoa maagizo hayo pamoja na kuweka namba ya simu ya 0733008787 ya kupokea malalamiko,’’alieleza.

 

Aidha Mkuu huyo wa mkoa alisema, pamoja na kwamba amejiwekea utaratibu wa kila Jumanne wa kukutana na wananchi, lakini ameweka utaratibu wa kila mwisho wa mwezi kuzungumza na wananchi.

 

‘’Kila mwisho wa mwezi huchukua shehia tano za mjini Chake chake kuzungumza nao kwenye mkutano wa wazi, uwanja Tenis, lengo ni kusikiliza malalamiko ya wananchi,’’alieleza.

 

Mkuu wa wilaya ya Chake chake Abdalla Rashid Ali, alisema ni kweli kuwa, kwa baadhi ya wananchi hulazimika kukosa kukutana nao, kutokana na kuingiliana kwa majukumu.

 

‘’Inawezekana siku kama ya Jumanne na Alhamis ambayo mimi ndio siku za kukutana na wananchi, pengine nisiwepo ofisini maana hutokezea mizozo baina ya wananchi na hulazimika kuifuatilia,’’alieleza.

 


Hata hivyo Mkuu huyo wa wilaya alisema, suala la kukutana na wananchi sio siku mbili pekee, bali hata Jumapili, kwenye mikutano na jamii na wakati mwengine hata kwa njia ya simu, fursa hiyo ipo.

 

Hivyo amewataka wananchi wanapokuwa na changamoto wasisubiri siku mbili zilizotengwa katika wiki, bali wakati wowote milango ya ofisi yake, iko wazi.

 

Kwa upande wa mkuu wa wilaya ya Micheweni Mgeni Khatib Yahya, alisema baada ya kuona siku moja ya kazi haikidhi haja kwa wananchi, amejiwekea utaratibu mwengine.

 

‘’Kwa sasa kuanzia saa 1:00 hadi saa 3:00 asubuhi kila siku ya kazi, ni muda wananchi na mimi huingia kazini saa 12:45 asubuhi, ili kuwasubiri wao,’’alifafanua.

 

Katika siku za hivi karibuni, ofisi kadhaa za umma zimejiwekea utaratibu wa kila wiki mara moja au mbili, kukutana na wananchi, wakati kwa Rais wa Zanzibar Dk. Hussein Ali Mwinyi hukutana na waandishi wa habari kila mwisho wa mwezi.

                                        Mwisho   

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch