Skip to main content

WAANDISHI WA HABARI WAHIMIZWA KUANDIKA HABARI ZA UCHUNGUUZI

 


HABIBA ZARALI, PEMBA

WAANDISHI wa habari nchini, wametakiwa kuacha kuandika habari kimazowea na  badala yake wajikite kuandika habari za uchunguzi (Investigative Journalism), ili kuweza kufichua maovu na kuisaidia jamii, kupata matokeo chanya.

Kauli hiyo imetolewa Septemba 09, mwaka 2022 na Mkufunzi Mwandamizi kutoka shirika la Intenews Tanzania Alakok Mayombo alipokuwa akifungua mafunzo ya siku tatu ya uandishi wa habari za uchunguuzi, yaliyoendeshwa na shirika hilo kwa njia ya kielektroniki ya zoom,  uliowashirikisha waandishi wa vyombo mbalimbali vya Tanzania bara na visiwani.

Alisema waandishi wa  habari walio wengi hawaandiki habari za uchunguzi ingawa ni eneo muhimu lenye nguvu katika kuasaidia kufanya maamuzi mazito na  kuleta mafanikio ya haraka.

Alifahamisha kuwa ni vyema kwa waandishi wa habari kuwa habunifu kwani habari hizo zinahusu mtu mmoja mmoja na wakati mwengine serikali hivyo kila mmoja anauwezo wa kujikita katika eneo hilo.

“Nguvu za habari za uchunguzi ni kubwa na mara nyingi habari hizi zinakuwa zimejificha na waandishi hamutakiwi kulala fichueni kwa malengo mema”,alisema.

Kwa upande wake mkufunzi kutoka shirika la Intenews Erick Kabendera alisema mbali na changamoto nyingi walizonazo waandishi wa habari bado wana jukumu la kuwa na moyo wa kuandika habari za uchunguzi.

Alisema kusudio la habari za uchunguzi si la kumripua mtu isipokuwani kuonesha uhalisia wa jambo na kuweza kuleta matokeo yenye faida kwa jamii na nchi nzima.

“Waandisi tusianagalie tu kuandika stori kwa ajili ya kesho pekee na hizi za uchunguzi lazima tuhakikishe tunaziandika kwa lengo jema kabisa”,alifahamisha.

Katika hatuwa nyengine kabendera alishauri waandishi wa habari hizo kuwa na uwelewa wa kitaalamu ,waweze kujifunza , wafanye uchunguzi kwa kina (research), waweze kuwa na vyanzo vingi vya habari, vyanzo nyaraka ili kupata habari zenye ukweli .

“huwezi kuwa mwandishi mzuri wa uchunguzi kama kama hutokuwa na moyo wa ustahamilivu na kuweza siri ya kile unachokifanya,hivyo ni lazima kila mmoja kutimiza wajibu wake na sio kuleta woga”alisema.

Akizungumza na waandishi hao baada ya kumaliza mkutano huo mkufunzi mkuu wa Internews Temigunga Mahondo alisisitiza kuzingatia maadili, na kutenda haki kwa waandishi wa habari ili kujenga uwajibikaji unaofaa kwa jamii.

Alisema iwapo waandishi wataandika habari hizo za uchunguzi zitasaidia kuondowa maovu ikiwemo ya rushwa,udhalilishaji na maovu mengine mengi yanayoikabili jamii na nchi kwa ujumla.

“Licha ya kuwa kazi hizi ni hatari lakini kama waandishi watakubali kunyamazishwa na wasipofichua basi uwajibikaji hautokuwepo”,alieleza.

Wakitowa shukrani zao kwa shirika la Intanews  washiririki wa mafunzo hayo walisema mafunzo hayo ni muhimu kwani kufanikiwa kuandikwa kwa habari hizo ni mafanikio ya kuleta matokeo mazuri hasa kwa jamii isiyo na sauti.

Hata hivyo waliliomba shirika la Internews kuendelea kutowa mafunzo mbali mbali kwa waandishi wa habari kwani kunawawezesha kufanya kazi zao kwa ufanisi zaidi.

                                     Mwisho.

 

 

Comments