Skip to main content

NURU FOUNDATION YASAIDIA WATOTO WANAOISHI MAZINGIRA MAGUMU

                  



Na Mwandishi wetu OMKR                                                                          

Mwenyekiti wa Nuru Foundation Mama Zainab Kombo Shaib ambae pia ni mke wa Makamu wa Kwanza wa Rais amesema Jumuiya yao imeamua kujikita zaidi kumuangalia mtoto wa aina yeyote hasa yatima na anaeishi kwenye mazingira magumu

Ameeeleza hayo wakati alipofanya ziara ya kuwatembelea watoto wenye vichwa maji na mgongo wazi katika kituo chao cha nyumba ya matumaini iliyopo eneo la Mwanakwerekwe ndani ya Wilaya ya Magharibi B.

Mama Zainab amesema kumlea mtoto mwenye kichwa maji na mgongo wazi kunahitaji elimu kwa mzazi na walezi ili kufahamu namna ya kumlea hatimae nae mtoto akuwe katika mazingira mazuri yaliyo salama katika hali zote

Ameahidi kuwa taasisi ya Nuru Foundation ina kila sababu kuona inawasaidia kielimu kwa kutafuta njia za kupata ufadhili na kupata vifaa visaidizi pamoja na kumuandaa kisaikolojia mama au familia yenye mtoto mwenye ulemavu wa aina hii ili waweze kujikomboa na kujihudumia kiuchumi.

Aidha amesema kuwa Taasisi ya Nuru Foundation pia ina jukumu la kumuwezesha mwanamke ambae kwa kawaida ndie mlezi anaekuwa karibu sana na watoto hivyo taasisi hio itaanza rasmi kutoa mafunzo kwa akina mama wenye watoto wenye ulemavu na mazingira magumu ili waweze kuwa na mipango mizuri ya kujiinua kimaisha.

Mwenyekiti huyo wa Taasisi ya Nuru Foundation ameikumbusha jamii kuwa na utamaduni wa kubadili matumizi ya vyakula na kuzingatia ulaji vyakula vyenye afya ili kulinda afya ya mwili hasa kwa akina mama wanapokuwa wajawazito na

Pia amewakumbusha akina baba kuwa karibu na wake zao hasa wakati wa ujauzito pamoja na kusaidiana ulezi mama anapojifungua kwani mtoto ni mtoto ila mwenye ulemavu anahitaji uangalizi zaidi

Nae Katibu wa Umoja wa wenye vichwa maji na mgongo wazi ndugu Hussein Moh’d Saleh ameishukuru Taasisi ya Nuru Foundation kwa kuwa ni taasisi ya mwanzo kuwatembelea na kutoa msaada ambao kwa sasa wanauhitaji



Hussein amesema nyumba ya matumaini inahitaji ushirikiano mkubwa na Serikali, jamii na taasisi zisizo za kiserikali na wafanya biashara ili kuweza kutatua kwa pamoja changamoto zinazowakabili ikiwemo pempas, suala elimu, vifaa visaidizi, chakula, wataalamu na kuandika miradi

Nao akina mama na walezi wa watoto wenye vichwa maji na mgongo wazi wameelezea changamoto wanazozipata kutoka kwa wanajamii ikiwa ni pamoja na kudharauliwa na familia, majirani, watoto kupewa majina mabaya na kuachika kwa waume

“siku moja alikuja jirani yangu kuniangalia akaniuliza nimeambiwa umezaa mtoto mlemavu nikamwambia ndio lakini baada kumuona akaniambia huyo si mtoto ni jini niliumia sana sana”alisema mama huyo ambae hakutaka jina lake kutajwa.



Kina mama hao wamesema bado jamii hawajaelewa kuhusu watoto wenye ulemavu wenye vichwa vikubwa na mgongo wazi hivyo wameomba jamii wapatiwe elimu ili kuondosha unyanyapaa na dharau.

Kikao pia kilihudhuriwa na Katibu wa Umoja huo Omar Kaiza Omar ambapo Mama Zainab amekubali kuwa mlezi wa umoja huo na kukabidhi zawadi ya Box 20 za mchele lishe na Pempas kwa ajili ya wale wanaofika katika nyumba yao mara wanapotoka hospitali baada ya kupata matibabu katika hospitali ya Mnazi Mmoja na wale wanaosubiri matibabu

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch