Skip to main content

'FENS' ZA NYUMBA ZISIATHIRI UKUWAJI WA MTOTO: WANAHARAKATI PEMBA


                 


NA HAJI NASSOR, PEMBA::::

WANAHARAKATI wa haki za watoto kisiwani Pemba, wamewataka wazazi na walezi, wanaomiliki nyumba zilizozungushwa kuta ‘fens’ kuwapa muda watoto wao kuchangamana na wenzao, ili kucheza pamoja, ikiwa ni sehemu moja wapo ya kukuza ubongo wao.

Walisema, njia moja na rahisi ambayo haihitaji gharama katika kumkuza mtoto ni kumpa haki ya kucheza na wenzake wasioishi pamoja, ili kupata habari na matukio ya mtaani.

Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi juu ya njia rahisi ya kukuza ubongo wa mtoto, wanaharakati hao walisema, wazazi wasipokuwa makini wanaweza kudumaza akili na ukuaji wa watoto wao.

Walisema, akili ya mtoto haijengwi kwa chakula bora, gari ya kwendea skuli, uzuri wa nyumba pekee tu, bali njia nyingine rahisi ni kuwapa fursa watoto, kuchangamana na wenzao katika michezo mbali mbali.

Mwanaharakati Khamis Uledi Khamis, amesema mtoto anapofungiwa ndani kwa madai ya kuepushwa kupigwa na wenzake, ni kudumaza ubongo na kusinyaa ufahamu wake.

‘’Inawezekana wazazi wanamaisha mazuri na nyumba kubwa yenye ukuta na mbwa mkali, lakini kama mtoto hawakumtoa nje kucheza na wenzake, atanyemelewa na udumavu wa kuduma,’’alieleza.

Mwanaharakati Aisha Hemed Khamis wa Chake chake, alisema mtoto anapopata taarifa kutoka nje ya nyumba yao, huwa rahisi kutanua akili na ufahamu wake mara moja.

‘’Kadiri mtoto anapochangamana na wenzake wa nyumba za jirani au mtaa wa pili, na ufahamu wake ndivyo unavyoongezeka mara dufu,’’alisisitiza.

Afisa Ustawi wa Jamii wilaya ya Chake chake Rashid Said Nassor, alisema wazazi waliowengi wenye uwezo, wanadhani ni dhambi kubwa, watoto wao kuchangamana na kucheza na watoto wengine.

Alieleza kuwa, kadiri mtoto anavyokwenda masafa yenye usalama kwa ajli ya kucheza na wenzake, vivyo hivyo na akili yake hupanuka kwa haraka.

Mkuu wa wilaya ya Chake chake Abdalla Rashid Ali, akizungumza hivi karibuni, aliwataka wazazi na walezi pamoja na kuwapa fursa watoto wao kucheza na wengine, hata wao wajitengee muda kushirikana kwa michezo.

‘’Ipo michezo kama vile mdako, kupigana mito, mpira, kurusha chungwa, kupangwa kokoto kwa mfumo wa picha na kung’waruziana macho kwa njia ya kutishana mzazi na walezi wanaweza kucheza na watoto kama sehemu ya uchangamshi,’’alieleza.

Nae Mkuu wa Idara ya Ustawi wa Jamii Pemba Omar Mohamed Ali, amesema haki ya kucheza kwa mtoto, inatambuliwa na sheria ya mtoto nambari 6 ya mwaka 2011, hivyo ni wajibu kwa wazazi kuitekeleza kwa vitendo.

‘’Sheria inataka watoto wapewa haki ya kucheza na wenzao, sasa kama kuna wazazi wanafungia kwenye mageti, wanaweza kuwa chanzo cha kusinyaa kwa akili yao.

  Nae Msimamizi wa kitengo cha lishe Wilaya ya Chake Chake, Harusi Masoud Ali, akizungumza hivi karibuni, amewakumbusha wazazi na walezi, kuwapatia lishe bora watoto wao.

Waziri wa Afya Zanzibar Nassor Ahmed Mazrui, alisema yapo mambo ambayo jamii wanatakiwa kuyafanya, ili kuwa na kizazi bora cha hapo baadae.

‘’Ni nafasi kwa wazazi na walezi, pamoja na kuwapa haki watoto wao kushiriki michezo mbali mbali, lakini wajenge utamaduni wa kuwashauri watoto kwa mambo yanayowahusu,’’alieleza.

Mzazi Is-mail Ali Juma, amekiri kuwa, wamekuwa wakiwafungia watoto wao kwenye kuta ‘fens’ kutokana na uwepo wa majanga kadhaa kwa watoto.

‘’Mtoto ukiwa humuoni dakika 30, tayari wasi wasi, sasa mimi huwafungia, lakini pia huwatoa nje kucheza nawenzao pale nikiwepo,’’alieleza.


Mjumbe wa baraza la watoto shehia ya Mwambe Hija Omar Ussi na mwenzake wa Mkoani Hamida Issa Machano, waliwakumbusha wazazi kuwa, suala la kucheza kwao halina mbadala.

''Wazazi na walezi wetu wamekuwa wakitengea muda wa kucheza na kupumzika, na sisi ni sawa na binaadamu mwengine yote hayo tunayahitaji,''walisema.

Nae Aisha Haji Mohamed wa Machomane Chake chake, alisema huwa wanafanya hivyo, ingawa kwa ule muda ambao wazazi wapo nyumbani.

Muwezeshaji kwenye mafunzo ya Kitaifa ya Sayansi ya Malezi, Makuzi na Maendeleo ya Awali ya Mtoto ‘SECD’ Everlyne Okeyo, yaliofanyika mkoani Dodoma Tanzania anasema, watoto wanakosa ukuaji mzuri wa kutengeneza ubongo wao, kwa kule wazazi kutowapa muda nafasi ya kucheza.

Katika hatua nyingine, Everlyne alisema, ubongo wa binadamu una nyuroni bilioni 100, na ndio maana mtoto mara anapozaliwa, huwa na asilimi 25 ya ubongo wake ni mtu mzima.

‘’Mtoto anapofikia mwaka mmoja, hufikia asilimia 60, wakati miaka miwili huwa na asilimia 75 na kuanzia miaka minne hadi sita, hubeba asilimia 90 ya uwelewa,’’alieleza.

Akizungumza kwenye ufunguzi wa mafunzo hayo, Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum wa Tanzania bara Dk. Dorothy Gwajima, aliwataka waandishi wa habari, kuifikisha kwa jamii, dhana ya malezi ya kisayansi ‘SECD.

                             Mwisho

 

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch