Skip to main content

RISITI ZA KIELEKTRONIKI MWARUBAINI KUTUNISHA MFUKO WA SERIKALI, WANANCHI WAKUMBUSHWA KUZIDAI

 



HABIBA ZARALI, PEMBA::::

 

MAENDELEO ni mabadiliko yanayoonekana kuimarisha katika nyanja mbali mbali za maisha, ikiwemo za uchumi, sayansi, historia, falsafa na hata za kijamii.

 

Kupitia msemo wa mjenga nchi ni mwananchi na nvunja nchi ni mwananchi, inaonesha dhahiri kuwa, hali nzuri ya upatikanaji wa huduma na nyenzo zilizo bora, haziwezi kuja wenyewe bila wananchi kuwa na utayari.

 

Kwa maana hiyo basi, ulipaji wa kodi, utowaji na kudai risiti unapouza na kununua bidhaa, ni moja ya utayari huo wa kufikia maendeleo endelevu ya nchi.

 

Kodi hiyo Serikali, imekuwa ikiitegemea kujipatia mapato yake, hutekeleza miradi mbali mbali huduma za kijamii ikiwemo afya, elimu, maji safi na salama, miundo mbinu ya umeme, barabara na nyengine ambazo ni muhimu kwa wananchi.

 

Ni dhahiri kwamba, kwa sasa dunia imo kwenye katika mabadiliko ya sayansi na teknolojia, jambo ambalo linatufanya na sisi tuwe macho, ili tusibakie nyuma na mabadiliko hayo.

 

Zanzibar kama ilivyo nchi nyengine, zinazoendelea duniani, mbali na rasilimali walizonazo, lakini kodi inaendelea kubaki kuwa ni chanzo muhimu katika kujipatia mapato ambayo huleta maendeleo.

 

Kwa vile Serikali ina dhamana kwa wananchi wake imeweka vipau mbele kadhaa, ikiwemo vya ulipaji kodi kwa hiari kwa kutumia mashine za kielektroniki, bila ya kumpendelea mtu yoyote.

 

Kwa maana hiyo, Serikali imechukua hatua ya kutangaza utoaji wa risiti za kielektroniki (VFMS) wala haikuwa na nia mbaya ya kuwakandamiza wafanyabiashara ama kuwaumiza wananchi wake.

 

Bali bali ni kuhakikisha inadhibiti mapato na kuimarisha huduma za kimaendeleo ambazo ndio ndoto ya wananchi wake.

 

Kifungu cha 23 (1) cha Sheria ya usimamizi wa kodi (TAPA) kinamtaka kila mlipa kodi ambae anauza bidhaa ama huduma kwa fedha taslim au mkopo ni lazima ampe mteja wake ankara ya kodi au risiti.

 

WANANCHI WANASEMAJE

 

Ali Mohamed Ali wa Mkoani na Asha Kombo Bakar wa Mwambe wanasema, hakuna kitu chochote kinacholeta faida kikawa na ubaya hivyo kulipa kodi kwa njia ya risiti za kielektronik ni jambo jema kwa vile linaleta faida.  

 

“Kwa vile wananchi wanategemea Serikali yao katika kuwaletea maendeleo, ili waweze kuwa na maisha bora yenye manufaa, haina budi kuendeleza yale ambayo yataweza kufanikisha hilo”, Ali anasema.

 

Farida Abdi wa Mtambile alivyofahamu baada ya kupata elimu kupitia kwa baadhi ya viongozi wa Serikali, kodi ina asilimia kubwa ya kuiwezesha nchi kuleta huduma za kimaendeleo.

 

“Katika nchi hali zinatofautiana wapo wanaomudu huduma katika familia zao kama vile za afya, elimu na nyengine nyingi lakini pia wapo ambao wanategemea kupata huduma hizo kupitia Serikalini”, anaongeza.

 

WAFANYA BIASHARA WANASEMAJE

 

Gharib Mohamed Ali ambae ni Meneja wa sheli ya Mkoani Pemba anasema, kutumia mashine za kielektroniki kwa wafanyabiashara kunaleta usawa kila mmoja analipa kodi bila ya kufanya ubabaifu.

 

Anasema, katika kazi zake hulazimika kutumia muda wa kuwapa elimu ya kupokea risiti hizo kwa wateja wanaofika hapo kutaka huduma, kwani wengi huwa na haraka ya kutaka kuondoka kabla ya kupewa risiti hizo.

 

“Ni vyema kila mmoja kuchukuwa jitihada yakuelimisha kuhusianana umuhimu wa kutowa risiti za kielektroniki kwani zinaleta faida kwa wananchi na nchi yao”, anasema.

 

Habiba Mohamed Kombo ni mfanyabiashara ya nguo Chakechake anasema kutumia risiti za kielektroniki ni sahihi, kwani zinafikisha mapato kule kunakostahiki.

 

Anasema kila mfanyabiashara ana wajibu wa kufuata utaratibu huo uliowekwa na serikali ili kufikia malengo yaliyokusudiwa ya kuhakikisha maendeleo yanakuwa mazuri zaidi.

 

Said Ali mfanyakazi wa Cable tv Mkoani anasema, ni jambo jema la kutumia risiti za kielektroniki, ingawa yeye humlazimu kutumia kalamu kujaza baadhi ya sehemu kutokana na mashine hizo zilivotengenezwa.

 


“Risiti zenyewe haziendani na matumizi sawa kwa wafanyabiashara wate, hivyo kwa vile kazi zetu hutofautiana na risiti hizo, mimi huandika kwa kalamu mwezi anaolipa mteja wangu”, anasema.

Nuru Abdalla mmiliki wa duka la nguo chakechake anasema sheria iliyowekwa na serikali ikiwemo za ulipaji wa kodi kwa njia za kielektroniki itawasaidia wafanyabiashara wenyewe kwani kumbukumbu zake zinabakia tofauti na risiti za karatasi.

 


VIONGOZI WA SERIKALI WANASEMAJE

 

Raisi wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi ni namba moja kati ya viongozi wanaoelezea umuhimu wa kulipa kodi kwa njia ya elektroniki .

 

Anasema, bila ya kodi nchi haiwezi kupiga hatua za maendeleo kama vile elimu, afya, maji safi na salama, ujenzi wa miundo mbinu na mambo mengine mengi yanayofanywa na Serikali yanategemea fedha zitokanazo na kodi.

 

Makamu wa Pili wa rais wa Zanzibar Hemed Suleiman Abdalla katika matembezi ya kuhamasisha zoezi la kudai risiti za kielektroniki anasema, umuhimu wa kukusanya kodi kwa kutumia mashine za kielektroniki ni kukuza mapato ya nchi.

 

Anasema, ni vyema wananchi kudai na kutoa risiti kwa wanaofanya miamala ya kibiashara, ili kudhibiti ukusanyaji wa mapato yasiweze kupotea.

 

“Jukumu la msingi kwa serikali ni kuweka mipango madhubuti ya ukusanyaji wa mapato ambayo yatatumika katika ujenzi wa miradi mbali mbali ya maendeleo ili kuijenga Zanzibar mpya”, anasema.

 

Waziri wa nchi Ofisi ya Rais fedha na Mipango wakati akitoa tamko la kuwataka wafanyabiashara wote waliopo Zanzibar kuhakikisha wanatumia mashine za kielektroniki (VFMS).

 

Anasema, mfumo huo maalum ambao unatengenezwa na bodi ya mapato Zanzibar (ZRB) unalenga kuziba mianya ya upotevu wa mapato nchini na kuongeza ari ya ukusanyaji wa mapato.

 

‘Virtual fiscal management system’ (VFMS) ni mfumo ambao tayari umeshazinduliwa kwa matumizi rasmi ya kuuzia bidhaa, kutoa huduma na unatengenezwa kuongeza mapato ya Serikali na kuondoa mianya ya upotevu wa mapato.

 

“Mfumo huu unawezesha kuhifadhi na kutoa taarifa za mauzo, kukokotoa mauzo na kodi, urahisi wa ujazaji ritani za kodi pamoja na kufatilia taarifa za wageni wanaoingia”, anasema.

 

Spika wa Baraza la Wawakilishi la Zanzibar Zubeir Ali Maulid anasema  kuwa, ni vyema kwa wauzaji na wafanyabiashara kuweka matangazo katika maeneo yao ya biashara ambayo yataonesha umuhimu wa kudai risiti kwa anaenunua bidhaa katika maeneo yao ya kazi.

 

ZRB WANASEMAJE

 

Kamishna wa Bodi ya Mapato Zanzibar (ZRB) Yussuf Juma Mwenda anasema, risiti ama Ankara ndicho kidhibiti cha taasisi za kodi kuthibitisha kwamba mfanyabiashara ameuza bidhaa au huduma na ametoza kodi na kuifanya Serikali ikusanye mapato yake inavyostahiki.

 

Anasema, Serikali imeanzisha mfumo huo ili kuhakikisha kodi yake inafika Serikalini kwani wadau wakubwa wa kodi ni wananchi wanaonunua bidhaa kwa wafanyabiashara.



Meneja wa Idara ya Sera, Utafiti na Mipango wa Bodi ya mapato Zanzibar (ZRB), Ahmed Haji Sadat anasema ni vyema wafanya biashara kuwa na utamaduni kutoa risiti za bidhaa zao, ili waweze kufahamu faida na hasara ya biashara wanazozifanya.

“Wafanyabiashara tambueni suala la risiti ni kitu muhimu kwenu  kwani kutawawezesha kufahamu maendeleo ya biashara zenu”, alisema Saadat.          

Mkuu wa kitengo cha walipa kodi, Bodi ya Mapato ZRB, Shaaban Yahya Ramadhan anasema ulipaji wa kodi ni jambo rahisi, iwapo wafanyabiashara watakuwa na utamaduni wa kuweka kumbu kumbu za kudumu pale wanapofanya mauzo ama manunuzi katika biashara zao.

Anawataka wafanyabiashara wasiogope kutumia mashine za kutolea risiti kwa kisingizio chochote kile kwani ziko salama hasa kwa vile zinawawekea kumbukumbu ya kudumu.

Mkurugenzi wa ZRB Pemba Jamal Hassan Jamal anasema kuwa iwapo mashine za kielektroniki zitatumika ipasavyo zitaongeza mapato zaidi na hata kuvuuka malengo ya makusanyo ya shilingi bilioni 33.226 ambazo wamewekewa kwa Pemba.

‘’Kwa mwaka wa fedha wa 2022/2023 kwa Pemba tumepangiwa kukusanya kiasi hicho, na naamini tutavuuka lengo, maana sasa kunaukusanyaji wa mapato kwa njia ya kielektroniki,’’anaeleza

Anasema kazi kubwa ya ‘ZRB’ ni kusimamia na kuhakikisha ulipaji wa kodi kwa kutumia mashine hizo, kwani kodi inayolipwa itakwenda moja kwa moja kwenye mfuko wa serikali, tofauti na hapo awali ambapo risiti zilitolewa kwa mkono”,anafahamisha.

VIONGOZI WA DINI

 

Sheikh Said wa ofisi ya mufti Pemba anasema asili ya kodi inatoka katika uislam kama vile kwenye  zaka, ngawira , kodi ya ardhi ,kichwa ambapo zilikuwepo katika dola ya kiislamu na zilikuwa zinahifadhiwa katika hazina ya serikali iliyokuwa ikijulikana kwa jina la Bait-ul-mal.

 

 Anasema katika uislamu kiongozi wa nchi anayohaki ya kuwataka wananchi wachangie kodi kwa dharura maalum anaweza kuweka kiwango ama asiweke.

 

“Mfano wa hilo Mtume Muhammad (S.A.W) katika vita vya taabuk dola ya kiislamu haikuwa na uwezo katika kufadhili vita hivo lakini bwana Mtume aliwataka waislamu wachangie katika vita hivyo”,anafafanua.

 

Samwel Elias Maganga wa kanisa la TAG Makangale anasema kwa dini ya kikiristo kodi sio dhambi kwani inatambua uwepo wa mamlaka nyengine ikiwemo ya Serikali.

 


Anasema, dini hiyo inatambuwa kuwa Serikali ni sawa na baba hivyo ni wajibu wake kupanga mipango yake ikiwemo ya kiuchumi na kuifanya iendelee mbele.

 

“Bibilia inasema tutii mamlaka zilizopo na kodi ambayo haikubaliki ni kama ile ya utapeli, dhuluma lakini kama ni andiko la Serikali lenye haki na usawa inakubalika”, anasema.

 

Serikali ya Mapinduzi Zanzibar inahimiza wafanyabiashara na wananchi kutoana kudai risiti za elektoniki, ili iweze kufanya shughuli zake za kuwaletea wananchi maendeleo endelevu.

 

                                              Mwisho

 

 

 

 

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch