Skip to main content

'UTITIRI WA MADRASSA TISHIO LA UDHALILISHAJI KWA WANAFUNZI'

 



NA HAJI NASSOR, PEMBA::::

MOJA ya kichecheo kikubwa cha kujitokeza kwa matendo ya ukatili na udhalilishaji kwa wamafunzi, ni uwepo wa utitiri mkubwa wa madrassa na unaokosa waalimu na kisha wanafunzi kujisimamia wenyewe kwa muda mrefu.

Utafiti mdogo uliofanywa na Chama cha waandishi wa habari wanawake Tanzania TAMWA-Zanzibar kisiwani Pemba, umebaini kuwa, idadi kubwa ya madrassa inayobeba wanafunzi wengi na kukosa waalimu wa kutosha, ni sababu ya kujitokeza matendo hayo.

Utafiti huo unaeleza kuwa, zipo baadhi ya Madrassa zenye idadi kubwa ya wanafunzi, ingawa waalimu ni wachache na kupelekea wanafunzi wenye mkubwa kuwaongoza wenzao wapendavyo.

Wakizungumza kwenye utafiti huo, katika wilaya ya Chake chake, waalimu walisema idadi kubwa ya madrassa inayokosa waalimu ni chanzo cha matendo ya udhalilishaji.

Mwalimu ambae alikataa jina lake kuchapishwa, alisema haiwezekani madrassa kuwa na wanafunzi 80, lakini kuongozwa na waalimu wawili.

Mwengine alisema, hao idadi ndogo ya waalimu waliopo katika baadhi ya madrassa hawana muda mkubwa wa kukaa na wanafunzi, jambo linalopelekea wanafunzi waliopo kujiongoza.

“Kama waalimu muda mrefu hawapo, huwa ni fursa chafu kwa wanafunzi kujiingiza kwenye matendo maovu, hivyo ni jukumu la jamii kulijiua hilo,’’alieleza.

Kwa upande wake mwalimu mkuu wa Madrassa iliyopo soko la Tibirinzi wilaya ya Chake chake Walid Muhsin Juma, alisema suala la waalimu kujiingiza kwenye vitendo vya udhalilishaji kwa wanafunzi wao, ni tabia ya mtu na sio kwa idadi kubwa ya wanafunzi.

“Kama mwalimu hajielewi na hawezi kudbiti matamanio yake, hata kama hayupo madrassa, anaweza kujiingiza kwenye matendo hayo,’’alieleza.

Afisa Miskti na madrassa kutoka Afisi ya Mufti Pemba Abdull-latif Abdalla Salum, alisema wamekuwa wakijitahidi kutoa elimu ya madhara ya matendo hayo kwa wasimamizi wa nyumba za ibada na madrassa.

Alieleza kuwa, wamekuwa na miongozo maalum kwa waalimu na hata madrassa yenyewe, kabla ya kuisajili, ili kujiridhisha kwa lengo la kuwalinda wanafunzi.

“Ofisi ya Mufti kila wakati inazitembelea madrassa na kuwaelezea athari ya waalimu kujihusisha na matendo ya ukatili na udhalilishaji,’’alieleza.



Mzazi Issa Haji Omar na mwenzake Asha Muhsin Is-mail wa Chake chake walisema, bado Ofisi ya Mufti inatakiwa kuwa imara kabla ya kuanzishwa kwa madrassa.

Utafiti umebaini kuwa, hadi mwezi August mwaka huu, kisiwa cha Pemba pekee kina Madrassa 814 zilizosajiliwa na Ofisi ya Mufti, ambapo ni wastani wa madrassa 204 kwa kila wilaya, kati ya wilaya nne za Pemba.

Wilaya ya Wete inazo madrassa 190, Mkoani 155 na wilaya ya Micheweni inazo jumla ya madrassa 170 na Chake chake 299 ambazo zimesajiliwa ramsi.

Mratibu wa TAMWA Zanzibar ofisi ya Pemba Fat-hya Mussa Said, amesema wapo baadhi ya waalimu wa madrassa kwa kule kukosa kwao maadili, wamekuwa wakijihusisha na matendo hayo.

‘’TAMWA imeshakutana na waalimu mara kadhaa kuwapa elimu ya athari ya matendo hayo, ingawa bado hali inaendelea kutisha kwa baadhi ya madrassa,’’alieleza.

Hata hivyo amewakumbusha wazazi na walezi, wasikubali matendo hayo kuyafanyia sulhu, na badala yake washirikiane na vyombo vya sheria kuyatokomeza.



Mkuu wa mkoa wa kusini Pemba Mattar Zahor Massoud, aliitaka Ofisi ya Mufti kuwachukulia hatua za kinadhamu mara maoja, waalimu wanaojihusisha na matendo hayo.

Mkurugenzi wa Tumaini Jipay Pemba Tatu Abdalla Msellem, alisema uanzishwaji ovyo ovyo wa madrassa na waalimu wenye umri mdogo, ni moja ya vyanzo vya kujitokeza matendo ya udhalilishaji.

Mwanafunzi mmoja aliyewahi kubakwa na mwalimu wake Pujini wilaya ya Chake chake, amesema kama adhabu itaendelea kutolewa ndogo, matendo hayo yatendelea kunawiri katika jamii.

Mei 16 mwaka 2022, Mahakama ya mkoa Chake Chake, ilimuhukumu kwenda chuo cha mafunzo miaka 15 mwalimu wa Madrassa kutoka shehia ya Mchakwe Mwambe wilaya ya Mkoani Ali Ussi Simai mwenye miaka 25, baada ya kupatikana na hatia ya kumbaka mwanafunzi wake, mwenye miaka minane (8), kosa hilo alilitenda Novemba 28 mwaka 2021.



Oktoba 4, mwaka 2021 Ofisi ya Mufti Zanzibar ikiongozwa na Katibu wa ofisi hiyo sheikh Khalid Ali Mfaume, ilifika kwenye madrassatul-bisimmillah Unguja, kufuatilia tukio ulawiti la mwanafunzi alilofanyiwa na mwalimu wake Ali Abdalla Ali na kisha kuifunga madrassa hiyo.

Aidha mahkama ya mkoa Mwera, ilimfunga miaka 80 chuo cha mafunzo mwalimu wa madrassa miaka (21), na faini ya shilingi milioni 3, baada ya kutiwa hatiani kwa kosa la kumbaka mwanafunzi wake mwenye miaka 15.

                              Mwisho

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch