Skip to main content

WATOTO WATANO WASALIMIKA KUPOTEZA UHAI PEMBA NYUMBA YAO IKITEKETEA KWA MOTO


 


NA HAJI NASSOR, PEMBA:::


WATOTO watano  wa  familia  moja  wakaazi wa kijiji cha Mtega Wawi Wilaya  ya  Chake chake  Pemba, wamesalimika  kufa baada ya  nyumba  waliokuwa wakiishi kuteketea  kwa moto na kuunguza  vitu  vyote  vilivyo kuwemo ndani.

Mashuhuda  wa tukio  hilo  wamesema  kuwa , wameona  moshi mkubwa  ukitokea kwenye  mapaaa ya nyumba  hiyo huku  watoto hao  , wakiwa  nje  ya  nyumba  yao  wakipga  kelele  kuashiria kuomba  msaada.

Mmoja kati ya mashuhuda  hao Ibrahim Mohamed  Ali , amesema  kuwa  baada  ya  kusikia kelele hizo,  alifika  kwenye  nyumba  hiyo, na kuwakuta  baadhi  ya  watu wengine wakianza  kuokoa  vitu  vilivyokuwa  ukumbini .

Alieleza  kuwa wakati huo baadhi yao wameshapiga  simu Kikosi  cha  zima  moto na uokozi na  baada ya dakika  10 kilifika  na kuanza kuuzima moto huo ingawa nyumba yote  iliteketea kwa moto.

 “ Moto  ulikuwa  mkubwa  sana na  vyumbani kulizidiwa  na   moshi  mkubwa  mweusi  ambao  ulituzuia kuweza  kuingia  kwa  ajili  ya kuokoa  vitu  vyengine , ‘’ alieleza .

Nae shuhuda  Hassan  Mohamed  Hassan  alisema , kama  moto  huo  usingeanza  juu ya  mapaa kikosi  cha  zima  moto na  uokozi chenge fanikiwa kuuzibiti .

Mapema Mkuu wa Kikosi  cha Zima  moto na  uokozi Chanjaani  Wilaya ya  Chake chake  Inspekta Mwichande Hassan  Khamis ,Alisema kuwa walipokea taarifa hizo  majira  ya  saa 10 : 30 jioni na dakika 10  baadae waliwasili  kaika  eneo  la tukio na kuuzima  moto  huo .

“Moto ulikuwa ni mkubwa  mno na engekuwa twengepata  taarifa  mapema  zaidi twenge fanikiwa  kuudhibiti  moto  huo  na  nyumba  isinge  teketea  yote,’’alieleza .

Hata hivyo amewataka wananchi kuwasiliana na kikosi  chake moja  kwa moja linapotokea  tukio la moto au  janga jengine kwa kupiga simu namba 114 ambayo ni  bure.

Kwa upande wake Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kusini  Pemba Abdalla Hussein  Mussa  alikiri kutokea  kwa tukio  hilo  jana Julai 20 , mwaka  huu majira  ya  saa  10 : 30 jioni wakati  mmiliki wa nyumba  hiyo Mwalim Juma Yahya na mke wake  wakiwa  kazini .

Kamanda huyo alieleza kuwa, nyumba hiyo pamoja na  vitu  vyake kadhaa vimeteketea kwa moto ingawa hakuna  majeruhi  wala  mtu  aliye poteza  uhai.

“Sisi  jeshi la Polisi tunawashukuru wananchi kwa kutoa  taarifa za haraka kwa  tukio  hili  ingawa , ushauri  wangu  kwao wajiwekee vifaa vya kuzimia moto majumbani  mwao ,” alifafanua.

Mratibu  wa Maafa  Pemba, Khamis  Arazak Khamis  alisema  kuwa, hadi  sasa  hawajapata  tathmini  halisi  ya hasara  iliyopatikana  katika  tukio  hilo . 






Hili ni tukio la tano kuwahi kutokea kwa mwaka huu kisiwani Pemba ambapo tukio la kwanza ni Skuli  ya  Sekondari ya Utaani ,nyumba ya mwananchi Wete , Madungu , Chuo  cha  ufundi  Kengeja na nyumba  hiyo  ya Wawi.

        Mwisho .

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch