Skip to main content

JAJI MKUU AWAKOLEZA 'SPEED' MAHAKIMU KESI ZA UDHALILISHAJI PEMBA

 


NA ZUHURA JUMA, PEMBA

JAJI Mkuu wa Zanzibar Khamis Ramadhan Abdalla amewataka mahakimu kuendelea na kasi ya kusikiliza kesi za udhalilishaji kwa haraka, ili ziweze kupata hatia kwa muda mfupi.

Akiwasilisha ripoti ya ziara ya Jaji huyo iliyofanyika kuanzia Julai 18 mwaka huuu, Kaimu Mrajis Mahakama Kuu Zanzibar Salum Hassan Bakar alisema, takwimu zinaonesha kupungua kwa kiasi kikubwa mrundikano wa mashauri hayo mahakamani.

Alisema kuwa, katika ripoti hiyo Jaji Mkuu aleleza kuwa, pamoja na kuridhika kwa kasi ya uendeshaji wa mashauri hayo kwa mahakama za udhalilishji Mkoa wa Kaskazini na Kusini Pemba, lakini bado mahakimu wana jukumu la kuziendesha kesi hizo kwa haraka zaidi.

‘’Vile vile aliridhishwa na ujaji wa mashahidi mahakamani na kuwaasa wale wachache ambao wanakaidi, wajitokeze kufika mahakamani ili kuyamaliza kabisa mashauri hayo’’, alisema Kaimu huyo.

Aidha aliwaagiza mahakimu na makadhi kuyafanyia kazi mashauri yaliyofikishwa mahakamani kuanzia mwaka 2020 kuja chini, ambapo katika kutekeleza hilo amewataka kushirikiana na wadau wote wanaohusika ili kufanya kazi hadi siku za mapumziko.

‘’Mushirikiane na ofisi ya Mkurugenzi wa mashitaka pamoja na mawakili wa kujitegemea katika kuhakikisha kesi hizo zinamalizika haraka, ambapo mahakama imeandaa bajeti maalumu kwa ajili ya kufanya kazi hiyo kwa siku ambazo ni za mapumziko’’, alifafanua.

Kaimu huyo alisema kuwa, Jaji mkuu katika ziara yake hiyo pia amepiga marufuku utengenezaji wa hati zote za kisheria ikiwemo hati za madai, majibu ya madai, sababu za rufaa, hati za kiapo na mikataba kwenye mahakama zote Unguja na Pemba.

‘’Hati hizo zinatakiwa zitengenezwe kwenye ofisi za mawakili, mavakili, Idara ya msaada wa kisheria au vituo vya msaada wa kisheria, kwani ni kazi yao na wao wanalipa kodi Serikalini, hivyo kazi hizo zinatakiwa kufanyika huko’’, alisema.

Kwa upande wake Naibu Mrajis Mahakama Kuu Pemba Faraji Shomari alisema kuwa, jumla ya kesi 56 za udhalilishaji zimefunguliwa kwa mahakama za Pemba, ambapo Kaskazini ni kesi 27 na Kusini ni kesi 26.

Alifafanua kuwa, kati ya kesi hizo 27 za Mkoa wa Kaskazini Pemba kesi tisa zimetolewa maamuzi na kesi 18 zinaendelea huku Mkoa wa Kusini Pemba kesi tisa zimetolewa maamuzi na 17 zimnaendelea.

Aliwataka mahakimu kwamba wasijibweteke katika kuzitolea maamuzi kesi hizo, ili kuona kwamba zinamalizika kwa muda mfupi jambo ambalo litasaidia kupunguzika kwa matendo hayo katika jamii.

Ziara hiyo ya siku tatu ilikuwa na lengo la kuwashukuru wafanyakazi kwa ushirikiano wao pamoja na kusikiliza na kujadiliana na wafanyakazi kuhusu changamoto mbali mbali zinazokwamisha utendaji kazi za kila siku na kuweka mikakati ya kuzipatia ufumbuzi.

                                                      MWISHO.

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch