Skip to main content

TAMWA-ZANZIBAR WAANDISHI ONGEZENI NGUVU KUWAAMSHA WANAWAKE KUDAI HAKI ZAO



NA HABIBA ZARALI, PEMBA

WAANDISHI wa habari wametakiwa  kuongeza nguvu katika kuandika habari zinazowajengea uwezo wanawake kutambua sera mbalimbali zinazozungumzia haki zao, ili iwe rahisi kujua namna ya kushiriki na kudai haki zao za uongozi.

Kauli hiyo   imetolewa na Mkurugenzi wa Chama Cha waandishi wa habari  TAMWA Zanzibar Dk. Mzuri Issa Ali wakati akifunguwa mafunzo ya kuwajengea uwezo  waandishi wa kuandika habari za uchambuzi kuhusu ushiriki wa wanawake katika masuala ya uongozi.



Alisema ni wajibu wa waandishi kuendelea kuelimisha jamii kuondokana na mitazamo hasi  inayorudisha nyuma jitihada za wanawake kuweza kushika nafasi za uongozi.

Alifahamisha kuwa  ni vyema kwa waandishi hao kuelimisha jamii kuhusu itikadi mbovu zinazowavunja moyo wanawake na watoto wa kike na badala yake ziweze kuwajengea uwezo kuhusu kuwania nafasi za uongozi.



"Tunataka nafasi za uongozi kwa sasa ziangalie uwiano wa kijinsia kwa wanaume na wanawake wakati tukijiandaa kwa safari ya 2025", alisema.

Alisema ni  vizuri kuwahamasisha wanawake na wanaume kubadilika na kutenga muda maalum kushirikiana na wake zao katika utekelezaji wa majukumu ya kifamilia ili iwe kikwazo kwa mwanamke kufikia katika nafasi ya uongozi.

Kwa upande wake Mratibu wa chama cha waandishi wa habari Pemba Fat-hiya Mussa Saidi alisema ni vyema waandishi wa habari kuandika na kutangaza vikwazo ambavyo vinawakwamisha wanawake  na kuonesha njia ya kuzipatia ufumbuzi kwa maslahi mapana ya Taifa.

Alisema licha ya juhudi mbalimbali zinazochukuliwa na Serikali na taasisi binafsi lakini bado baadhi ya mifumo inakwamisha wanawake kuweza kufikia usawa katika vyombo vya kutowa maamuzi.

"Katika mafunzo ya Leo hakikisheni mnayatumia vizuri kwa kuleta usawa na kufikia malengo ya kuwepo uwiyano katika ngazi ya kutowa maamuzi",alielekeza.


Akitowa mada ya jinsia na uongozi mwandishi  Haji Nassor  Mohamed alisema bado mifumo dume inaendelea kuwakosesha wanawake haki zao za msingi ikiwemo za uongozi.

Alifahamisha kuwa ni vyombo vya habari pekee ndivo visivotumia nguvu  kubadilisha mfumo huo na  mitazamo finyu mbalimbali ya kubadilisha kundi moja ama jengine hivyo ni wajibu wao kuhakikisha wanatumia vyombo vyao kutowa elimu hiyo.



Wakitowa mchango wao katika mafunzo hayo mwandishi wa ZBC Mchanga haroub na Asma Abas walisema mbali na waandishi kuandika  habari za Wanawake na uongozi lkn bado Kuna changamoto zinazowakabili Wanawake hao ikiwemo umaskini na tabia ya kukata tamaa.

Walisema wanawake ni chachu ya kuleta maendeleo kwani anaweza kushika nafasi za uongozi katika sekta zote na kufikisha sauti kwa walio chini yao.



Mafunzo hayo ya siku tatu ni kupipitia mradi wa kuwawezesha wanawake kushiriki katika masuala ya uongozi na demokrasia unaotekelezwa kwa mashirikiano na taasisi za chama Cha waandishi wa habari wanawake Tanzania,TAMWA-Zanzibar, jumuiya ya wanasheria wanawake Zanzibar ZAFELA, na jumuiya ya utetezi wa jinsia na mazingira Pemba (PEGAO) kwa ufadhili wa ubalozi wa Norway.

                                        Mwisho.


Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch