Skip to main content

WATAALAMU 'ECD' PEMBA: WATOA RAI KWA WAZAZI

 



NA HAJI NASSOR, PEMBA

WAZAZI na walezi kisiwani Pemba, wametakiwa kuwasiliana kwa ishara, maneno na kuwafanyia uchangamshi wa michezo kadhaa watoto wao wachanga, kwani kufanya hivyo ni njia rahisi ya kugundua, ikiwa wamezaliwa na ulemavu ama laa.

Aidha wazazi hao wameelezwa kuwa, kufanya njia hizo zitakuza kwa haraka ufahamu wa wazazi kwa watoto wao, ikiwa wamezaliwa na ulemavu ama laa.

Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi, wataalamu wa malezi na makuzi ya awali ya kisayansi ya mtoto ‘SECD’ kisiwani Pemba, walisema wapo watoto wamekuwa wakizaliwa na ulemavu, ingawa kisha huishi nao kwa wazazi kukosa kuwafuatilia.

Mmoja kati ya wataalamu hao, Rashid Said Nassor alisema, ni rahisi kwa wazazi na walezi, kutambua ulemavu wa awali wa watoto wao, ikiwa wataanza utamaduni wa kuwasiliana nao mapema.

Alisema, mtoto baada ya kuzaliwa ubongo wake uko tayari kupokea jambo lolote, hivyo ni wakati mwafaka kwa wazazi na walezi, kuanza nao mawasiliano na uchangamshi ili kujua, ikiwa wana aina yoyote ya ulemavu waliozaliwa nao.

Mtaalamu huyo alisema, sayansi inakubali kuwa, mtoto baada ya kuzaliwa anauwelewa mkubwa ikiwemo kusikia suati na milio mbali mbali, hivyo ni wakati mwafaka kwa wazazi kufanya uchangamshi.

‘’Njia moja ya kumgundua mtoto ikiwa amezaliwa na ulemavu ama laa, ni wazazi na walezi kuchangamana na watoto kuanzia siku moja baada ya kuzaliwa hadi miaka minane kwa kufanya michezo mbali mbali,’’alieleza.

Aidha mtaalamu huyo wa ‘ECD’ alifahamisha kuwa, kazi ya kuchangamana na mtoto sio jukumu la mama pekee, bali hata akinababa wanatakiwa kufanya hivyo.

Nae mtaalamu wa ‘ECD’ Omar Mohamed Ali, alisema upo uwezekano mkubwa wa mtoto aliyezaliwa na ulemavu na kama ukiwahiwa mapema kutibika.

‘’Hili haliwezi kugundulika, ikiwa wazazi na walezi wataacha kuwasiliana, kuchangamana na kufanya uchangamshi na watoto wao kwenye makuzi ya awali,’’alifafanua.

Hivyo amewaasa wazazi na walezi, kujenga utamaduni wa kuwa karibu kimawasiliano na watoto, na kufuatilia usikivu wao ili kugundua umahiri na udhaifu wao mapema.

‘’Inawezekana watoto wanahitaji kupata matibabu ya mapema, iwe koo, maskio, macho, viungo au ngozi kwa lengo la kuzuia ulemavu wa kudumu, na hili litawezekana kwa ukaribu wa wazazi kwa watoto wao wachanga,’’alifafanua.

Nae mkufunzi wa mafunzo ya ‘ECD’ Davis Gisuka kutoka tasisi ya Children in Crossfire Tanzania alisema, watoto wanaweza kuepushwa na ulemavu, kama wazazi watakajenga utamaduni wa kuchangamana na watoto wao.

Alieleza kuwa, ubongo wa mtoto mchanga unawezo wa ufahamu wa asilimia 25 na kupokea kila kitu, ambapo ni wakati mwafaka kwa wazazi na walezi, kuchangamana nao.

‘’Wazazi wasisite kuchangamana na watoto wao, maana sayansi inakubali kuwa, ukitaka kumgundua mtoto juu ya aina ya ulemavu alionao, hiyo ni njia moja wapo,’’alieleza.

Baadi ya wazazi na walezi wamesema, wamekuwa karibu na watoto kufanya uchangamshi, ingawa sio kwa kugundua aina ya ulemavu walio nao.

Mzazi Mwanaisha Himid Hussein wa Wawi Chake chake, alisema hawana uwelewa wa elimu ya malezi ya kisayansi na makuzi ya awali ya watoto ‘ECD’ bali, wamekuwa wakifanya kama mazoea tu.

‘’Tunawasiliana na watoto wetu na kufanyanao uchangamshi, ingawa hatutengi muda maalum kama wataalam wanavyopendekez,’’alieleza.

Nao wazazi Habiba Soud Khalfan na mwenzake Aisha Hussein Khamis walisema, wakati mwengine wamekuwa wakipuuzia uchangamshi na kufanya mawasiliano na watoto wao, wakidhani hawana uwezo wa uwelewa.

‘’Kwanza hatuamini kuwa, mtoto aliyezaliwa ndani ya siku moja, anauwezo wa kusikia zaidi ya lugha 600, kama watalaamu wanavyotueleza, na ndio maana hatukuona umuhimu huo,’’alieleza.

Kwa upande wake Meneja ‘ECD’ tasisi ya Maendeleo ya Binadamu kutoka Chuo Kikuu cha Aga Khan, Mombasa Kenya Joyce Marangu alisisitiza kuwa, wataendelea kuisaidia Tanzania katika malezi ya kisayansi.

‘’Moja ya faida kubwa ya malezi ya ‘CED’ kwa wazazi na walezi ni kugundua ufahamu na umahiri wa mtoto tokea mapema, lakini hata juu ya uwezo wake wa kutambua mambo kadhaa,’’alifafanua.

Kaimu Afisa Mdhamini wizara ya Afya Pemba Dk. Yussuf Hamad, alisema elimu hiyo ya ‘ECD’ hutolewa kwenye kliniki za mama wajawazito.

‘’Lengo ni kuona wazazi na walezi, wanagundua mapema uwezo wa watoto wao, iwe ni kusikia, kuona, kucheza na kuanza mazungumzo, ili kama kuna tatizo kuwawahisha matibabuni mapema,’’alifafanua.

Hata hivyo alikiri kuwa, elimu hiyo inalazimika kutolewa kwa ngazi ya jamii nzima, ili malezi hayo yawe maarufu, katika malezi, makuzi ya watoto wote.

Mkurugenzi Mkaazi wa tasisi ya Children in Cross fire Cragi Ferla aliwataka waandishi wa habari kuisambaaza elimu ya ‘ECD’ kwa jamii, ili taifa liwe na watoto wanaojifahamu.

                                Mwisho            

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch