Skip to main content

‘WEPO’ YAWAFIKIA WANANCHI 473 KAMBI YA MSAADA WA KISHERIA

 

NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

WANANCHI 473, kati yao wanawake 295 na wanaume 178, wa shehia za Kigongoni na Kiuyu Minungwini, wamefikiwa na elimu, ushauri na msaada wa kisheria, ikiwemo utaratibu wa upatikanaji cheti cha kuzaliwa, kwenye kambi ya msaada wa kisheria, iliyowekwa na Jumuiya ya Wasaidizi wa sheria wilaya ya Wete ‘WEPO’.

Kambi hiyo ya siku moja, iliyofanyika leo Julai 7, kuanzia saa 3:00 asubuhi hadi saa 9:30 jioni, wengi wa wananchi waliofika, walikuwa na malalamiko ya kukosa vyeti vya kuzaliwa.

Ilifhamika kuwa, wingine ni wanaolalamikia kukosa vitambulisho vya mzanzibari mkaazi pamoja na vile ya taifa.

Akizungumza na waandishi wa habari, Msaidizi wa sheria kutoka ‘WEPO’, Siti Faki Ali, alisema kambi hiyo imewasaidia kuwapa mwanga, wa aina ya changamoto iliomo ndani ya jamii.

Alisema, kambi hiyo imewaamsha kwamba, kazi ya kuwaelimisha wananchi kupitia wasaidizi wa sheria, inahitaji kuongezwa nguvu, kwani wapo ambao hawajui hata utaratibu wa kupata nyaraka hizo muhimu.

Siti, alifahamisha kuwa, jingine walilobaini kwenye kambi hiyo, ni kuwepo kwa baadhi ya wananchi ambao, uwelewa wao juu ya kuitumia ofisi ya sheha, uko chini.

Alieleza, wapo wananchi wakati wanawapa msaada wa kisheria, walidai kuwa hawajui kuwa, kama una mri mkubwa unaweza kwenda wa sheha, na kuanza kwa hatua ya kwanza, kabla ya kufika wilayani.

Hata hivyo, alisema wapo wingine wameshindwa kufuatilia wenyewe, maana walishaanza harakati ingawa nenda rudi ya wilayani, walikata tamaa, kwa kupoteza gharama.



‘’Sisi ‘WEPO’ imetulazima kurudia tena kwenye sheha hizo za Kigogoni na Kiuyu Minungwini, maana wapo wananchi ambao hatukuwamalizia taratibu nyingine za kisheria,’’alifafanua.

Mapema Mratibu wa Mradi wa Uwezeshaji wa Kisheria na Upatikanaji wa Haki ‘Legal Empowerment and Access to Justice’ Rashid Hassan Mshamata kutoka WEPO, alisema mradi huo, unaovipengele kadhaa, kikiwemo cha kuweka kambi katika shehia.


Alieleza kuwa, mradi huo ambao sasa unakwendea ukingoni ndani ya mwaka huu, umeshasaidia mno, kwanza kwa kundi la wanafunzi na vijana. kutambua viashria vya ukatili na udhalilishaji, kupitia makongamano na semina zao.

‘’Kwa hakika wenzetu wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa ‘UNDP’, kuturidhia mradi huu, wameiokoa jamii ya Wete, katika kujua haki na wajibu wao, maana ilikuwa nyuma,’’alieleza.

Alifahamisha kuwa, wanatamani mno mradi kama huo, waupate tena, ili kuendeleza nguvu ya elimu ya kisheria, pale walipofikia, ili kutimiza mwelekeo wa ‘WEPO’ wa kujua haki na wajibu wao wanajamii.

Awali akizungumza kwenye baadhi ya mikutano, Mkurugenzi wa ‘WEPO’ Mwalimu. Hemed Ali Hemed, alisema sasa wapo wananchi wamejua haki na wajibu wao, kupitia mradi huo.




Sheha wa Kiuyu Minungwini Nachia Yahya Salum, alisema ujio wa kampeni hiyo, sasa wananchi wake, wameamka katika kutafuta nyaraka za lazima, ikiwemo cheti cha kuzaliwa na cha ndoa.

Akizungumza kabla ya kuanza kwa kambi hiyo, Afisa sheria kutoka Kamisheni ya Ardhi Pemba Asha Suleiman Said, aliwatahadharisha wananchi hao, kuacha kununua na kuuza ardhi kiholela.

Mwanasheria Afisi ya Mwanasheria Mkuu, Ali Hamad Mbarouk, alisifu ‘WEPO’ kwa kambi hiyo, ambayo imetoa fursa kwa wananchi wa shehia hizo, kupata uwelewa wa changamoto zao za kisheria.


Hata hivyo, Msaidizi wa sheria, shehia ya Mtemani Wete Said Rashid Hassan, alisema kazi iliyofanywa na ‘WEPO’ inafaa kuungwa mkono na jamii, ili kuendelea kupata uwelewa wa kisheria.

Tayari ‘WEPO’ kupitia mradi huo, umeshaanzisha vilabu vya kupambana na ukatili na udhalilishi kwa skuli za Uwondwe, Chasasa, Pandani na baadhi ya madrassa za qur-an.

Aidha vilabu kama hivyo kupitia mradi huo, vimeanzishwa shehia za Uwondwe, Mzambarauni, Mlindo, Utaani, Kipangani, Bopwe na Kinyasini.

                               MWISHO


Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...

…….SUZA WATOA USHAURI WA ADHABU YA KUNYONGWA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WANAFUNZI wanaosomea uwalimu Chuo cha taifa cha Zanzibar ‘SUZA’ kampasi ya Benjamin Wiliam Mkapa Wete Pemba, wamependekeza adhabu ya kunyongwa hadi kufa, kwa mtu atakaetiwa hatiani, kwa kosa la dawa za kulevya. Walisema, haiingii akili kuona, mahkama imeshamtia hatiani mtu kwa kukutwa na dawa za kulevya, ambazo huathiri nguvu kazi ya taifa na kisha, kupewa hukumu ya kifungo pekee. Wakizungumza leo Juni 26, 2024 kwenye kongamano la vyuo vikuu, juu ya masuala ya msaada wa kisheria, kuelekea wiki ya msaada wa kisheria Zanzibar, lililofanyika Chuoni hapo, walisema wakati umefika sasa kutolewa kwa hukumu hiyo. Walipendekeza kuwa, ni vyema kwa mtu anayetiwa hatiani asibakie chuo cha Mafunzo pekee kuitia tena hasara serikali kwa chakula na wakati mwingine matibabu, wakati tayari ameshasababisha madhara, kwa vijana. Mshiriki Juma Nafasi Juma, alifafanua kuwa kama mtu ameamua kuliumiza taifa kwa kuingiza, kusafirisha, kusambaaza dawa za kulevya, hivyo n...