Skip to main content

'WEPO' KUENDESHA KAMBI YA MSAADA WA KISHERIA KIGONGONI, KIUYU MINUNGWINI ASUBUHI HII

 

 



NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

JUMUIYA ya Wasaidizi wa sheria wilaya ya Wete Pemba ‘WEPO’ asubuhi hii, inatarajia kuendesha kambi ya siku moja, ya msaada wa kisheria kwa wananchi wa shehia za Kigongoni na Kiuyu Minunwgini wilayani humo, bila ya malipo.

Kambi hiyo, ambayo inatarajiwa kuwakusanya zaidi ya wananchi 500 wa shehia hizo, ni sehemu ya utekelezaji wa mradi wa kupambana na ukatili na udhalilishaji, chini ya ufadhili wa shirika la UNDP.

Akitoa taarifa kwa waandishi wa habari, Mratibu wa mradi huo, Rashid Hassan Mshamata, alisema kambi hiyo itawahusisha wataalamu wa masuala ya ardhi, mahakama, ofisi ya Mkurugenzi wa mashtaka, ofisi ya Mwanasheria mkuu.

Alieleza kuwa, wataalam wingine watakaokuwepo kwenye kambi hiyo ni Jeshi la Polisi, dawati pamoja na wasaidizi wa sheria, kutoka Jumuiya ya wasaidizi wa sheria wilaya ya Wete Pemba ‘WEPO’.

Aliwataka wananchi wa shehia hizo na nyingine, kufika kwenye kambi hiyo ya siku moja, ili kuwasilisha matatizo yao ya kisheria, ikiwemo migogoro ya ardhi, mirathi, matunzo ya huduma za mtoto, migogoro ya ndoa.

Eneo jingine ambalo aliwakaribisha wananchi hao, ni wale waliochukuliwa ardhi zao bila ya kulipwa fidia, waliokosa vitambulisho, vyeti vya kuzaliwa, vya ndoa pamoja kupata elimu ya kisheria bila ya malipo.

‘’Niwaombe sana wananchi wa shehia hizi, kuitumia siku ya leo kuanzia saa 3: 00 hadi saa 10: 00 jioni, kufika skuli ya Minungwini, kufikisha malalamiko yao ya kisheria, ili kupatiwa ufumbuzi wa papo hapo,’’alifafanua.

Mapema Mkurugenzi wa Jumuiya hiyo, Hemed Ali Hemed, alisema fursa hiyo ni adhimu na adimu kwa timu ya wataalamu wa masuala ya sheria, kuwafuata wananchi walipo.

‘’Ijapokuwa kazi ya wasaidizi wa sheria ni kuwafuata wananchi walipo na kuwatatulia shida zao za kisheria, lakini kwa kambi hii ambayo itahusisha wataalamu wa masuala ya kisheria, ni muhimu mno,’’alifafanua.

Msaidizi wa sheria, shehia ya Mtemani Wete Said Rashid Hassan, alisema kazi iliyofanywa na ‘WEPO’ kuupata mradi huo ni jambo jema, hasa kwa wananchi kupata haki zao.



‘’Ni kweli leo hii, skuli ya Minungwini ni fursa ya bure kwa wananchi kupata ufumbuzi wa changamoto mbali mbali za kisheria, maana kila aina ya wanasheria watakuwepo,’’alifafanua.

Hata hivyo, alisema bado wasaidizi wa sheria wataendelea kuwa mwega kwa wananchi wasiokuwa na uwezo, kupata haki zao za kisheria.

WEPO, inaendelea kutekeleza mradi wa upatikanaji haki na kupamba na ukatili na udhalilishaji, ambapo mradi huo unatarajiwa kumalizika mwishoni mwa mwaka huu.


Tayari ‘WEPO’ kupitia mradi huo, umeshaanzisha vilabu vya kupambana na ukatili na udhalilishi kwa skuli kadhaa, ikiwemo Uwondwe, Chasasa, Pandani na baadhi ya madrasaa za qur-an.

Aidha vilabu hivyo kupitia mradi huo, vimeanzishwa shehia za Uwonde, Mzambarauni, Mlindo, Utaani, Kipangani, Bopwe na Kinyasini.

                               MWISHO

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

Vikausha damu vya mjamzito hivi hapa, umo mchele, udongo, mkaa, chaki Uwezekano wa kuzaliwa watoto wenye udumavu, utapiamlo ni mkubwa

  NA ZUHURA JUMA, PEMBA@@@@ ‘’KILA ninapobeba mimba nimezoea kula mchele kwa wingi naweza kusamehe pilau au biriani,’’ ndio maneno ya mwanzao ya Bahati Mohamed Ali (sio jina lake halisi). Nilimfuma akiwa barazani kwake, mjini Ole wilaya ya Chake chake, pembeni yake akiwa na kibakuli cha mwazi, kwa umbali utaona amejaza chakula aina ya pepe, kumbe ni mchele wa Mbeya. Hujichotea kidogo kidogo na kuushindilia mdomoni mwake, huku akiendela kupiga storia na wenzake, bila ya kujali kuwa ujauzito alionayo na mchele huo hauna mwisho mwema. Kawaida yake akiwa mjamzito, kila anapoamka asubuhi anaroweka mchele upatao robo kilo hivi…na baada ya kumaliza kupika, yeye huchukua mchele wake kutafuna (kula). Wakati mwenza wake na watoto wao, wanakula chakula cha mchana, Bahati yeye hukaa pembeni na kibakuli chake cha mchele akiendelea kubahatisha afya yake. ‘’Mimba nyengine hupenda sana kutafuna mchele wa Mbea na nyengine hupenda mchele wa mapembe, kwa kweli huwa nina hamu (kileo), kwan...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...