Skip to main content

MDHAMINI FEDHA PEMBA: ‘NGOs NJOONI MCHUKUE TAKWIMU SAHIHI KWETU KABLA ANDIKO LA MRADI’

 


NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

AFISA Mdhamini wizara ya Fedha na Mipango Pemba Abdul-wahab Said Abubakar, amezitaka asasi za kiraia Pemba, kuitumia ofisi yake, wakati wanapotaka kuandika miradi, ili kupata takwimu sahihi.

Alisema, ili waweze kupata andiko lenye mashiko la mradi, hawanabudi kuwa karibu mno na ofisi hiyo, ili kupata takwimu sahihi, zinazotambuliwa na mamlaka husika.

Afisa Mdhamini huyo aliyasema hayo, leo Novemba 24, 2024  ukumbi wa Kiwanda cha Makonyo Wawi Chake chake, alipokuwa akifungua mjadala kwa asasi za kiraia, juu ya changamoto za sekta zilizopo kisiwani Pemba zilizolalamikiwa kurudisha nyuma harakati za maendeleo kwa asasi  na wananchi .



Alisema, asasi za kiraia zimekuwa ndio mdomo wa changamoto zilizopo ndani ya jamii, hivyo wakiitumia ofisi yake, wanaweza kupata takwimu zinazoweza, kupata mashiko ya hoja zao.

Alifahamisha kuwa, haiwezekani kwa asasi za kiraia, kukaa mbali na wizara ya Fedha, kwani imekuwa ndio eneo pekee lenye kukusanya kodi na takwimu nyingine za serikali.

‘’Nizitake asasi za kiraia Pemba, kuhakikisha wanafanyakazi kwa karibu na wizara ya Fedha, ili kupata takwimu sahihi zitakazo kuwa na mashiko, wakati wanapotetea au kuomba miradi,’’alieleza.

Katika hatua nyingine, Afisa Mdhaminu huyo wa Fedha na Mipango Pemba, alisema serikali inajali na kutambua kwa kiasi kikubwa, mchango wa asasi za kiraia katika maendeleo.



Mapema  kwa upande wake Afisa Mdhamini wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Pemba Mfamau Lali Mfamau, alizitaka asasi za kiraia, kuendelea kuwa mabalozi wa kulinda amani na utulivu  hususan ni  katika kundi la vijana kuelekea uchaguzi  .

‘’Mwakani tunatarajia kuingia kwenye uchaguzi mkuu wa vyama vingi, lazima asasi za kiraia, zitambue wajibu wa kulinda nchi na wananchi wake, na zisiwe sehemu ya machafuko hususan ni vijana ambao wao ndio hutumika vibaya mara nyingi,’’alieleza.

Akielezea mradi wa uraia wetu, Mratibu wa miradi kutoka Mwemvuli wa asasi za kiraia Pemba ‘PACSO’ Mohamed Najim Omar, alisema uraia wetu ni mradi wa kukuza mazingira wezeshi, kwa asasi za kiraia zenye uwezo wa kushiriki, katika utawala wa kidemokrasia nchini.



Mradi huo unaofadhiliwa na ‘the foundation for Civil society’ na kutekelezwa na   ‘PACSO’ kwa Pemba na kituo cha majadiliano kwa vijana ‘CYD’.

Alieleza kuwa, mradi huo umegawika maeneo matatu makuu, ikiwemo ngazi ya kitaifa, taifa na utekelezaji kwenye makundi maalum, wakiwemo wanawake na vijana.

Kwa ngazi ya kitaifa, mradi unatekelezwa na asasi kadhaa ikiwemo Jukwaa la Katiba Tanzania ‘JUKATA’, Tanganyika law society kwa upande wa Tanzania bara na JUWAUZA kwa Zanzibar.

‘’Kupitia mradi huu, tayari tumeshakutana na makundi ya watu wenye ulemavu, wanawake, vijana, waandishi wa habari na maafisa wa serikali, nao waliibua changamoto zao za kisheria na kisera,’’alifafanua.

Akizungumzia lengo la mradi, Mratibu huyo alisema ni kuchangia kuwepo kwa mfumo wa sera na kisheria, ambao umeimarishwa na kuwezesha mazingira mazuri ya ushirikishwaji wa asasi za kiraia, kama watendaji wakuu wa utawala bora na demokrasia.

 



Katibu Mkuu wa ‘PACSO’ Sifuni Ali Haji, alisema lengo la mjadala huo, ni kuibua changamoto hizo na kuzifanyia kazi.

Alisema, ‘PACSO’ kwa sasa inaendelea na utekelezaji wa mradi wa urai wetu, ambapo moja ya eneo la utekelezaji wake, ni kuibua changamoto za kisheria na sera, zinazokwaza makundi ya vijana, wanawake na watu wenye ulemavu.

Akiwasilisha changamoto za kisera na sheria zilizowasilisha Novemba 3,  mwaka huu mwanaharakati Juma Bakar Alawi, alisema moja ya changamoto hizo ni makampuni kutowapa mikataba watendaji wao.



Alisema jingine ni kuwepo kwa vifaa vya sayansi katika skuli za sekondari ambavyo vimeshapitiwa na muda wa matumizi, na kukosa kuteketezwa.

Mjadala huo, ni sehemu ya utekelezaji wa mradi wa ‘uraia wetu’ unaotekelezwa na ‘PACSO’ kwa muda wa miaka minne, kwa ufadhili wa ‘the foundation for civil society’ kupitia Umoja wa nchi za Ulaya ‘EU.

                       Mwisho 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kuta...