Skip to main content

‘UWT’ KUSINI PEMBA: '‘ZIARA YA MAKAMU MWENYEKITI WETU ILIKUWA YA KISAYANSI’

  


NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

UONGOZI wa Umoja wa wanawake wa CCM ‘UWT’ mkoa wa kusini Pemba, umesema ziara iliyofanywa hivi karibuni na Makamu Mwenyekiti wa umoja huo taifa Zainab Khamis Shomari, imekuwa ni darsa tosha, kuelekea ushindi wa CCM hapo mwakani.

 

Hayo yameelezwa na Mwenyekiti wa umoja huo mkoani humo, Zuwena Khamis Abdalla, alipokuwa akizungumza hivi karibuni, kufuatia kumalizika kwa ziara ya Makamu Mwenyekiti huyo, mkoani mwake.

 

Alisema ujio wake, umewaamsha na kuendeleza mbele umoja huo na chama kwa ujumla, kwani ametoa maagizo ambayo kama yakifanyiwa kazi, CCM itaendelea kuweka historia ya ushindi katika kila uchaguzi.

 

Alieleza kuwa, moja ambalo wanalikumbuka ni kuwataka viongozi wa UWT mkoa, wilaya na hadi shina kuhakikisha wanaongeza idadi ya wanachama wa CCM.

 

Alifahamisha kuwa, hilo ni jambo la msingi ndani ya UWT, na hivyo ni lazima viongozo wote hadi ngazi ya mkoa, kulitekeleza kwa vitendo agizo la Makamu Mwenyekiti huyo.

‘’Ni kweli ziara ya Mheshimiwa Zainab, imetuachia darsa na ukumbusho kwetu sisi viongozi wa ‘UWT’ na hata wanachama wa kawaida, na moja hili la kuongeza idadi na wanachama wapya,’’alisema.

 


Aidha Mwenyekiti huyo wa ‘UWT’ Mkoa wa kusini Pemba, alisema agizo jingine ni kuhakikisha, wanaUWT na wanaCCM kwa ujumla, wanaendelea kuwa waalimu wa kuvielimisha vyama vingine, juu ya maendeleo yaliopo.

 

‘’Alituambia, sisi UWT na jumuia nyingine ndani ya chama, tusiwe tunapiga kelele ovyo, na badala yake tuwaonesha wale wingine maendeleo yaliofanywa na Dk. Mwinyi na Mama Samia,’’alisisitiza.

 

Katika hatua nyingine Mwenyekiti huyo wa UWT mkoa wa kusini Pemba, Zuwena Khamis Abdalla, alisema watalifanyia kazi, agizo alilolitoa kuwataka ambao hawajajikusanya kwenye vikundi vya ushirika, kufanya hivyo.

 

‘’Alisema hadharani kuwa, sasa ule mkwamo kwa baadhi ya vyama ya ushirika hasa eneo la mashrti katika upatikanaji mikopo, wameshazungumza na serikali, hivyo ni jukumu la wananchi kujikusanya na kujisajili, ili kuiomba mikopo hiyo,’’alisema.

 

Nae Katibu wa UWT mkoani humo Asila Ali Salim, alisema ziara hiyo sio tu kupokea maagizo hayo na kuyafanyia kazi, bali imesaidia uhai wa ‘UWT’ na chama kwa ujumla.


 


‘Unajua tunapokuwa na viongozi wanaotutembelea kwenye maeneo yetu ya kazi kama hivi, kuanzia sisi viongozi na wanachama, huhamasika zaidi kutekeleza majukumu yetu, kwa hili tunampongeza Makamu Mwenyekiti,’’alieleza.

 

Aidha alieleza kuwa, jambo jingine ambalo limewapa moyo, ni pale alipozungumza na wajasiriamali, katika ukumbi wa Manispaa ya jiji la Chake chake, na kuwapa moyo zaidi.

 


‘’Unajua Mwakamu Mwenyekiti wetu wa UWT, ziara yake ilikuwa ya kisayansi zaidi, maana pamoja na kuzungumza na wanaUWT, lakini alitembelea pia soko la Machomane na kuacha maagizo,’’alifafanua.

 

Akiwa katika mkoa wa kusini Pemba, Makamu huyo Mwenyekiti wa Umoja wa wanawake wa CCM Tanzania ‘UWT’ Zainab Khamis Shomar, alipata nafasi pia ya kukabidhi piki piki mbili, kwa ajili ya ofisi za UWT za wilaya ya Chake chake na Mkoani.

 

Wakati huo huo Makamu Mwenyekiti huyo, alivieleza vyama vyingine vya siasa kuwa, daima CCM, itaendelea kuhubiri amani na utulivu, maana ndio mwalimu wa vyama vingine nchini.

 

Alisema, CCM baada ya kuwahudumia wananchi wote wa Tanzania bila ya ubagauzi, msingi wake mwingine mkuu ni kuhubiri umoja, mshikamano, amani na utulivu kwa nia ya kuwaunganisha watu wote.

 


Aidha aliwataka viongozi wa UWT, kuanzia ngazi ya shina hadi taifa kuendelea kuhubiri jambo hilo, kwani ndio msingi mkuu kwa chama hicho, tokea kuasisi kwake.

 

‘’Sisi UWT na jumuia nyingine za chama, tumekuwa tukihimiza kila siku, kuwa ajenda yetu ya kwanza iwe ni kuhubiri amani na utulivu, kisha kuleta maendeleo kwa kila mtu,’’alifafanua.

 

Aidha Makamu Mwenyekiti huyo wa UWT taifa Zainab Khamis Shomar, aliwapongeza rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. Samia Suluhu Hassan na Dk. Hussein Ali Mwinyi wa Zanzibar, kwa kuchapuza miradi ya maendeleo.

 


Alieleza kuwa, tayari Dk. Mwinyi kwa upande wa Zanzibar ameshavuuka lengo la utekelezaji wa Ilani ya CCM ya mwaka 2020/2025, katika miradi kadhaa, aliyowaahidi wananchi wakati akiomba ridhaa.

 

‘’Kwa mfano, aliahidi ujenzi wa vyumba 1,500 vya madarasa, wakati wa kampeni ingawa ndani ya miaka yake mitatu ya utawala ameshajenga vyumba 2,273 hapa ameshavuuka lengo kwa asilimia 150,’’alifafanua.

 

                       Mwisho    

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

…….SUZA WATOA USHAURI WA ADHABU YA KUNYONGWA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WANAFUNZI wanaosomea uwalimu Chuo cha taifa cha Zanzibar ‘SUZA’ kampasi ya Benjamin Wiliam Mkapa Wete Pemba, wamependekeza adhabu ya kunyongwa hadi kufa, kwa mtu atakaetiwa hatiani, kwa kosa la dawa za kulevya. Walisema, haiingii akili kuona, mahkama imeshamtia hatiani mtu kwa kukutwa na dawa za kulevya, ambazo huathiri nguvu kazi ya taifa na kisha, kupewa hukumu ya kifungo pekee. Wakizungumza leo Juni 26, 2024 kwenye kongamano la vyuo vikuu, juu ya masuala ya msaada wa kisheria, kuelekea wiki ya msaada wa kisheria Zanzibar, lililofanyika Chuoni hapo, walisema wakati umefika sasa kutolewa kwa hukumu hiyo. Walipendekeza kuwa, ni vyema kwa mtu anayetiwa hatiani asibakie chuo cha Mafunzo pekee kuitia tena hasara serikali kwa chakula na wakati mwingine matibabu, wakati tayari ameshasababisha madhara, kwa vijana. Mshiriki Juma Nafasi Juma, alifafanua kuwa kama mtu ameamua kuliumiza taifa kwa kuingiza, kusafirisha, kusambaaza dawa za kulevya, hivyo ni vy

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan