Skip to main content

RAMLA: MWANAMKE ANAYEPAMBANIA SOKA KWA WANAWAKE, APITIA CHANGAMOTO LUKUKI

 


NA HABIBA ZARALI, PEMBA@@@@

‘MWANZO wa kuanza mchezo huu, nilipata changamoto kubwa na kuambiwa nacheza mchezo wa kiume, wa kihuni lakini sikuvunjika moyo’.

Hayo ni maneno ya kocha wa mpira wa miguu timu ya Mkoani Qunes, Ramla Khamis Juma aliyenza kwa kutandaza soka hapo awali.

Kocha Ramla  aliyasema maneno hayo wakati akizungumza na makala haya huko katika uwanja wa mpira wa miguu Mpikatango Mkoani kisiwani Pemba, wanapofanyia mazoezi.

Akinisimulia sababu ya kupenda michezo ni pale alipokuwa skuli ya msingi Ngwachani, akiwa darasa la sita baada ya kuwaona wanafunzi wenzake wakishiriki michezo mbalimbali ikiwemo mpira wa pete ‘netball’.

Wakati akiingia skuli ya Sekondari Uweleni, alikuwa anachezea timu ya netball ya wilaya, ndipo hapo hapo alipoanza kujifunza kucheza mpira wa miguu.

“Kwa vile mchezo wa mpira wa miguu kwa wanawake, ilikuwa haujazoeleka wilaya ya Mkoani na ni ajabu, ambapo wengi walishangaa na kunikataza lakini haikuwa lolote mimi niliendelea kujifunza,”alisema.

Baadae alikwenda kujiunga na Chuo kikuu cha Zanzibar ‘SUZA’ kisiwani Unguja, na baada ya kurudi Pemba ndipo aliposhawishiwa na rafiki yake anaeitwa Maida, kwenda kujifunza mchezo wa mpira wa miguu.

Na baada ya kumaliza kusoma na kurudi Pemba mwaka 2012, akaanza mchakato wa kuanzisha timu ya mpira wa miguu ya ‘Mkoani Queens’ mwaka 2014 na hadi leo inaendelea.

Akimtaja mwenzake ambae walibahatika kuchaguliwa kufudishwa mchezo huo ni Maida Mohamed Salum ,ambapo wote wanaendelea na  mpira huo.

Alianza kufundisha vijana mchezo huo wakiwa katika mazingira magumu, jamii haielewi wanachokifanya maneno na kejeli nyingi ingawa  hawakuvunjika moyo.

“Lakini kwa hatuwa ya mwanzo tulifundisha tukiwa hatuna vifaa vyovyote, ilikuwa ni duni mipira hatuna ni ya kubaka baka tu hakuna wadhamini,”anasema.

Pamoja na mazingira magumu ya mchezo huo, lakini waliendelea na kufundisha vijana kucheza wakiwa na kocha Mohamed Juma.

Anazidi kusimulia wakati wakiendelea na mchezo huo, jamii iliyowazuguka mwanzo haikukubali mchezo huo, na hapo ndipo, maneno kadhaa yaliweza kutoka kwa wanajamii kuwa mchezo wa mpira wa miguu.



 ‘’Kwa wanawake ni haramu, ukafiri, uhuni, umalaya, ingawa maneno hayo hayakufua dafu kwake,’’anafafanua.

 ‘Ingawa hakuna aliyekatisha njiani, kwani nilikuwa nashajihisha kwelikweli na mimi sikuvunjika moyo niliendelea mwanzo mwisho, hadi vijana wakaweza kucheza,”anaeleza.

Kumbe kila siku zinaposonga, wanachukuwa ushauri kwa Shirikisho la mpira wa Miguu Zanzibar ‘ZFF’  na siku zikisonga wanacheza kirafiki na timu ya Mkoa wa Kaskazini Wete.

Tumu nyingine ni za vijana chini ya umri wa miaka 17 za watoto wanaume ni kwa sababu hakuna timu ya wanawake kwa karibu.

Wakati akiwa katika ligi timu yake, iliwahi kushindana na timu ya New generation, ambayo ilikuwa ni tishio kwa Zanzibar, ingawa walifungwa mabao 3, lakini nao walijipinda na kuwaingia kwa goli moja la kufutia machozi.

“Watu walitushangaa na kutupongeza kwa sababu timu ya New generation, ilikuwa inatambana haifungwi lakini sisi tulipata goli moja,”alisema.


Anasema kwa vile mchezo huo ulikuwa dani ya moyo na damu yake, hakuridhika na kufungwa, ndipo alipoamuwa kushajihisha, ili waweze kupata ushindi.

‘Nakumbuka kila tunapocheza na timu yoyote ile  tutapambana, lakini tufunge na tukishindwa sawa lakini si kwa bila,”alisema.

Anasema ni jambo linalomuhuzunisha sana kuona timu hiyo inasuasua kwa namna moja ama nyingine na ndio maana, hutowa fedha zake mkononi kuhakikisha timu inasonga mbele.

Akitaja mafanikio anasema ni pamoja na kutambua kwa jamii ya Mkoani kuwa timu ya mpira wa miguu, ipo na kuwa na uelewa japo si kwa kiasi kikubwa.

Anasema jingine ni kutowa vijana nje ya Zanzibar hadi baadhi ya mikoa ya Tanzania Bara, kwa ajili ya kushiriki na kucheza.

Mafanikio mengine ni vijana wengi kuhudhuria mafunzo ya mpira wa miguu kupitia ZFF, kujiunga na timu ya taifa ya Zanzibar kwenda Kenya, kupata ajira kwenye serikali kupitia mchezo huo.

Kocha Ramla aliwahi kupata mafunzo mbalimbali ya ukocha, kupitia ZFF ambapo walikuja wakufunzi kutoka ndani na nje ya Zanzibar, kujifunza uwalimu wa soka kwa watoto wa kike.

‘Nilitamani niwe kama kocha Hatma Mwalim Khamis wa timu ya taifa ya Zanzibar, kutokana na utendaji wake mzuri, ufuatiliaji na ‘usmati’,’’anasema.



Anataja changamoto na kusema kwenye mchezo huo hakuna wafadhili, na hulazimika kutembeza bakuli, uhaba wa timu za mpira wa miguu za wanawake hasa kisiwani Pemba.

Uhaba wa mashindano ya mara kwa mara na mabonanza, umasikini wa familia za Watoto, jambo  ambalo liliifanya timu hiyo kutoshiriki ligi kuu ya soka la wanawake Zanzibar mwaka 2024/2025.

Nafasi alizowahi kukamata ni mjumbe wa Wilaya kamati tendaji Wilaya ZFF, kamati tendaji Mkoa, kamati tendaji taifa soka la wanawake Zanzibar.

Jambo ambalo hatoweza kulisahau, ni kule kuuanzisha mpira huo wilaya ya Mkoani, kuifunga timu New generation amabayo ni maarufu na mabingwa kwa mchezo huo Zanzibar.

Endapo atapata msaada (support) matarajio yake ni kuupeleka mchezo huo katika baadhi ya skuli wilaya ya Mkoani, ili waweze kuuendeleza.

Akitowa ushauri wake, anaiomba serikali kuongeza mkazo zaidi kuwaendeleza vijana wa kike hasa Pemba, kwani vipo vipaji vigi tokea mwaka 2014 ilipoanzishwa Mkoani Queens, bado hakuna timu nyengine wilayani humo.



Kocha Ramla alizaliwa mwaka 1986, ni mtoto wa tatu kwa mama Zainab na kwa baba ni mtoto wa tisa na hadi sasa mtoto wake wa kiume, Ibrahim miaka 13 ndie ambae anaonekana kumrithi.

Ibrahim yuko katika timu ya matayarisho ya watoto chini yamiaka 16, ambapo anamuona na hamu  na hamasa kubwa ya kushiriki mazoezi bila kuhimizwa.

 Akimzungumzia Kocha Ramla, mmoja wa wanawake wanaosiamia mpira wa miguu Zanzibar Hatma Mwalim Khamis, anasema ni mwanamke anaejitolea kwa hali na mali, kuhakikisha mpira wa miguu unasonga mbele.

Kocha Ramla kakulia kimichezo humlazimu kutowa chake cha mfukoni, alimradi mchezo uendelee kwani ni mmoja anaeonesha kuukubali mchezo huo

‘Sifa ya Ramla hakuwa mtu wa kukata tamaa na aliweza kujitia moyom na kuukubali mchezo wa mpira wa miguu, tokea akiwa mwanafunzi hadi leo tayari ni kocha wa kuaminika,’’anamsifia.

Mohamed Juma ni mmoja wa walimu walioanza kufundisha pamoja na kocha Ramla, anasema ingawa walianza pamoja kufundisha ilipoanzishwa timu hiyo lakini Ramla, hakusita hadi leo ni kocha bora.

Anasema wanajivunia kuwa katika wilaya ya Mkoani, wamekuwa wanasifikana kupitia mchezo huo chini ya kocha Ramla, kwani anaongoza timu hiyo, na kuhudhuria vikao kadhaa.

Anasema ni vyema makocha wakatambulika na wapatiwe nafasi za kusoma ukocha, hasa kwa wale wenye malengo ya kuendeleza mchezo.

Mmoja wa wachezaji wa timu hiyo Hamida Juma Amani anasema miongoni mwa sifa za kocha Ramla ni mstaarabu mwenye kueleweka wakati anapofundisha.

“Kocha wetu hatuachi mkono tunapokuwa na shida huwa nasi bega kwa bega na ndio maana tunamkubali,”anasema.

Afisa mradi wa kukuza usawa wa kijinsia na ujumuishi kwenye michezo unaofadhiliwa na shirika la maendeleo  la kimataifa la Ujerumani Khairat Haji,  anasema kila mtu anayo haki ya kushiriki katika michezo na hakuna sababu ya  wanawake kubakia nyuma.

Ndio maana anasema kupitia mradi huo TAMWA Zanzibar itahakikisha usawa wa kijinsia, unapatikana katika michezo ya aina mbali mbali.

Pamoja na kuwa  wanawake wako nyuma katika ushiriki wa michezo, aliwataka wasirudi nyuma na washiriki kwa hali ya kuridhisha.

Ili vijana wa kike waweze kukua kimichezo ni vyema Shirikisho la mpira wa miguu Zanzibar ‘ZFF’ lianzishe mashindano mbalimbali pamoja na mabonanza, kwani bila ya kuutangaza mchezo huo hautokwenda mbele.

                         MWISHO...

 

 

 

  

 

 



Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

…….SUZA WATOA USHAURI WA ADHABU YA KUNYONGWA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WANAFUNZI wanaosomea uwalimu Chuo cha taifa cha Zanzibar ‘SUZA’ kampasi ya Benjamin Wiliam Mkapa Wete Pemba, wamependekeza adhabu ya kunyongwa hadi kufa, kwa mtu atakaetiwa hatiani, kwa kosa la dawa za kulevya. Walisema, haiingii akili kuona, mahkama imeshamtia hatiani mtu kwa kukutwa na dawa za kulevya, ambazo huathiri nguvu kazi ya taifa na kisha, kupewa hukumu ya kifungo pekee. Wakizungumza leo Juni 26, 2024 kwenye kongamano la vyuo vikuu, juu ya masuala ya msaada wa kisheria, kuelekea wiki ya msaada wa kisheria Zanzibar, lililofanyika Chuoni hapo, walisema wakati umefika sasa kutolewa kwa hukumu hiyo. Walipendekeza kuwa, ni vyema kwa mtu anayetiwa hatiani asibakie chuo cha Mafunzo pekee kuitia tena hasara serikali kwa chakula na wakati mwingine matibabu, wakati tayari ameshasababisha madhara, kwa vijana. Mshiriki Juma Nafasi Juma, alifafanua kuwa kama mtu ameamua kuliumiza taifa kwa kuingiza, kusafirisha, kusambaaza dawa za kulevya, hivyo ni vy

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan