Skip to main content

WANAFUNZI CONNECTING: 'ZITUMIENI WIKI ZILIZOBAKI KABLA YA MTIHANI WA TAIFA MTAFANIKIWA''

 



NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

MWALIMU Mkuu wa skuli ya sekondari ya Connecting Continent, iliyopo Mgogoni wilaya ya Chake chake Pemba, Mwache Juma Abdalla, amewataka wanafunzi wa darasa la kumi na mbaili skulini hapo, kuzitumia kwa maandalizi ya hali ya juu, wiki 11 zilizobaki, kabla ya kufanya mtihani wao wa taifa.

Alisema, wiki hizo sio kidogo, kwa mwanafunzi kama ataweka pembeni uvivu, kudorora, kushughulikia anasa na kujikita kwenye masomo, hivyo anaweza kufanya vizuri, kwenye mtihani wa taifa.

Mwalimu mkuu huyo, aliyasema hayo leo Augost 24, 2024 skulini hapo, kwenye kikao cha wazazi na wanafunzi hao, cha kutoa matokeo ya mitihani ya majaribio ya kimkoa ‘MOCK’ yaliofanyika hivi karibuni.

Alisema, bado wanafunzi wanayonafasi ya kujiandaa na mitihani hayo, kwani waalimu wameshamaliza mtaala waliopangiwa, na sasa ni kazi wanafunzi wenyewe.

Alieleza kuwa, waalimu wamekuwa wakitumia jitihada binafsi ili kuhakikisha wanamaliza mitaala mapema, na sasa ni kazi ya wanafunzi kuangalia mitihani iliyopita.

‘’Tumebakiwa na wiki 11 kabla ya kukutana na mitihani ya taifa, sasa wanafunzi muongeze bidii, waalimu wapo kwa ajili yenu na wengine hata majumbani hawarudi kwa wakati,’’alieleza.

Akizungumzia kuhusu mitahani hayo ya majaribio, alisema skuli hiyo imekuwa na dara la tatu (c), ingawa matokeo hawakuridhika nayo kwa kiasi fulani.

‘’Matokeo ya ‘MOCK’ yameshatoka, lakini kiujumla sisi waalimu yametuhuzinisha, maana jitahada za waalimu ni kubwa, ingawa wanafunzi wanaoneka kuwa wavivu,’’alifafanua.

Hata hivyo Mwalimu huyo mkuu, alisema matokeo hayo sio mabaya sana, maana hakuna mwanafunzi aliyepata kiwango cha alama sifuri wala daraja la nne.

Mapema Mwenyekiti wa bodi ya wazazi ya skulini hapo Dk. Said Mohamed, alisema bado wazazi wanayonafasi ya kukaa na watoto wao, na kujua ni chanzo cha mtoto wake kufeli.

‘’Mzazi anayonafasi kubwa mno, kuhakikisha mtoto wake anaongeza juhudi na kisha anakuwa na matokeo mazuri kwenye mitihani ya taifa,’’alieleza.

Katika hatua nyingine Mwenyekiti huyo, alipongeza juhudi za waalimu skulini hapo, ambazo zimesaidia skuli hiyo kuendelea kujiwekea historia, ya kutokuwa na daraja la nne.



Mwalimu Khamis Mohamed, alisema kasoro anayoiona kwa wanafunzi hao, ni kutoelewa wajibu wao, hasa kwa yale madarasa yenye mitihani.

‘’Wanafunzi sio wabaya kiakili, ila changamoto iliyopo wapo wasiofahamu wajibu wao, na hili linahitaji nguvu pia za wazazi na walezi, maana mwalimi pekee, mwanafunzi hatofanikiwa,’’alishauri.

Mzazi Khamis Ali Juma, aliwashauri waalimu skulini hapo, kuweka mkazo wa ufahamu ya lugha ya kiengereza, kwani ndio msingi wa masomo kadhaa.

Asha Saleh Juma, alielezea kusikitishwa kwake na ufaulu mdogo wa somo la hesabati, na kuwataka wanafunzi kuacha woga, kwani somo hilo ni rahisi.

Mzazi Mohamed Juma, aliwataka wanafunzi kuongeza bidii, kwani kila kitu kinawezekana kufanikiwa, ikiwa mfanyaji atajielewa.

Wanafunzi 81 waliofanya mitihani ya majaribio ya ‘MOCK’ skulini hapo, waliopata daraja la kwanza ni wanane, daraja la pili 22, daraja la tatu 36, daraja la nne 15 na hakukua na mwanafunzi aliyepata daraja la mwisho.

Kati ya masomo 11, ambayo wanafunzi hao 81, waliyapasi kwa wingi ni masomo ya kiswahili walipasi wote 81, somo la uraia wanafunzi 79, dini ya kiislamu 79, Jiongrafia 78, english 72, chemia 65.

Kwa mitihani kama hayo ya mwaka 2023, wanafunzi wote walikuwa 53, ambapo hakukua na aliyefeli, na hakukua na mwanafunzi aliyepata daraja la nne.

Ambapo kwa mitihani ya taifa, kati ya wanafunzi hao, sita walipata daraja la kwanza, ambao ndio walioungana na wenzao juzi kula chakula cha pamoja na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi.

                  Mwisho

  

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

…….SUZA WATOA USHAURI WA ADHABU YA KUNYONGWA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WANAFUNZI wanaosomea uwalimu Chuo cha taifa cha Zanzibar ‘SUZA’ kampasi ya Benjamin Wiliam Mkapa Wete Pemba, wamependekeza adhabu ya kunyongwa hadi kufa, kwa mtu atakaetiwa hatiani, kwa kosa la dawa za kulevya. Walisema, haiingii akili kuona, mahkama imeshamtia hatiani mtu kwa kukutwa na dawa za kulevya, ambazo huathiri nguvu kazi ya taifa na kisha, kupewa hukumu ya kifungo pekee. Wakizungumza leo Juni 26, 2024 kwenye kongamano la vyuo vikuu, juu ya masuala ya msaada wa kisheria, kuelekea wiki ya msaada wa kisheria Zanzibar, lililofanyika Chuoni hapo, walisema wakati umefika sasa kutolewa kwa hukumu hiyo. Walipendekeza kuwa, ni vyema kwa mtu anayetiwa hatiani asibakie chuo cha Mafunzo pekee kuitia tena hasara serikali kwa chakula na wakati mwingine matibabu, wakati tayari ameshasababisha madhara, kwa vijana. Mshiriki Juma Nafasi Juma, alifafanua kuwa kama mtu ameamua kuliumiza taifa kwa kuingiza, kusafirisha, kusambaaza dawa za kulevya, hivyo ni vy

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan