Skip to main content

WADAU WATAJA DARZENI YA CHANGAMOTO ZINAZOWAKWAMISHA WATOTO WA WAKIKE MICHEZONI

 

HABIBA ZARALI, PEMBA@@@@

MICHEZO ni sehemu muhimu katika utamaduni wa kila jamii ya binadamu kote duniani.

Michezo iko ya aina nyingi, ambayo jamii ya makabila tofauti hushiriki kutokana na utamaduni walionao na kwa madhumuni tofauti.

Pamoja na michezo kuwa na faida lukuki, ikiwemo kupata ajira,  kujenga afya ya mwili na akili, kuburudisha, kuelimisha, kutambulisha, kujenga ukakamavu, kuonesha vipaji na kujenga urafiki, lakini bado jamii iko nyuma kwa hilo.

Ingawa hakuna tamko linaloonesha kuwa watoto wa kike hawapaswi kushiriki katika michezo, ingawa bado hali haijaridhisha.

Sera ya maendeleo ya michezo 2018 imeonesha hali ya sasa tangu kuanzishwa kwa wizara yenye dhamana ya michezo na baraza la michezo la taifa, maendeleo katika maeneo mbalimbali ya michezo yamepatikana.

Sera hiyo haikumbaguwa mtu yoyote kushiriki michezo na kuonesha kuwa, michezo mingi mipya imaenzishwa na kuleta mafanikio makubwa kulingana na vipaji na uwezo walionao wananchi.

Ambapo nayo Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984, kifungu cha 11  kimeeleza  kuwa binadamu wote ni sawa, na kifungu cha 12 kikaweka usawa ndani ya sheria.

Katika makala haya, inaangazia chanagamoto za watoto wa kike kuwa na ushiriki mdogo katika michezo.

WADAU WA MICHEZO

Mwenyekiti wa Shirikisho la mpira wa miguu ZFF Mkoa wa Kusini Pemba Nassor Hakim Haji, anasema kutokuwa na mazingira mazuri yaliyoandaliwa kuhusu watoto wa kike, kujishirikisha na michezo inachangia watoto hao kuwa na ushiriki mdogo.

Anasema mchanganyiko kati ya wanaume na wanawake katika viwanja vya michezo, ni jambo moja linalowarejesha nyuma huku ikizingatiwa wazazi bado mwamko wao ni mdogo.

Anasema kwa upande wa jamii, bado haijawa tayari kuona ushiriki wa wanawake katika masuala ya michezo kwani wao ndio chanzo cha kupiga kelele na kuweka dhana potofu kwa michezo ni uhuni.

“Mimi katika wanafunzi wangu nilionao tayari watatu wamefanikiwa kupata ajira kupitia michezo, wawili wako Jeshi la Polisi na mmoja mwanajeshi na si hao tu wako wengi,’’anasimulia.

Kocha wa mpira wa kikapu ‘basketball’ wilaya ya Mkoani  Mohamed Salim Khamis (Gabs) anasema, kutokuwa na uwanja maalum kwa watoto wa kike hasa katika hatuwa za awali kunapelekea ushiriki kuwa mdogo.

Anasema uwanja mmoja ambao wanacheza wanaume ndio huohuo wanaochezea wanawake huku ukiwa sehemu ya uwazi ni jambo jingine, linalowapelekea watoto wa kike kujiskia aibu na kukataa kujishiriki michezo.

Jambo jengine ni uhaba wa walimu kwa upande wa basketball ambapo kwa upande wa wilaya ya Mkoani, hakuna timu pinzani ambayo watashindana kirafiki ama kujipima hadi wafunge safari wilaya ya Chake chake au Wete.

Changamoto nyingine anasema ni ,muono finyu wa jamii kuhusu watoto wa kike, kushiriki michezo huku wakiwa na dhana ya kuwa ni uhuni.

“Na kuhusu mchezo wetu huu vifaa vyake ni ghali sana ikiwemo viatu , mipira, jezi, koni ‘Cones’ haya yote kwa watoto wa kike kwao ni sehemu ya changanamoto,’’anafafanua.

Kocha wa mpira wa miguu wanawake Ramla Juma Khamis anasema wazazi wengi wako nyuma, kuelewa faida zilizomo katika michezo na kupelekea kuwakataza watoto wao kushiriki.

Anasema pamoja na kuwa dini haikukataza wanawake kushiriki michezo, ingawa bado baadhi ya viongozi wa dini wanakuwa na tafsiri tofauti, ambayo inawarejesha nyuma watoto wa kike kushiriki michezo.

‘Huekwa mihadhara katika mitaa na kuzungumzia jinsi ya watoto wa kike wanavyojishirikisha na michezo kwa kisingizio cha kuwa watakuwa wahuni,’’alisema.



Mwalimu wa michezo skuli ya Sekondari Uweleni Abdull Ali Abdalla, anasema jamii inahitaji kupewa elimu ya kutosha kuhusiana na umuhimu wa michezo kwa watoto wa kike.

Alisema kuna tamaduni zilizowagubika wana jamii na kuona kuwa watoto wa kiume ndio wanaostahiki kujishughulisha na michezo pekee, kuliko wa kike linapaswa kufahamishwa.

WATOTO WA KIKE WANASEMAJE

Maimuna Fatawi Khamis, mwanafunzi wa kidato cha nne skuli ya sekondari Uweleni anasema baada ya kujishirikisha na michezo alikatazwa na wazazi wake kwa kisingizio cha uhuni, na jamii iliyomzunguka ili mbeza na kumuambia michezo haina faida.

Nassra Ali Sheha ni mwanafunzi kutoka skuli ya sekondari ya Uweleni, anasema baada ya kuanza kujishirikisha na michezo alikatazwa na wazazi wake, kwa kisingizio cha kuwa michezo ni uhuni.



Kwa vile alikuwa tayari keshavutika na michezo baada ya kuwaona wenzake wanacheza, aliamuwa kuendelea na sasa anamekuwa tofauti hata katika ufahamu wake wa masomo yake.

“Naamini kama michezo inajenga akili, kwani nimekuwa na utofauti mkubwa kabla sijaingia katika michezo na sasa, nimeweza kujuwana na watu wengi tunapokwenda kushindana,”anasimulia.

Fatma Massoud Kombo anasema awali wa kujulikana kuwa anashiriki katika michezo, aliambiwa hatoweza kufaulu kwani akili yake ataitowa kwenye kushughulikia masomo, jambo ambalo aliliona sio kweli.

Anacheza mpira wa pete ‘netball’ akiwa skuli na hata mchezo wa nage anapokuwa nyumbani, lakini hali yake ya masomo yake haijaathirika.

WAZAZI WANASEMAJE

Salma Suleiman wa Mkoani anasema, ili watoto wa kike waweze kuwa na ushiriki sawa na wanaume, lazima wawekewe mazingira sawa kuanzia viwanja  na hata mavazi.

Anasema wapo watoto wa kike wanaoshiriki michezoya aina mbalimbali lakini utamaduni haukubaliani iwapo watachanganyika pamoja na wanaume.

“Sisi wazazi hatuoni furaha kwa watoto wetu wakike kuona wanafanya jambo, lenye viashiria vibaya na tunasema lakini hebu serikali ifanye kuwaona watoto hawa wa kike, katika mazingira ya mazuri kwenye michezo”,anashauri.

Saumu Omar wa Kiwani, anasema mtoto wake wa kike aliacha kushiriki michezo akiwa skuli, baada ya kufanyiwa istizai na watoto wa kiume, lakini kama kungelikuwa na kiwanja maalum kwa ajili yao, engendelea.

Anasema bado jamii inahitaji kuelimishwa kuhusiana na umuhimu wa mtoto wa kike kujishirikisha na michezo, ili nao waweze kupata faida.

“Tunaona kama michezo inasaidia ana katika upatikanaji wa ajira, lakini jamii ilotuzungumka bado haina mwamko huo mtoto wako anapoingia kwenyemichezo, siku chache unaekewa vikao jambo ambalo siosahihi,’’anaeleza.

Kombo Shaibu wa Mwambe anasema  tokea enzi ya wazazi haikuonekana kama ipo haja kwa mtoto wa kike kujishirikisha na michezo .

Anasema ni jambo la busara kwa serikali ama taasisi zinazojishughulisha na michezo kuelimisha jamii kuhusiana na umuhimu wa watoto wa kike, kushiriki michezo mbalimbali.

VIONGOZI WA DINI WANASEMAJE

Sheikh Said Ahmad kutoka ofisi ya Mufti, anasema dini ya kiislam haijambagua mtu kushiriki kwenye michezo, kutokana na jinsia yake.

“Dini imeweka wazi watu wafanye mazoezi, ili kuweka mwili sawa na kuisitiza kufuata taratibu ikiwemo kuvaa nguo za stara,”anasisitiza.

Mchungaji Samwel Elias Maganga wa kanisa la Makangale anasema hata dini ya kikiristo, nayo haijamkataza mwanamke kujishirikisha na michezo, ila maadili yazingatiwe.

Michezo ni vitu vinawafanya watu wasahau chanagamoto zilizowapata watuna kuwakusanya pamoja na hilo linatokea tokea mtu anapokuwa mtoto kwani viungo vyake hukuwa kupitia michezo.

“Michezo ni ya watu wote na hata ulimwengu kutoka nchi moja na nyingine, unaunganika kupitia michezo,”alisema.

TAMWA ZANZIBAR                                                                         

Afisa mradi wa kukuza usawa wa kijinsia na ujumuishi kwenye michezo Khairat Haji, anasema baada ya kuona watoto wa kike wako nyuma katika suala la michezo, ndipo kupitia mradi wa michezo kwa maendeleo, imeona ipo haja ya kushirikiana na vyombo vya habari kuibua chanagamoto za aina hiyo.



‘’Ni kweli  watoto wa kike wako nyuma katika ushiriki wa michezo na kuwataka waandishi wa habari kuhakikisha wanatumia kalamu zao, kulisemea ili kuondoa mawazo finyu kwa jamii, kuwa watoto wa  kiume ndo wanaofaa kushiriki michezo pekee,’’anasisitiza.

Lengo la mradi huo unaofadhiliwa na shirika la maendeleo la kimataifa la Ujerumani, ambao unatekelezwa na jumuiya ya wanasheria wanawake Zanzibar ‘ZAFELA’, kituo cha majadiliano kwa vijana ‘CYD’ ni kuhakikisha wanawake wanashiriki katika michezo kwa hali ya kuridhisha.



‘Kwa vile kila mtu anayo haki ya kushiriki katika michezo, kwa nini wanawake wabakie nyuma na tutahakikisha usawa wa kijinsia unapatikana katika michezo,’’anaeleza.

WIZARA HUSIKA INASEMAJE

Mkuu wa divisheni ya michezo na utamaduni Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Pemba Mzee Ali Abdalla, anasema kupitia skuli, watoto wote wanashirikishwa na hawabaguliwi.

 Anasema watoto wanapokuwa masomoni, wanasomeshwa sawa somo la sanaa na ubunifu, kwa nadharia na vitendo kwa pamoja kati ya wanawake na wanaume.

“Tunaposhiriki katika mashindano ya elimu bila malipo tunakuwa nazo timuza wanaume na wanawake, bila yaubaguzi na fursa zote zinazotokea basi wanapewa sawa,’’anaeleza.

MWISHO

 

 

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

…….SUZA WATOA USHAURI WA ADHABU YA KUNYONGWA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WANAFUNZI wanaosomea uwalimu Chuo cha taifa cha Zanzibar ‘SUZA’ kampasi ya Benjamin Wiliam Mkapa Wete Pemba, wamependekeza adhabu ya kunyongwa hadi kufa, kwa mtu atakaetiwa hatiani, kwa kosa la dawa za kulevya. Walisema, haiingii akili kuona, mahkama imeshamtia hatiani mtu kwa kukutwa na dawa za kulevya, ambazo huathiri nguvu kazi ya taifa na kisha, kupewa hukumu ya kifungo pekee. Wakizungumza leo Juni 26, 2024 kwenye kongamano la vyuo vikuu, juu ya masuala ya msaada wa kisheria, kuelekea wiki ya msaada wa kisheria Zanzibar, lililofanyika Chuoni hapo, walisema wakati umefika sasa kutolewa kwa hukumu hiyo. Walipendekeza kuwa, ni vyema kwa mtu anayetiwa hatiani asibakie chuo cha Mafunzo pekee kuitia tena hasara serikali kwa chakula na wakati mwingine matibabu, wakati tayari ameshasababisha madhara, kwa vijana. Mshiriki Juma Nafasi Juma, alifafanua kuwa kama mtu ameamua kuliumiza taifa kwa kuingiza, kusafirisha, kusambaaza dawa za kulevya, hivyo ni vy

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan