Skip to main content

USHIRIKA WA WANAWAKE SHUNGI CHAKE CHAKE WAANZA KUUWAGA UMASKINI WA KIPATO

 


 NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

WANACHAMA wa ushirika wa ‘twaomba kheir’ wa wanawake wa kijiji cha Chanjamjawiri shehia ya Shungi wilaya ya Chake chake Pemba, wamekopeshana mikopo minane, yenye thamani ya shilingi 800,000 katika kipindi cha mwaka jana pekee.

Wapo wanachama sita, waliokopa shilingi 100,000 kila mmoja na wawili kukopa shilingi 50,000, kwa ajili ya kutimiza malengo yao mbali mbali, ikiwemo kukamilishia ujenzi wa nyumba zao.

Ushirika huo wenye wanachama 15, unasema kima hicho cha fedha walichokopeshana sio kidogo kwa wao, kutokana na hali zao za umaskini wa kipato ulivyokuwa hapo awali.

Akizungumza na mwandishi wa habari hizi, Mashika wa ushirika huo Sharifa Mohamed Khamis, alisema fedha hizo zilitokana na michango yao ya awali ya kila mwanachama, kujiwekea hisa ya shilingi 8,000 kwa mwezi, sawa na shilingi 2,000 kila mwisho wa wiki.





Alisema kuwa, utaratibu huo ulianza tokea mwezi Septemba mwaka 2022, ambapo kwa mwezi, wanauwezo wa kukusanya shilingi 120,000 wastani wa shilingi milioni 1,440,000 kwa mwaka.

‘’Fedha hizi ndio ambazo wapo waliokopa hadi shilingi 100,000 na wingine kufanikisha matibabu, kuendeleza ujenzi wa nyumba zao, harusi pamoja na vifaa vya masomo kwa watoto,’’alisema.

Mshika fedha huyo alieleza kuwa, kwa hali zao za maisha zilivyo, wamepiga hatua kubwa ya maendeleo, kutoka utegemezi wa kipato usio na uhakika hadi sasa kujiamini kukopa kima chochote kwa ajili ya kutatua changamoto.

Katibu wa ushirika huo Mkali Juma Ali alisema, baada ya kuona mafanikio, kisha walianza na mtaji wa kununua sabuni ya unga na kukopeshana, na kwa mara ya kwanza, walitumia shilingi 38,000 na kujiingizia faida ya shilingi 8,800.

‘’Tulifanya hivyo kwa mara saba na tukajikuta tumenunua sabuni ya unga ya shilingi 266,000 na kujipatia faida ya shilingi 61,600 kwa mtindo wa kuuzia paketi ya kilo moja kwa shilingi 1,700,’’alifafanua.

Mwenyekiti wa ushirika huo Bimkubwa Othman Khamis, alisema baada ya kuona wanapata faida, waliamua kujinunulia sukari kilo 200 kwa mara nne tofauti, kwa gharama ya shilingi 300,000 kwa wakati huo.

‘’Baada ya kuuziana kwa vipindi vinne tofauti, kwa bei ya kilo moja shilingi 2,000 tulijipatia shilingi 400,000 na kujiingizia faida ya shilingi 100,000 na hapo tulikuza mtaji wetu,’’alifafanua.

Alifafanua kuwa, kwa sasa baada ya kuimarika kwa hisa, wamekijikuta kuwa na miradi miwili ya uuzaji wa sabuni na usukari huku uwekaji wa hisa na ukopaji ukiendelea.

Mwanachama wa ushirika huo Asma Said Abdalla, alikiri kuwa, kwa sasa maisha yake ya kipato yako tofauti kabla na baada ya kuingia kwenye ushirika huo.

‘’Hivi karibuni niliwahi kukopa shilingi 150,000 na kumalizia ujenzi wa vyumba vitatu, jambo ambalo kama sio ushirika huu, nisingekuwa na uwezo huo,’’alieleza.

Nae mwanachama wa ushirika Zulekha Nassor Hilali, alisema alikopa shilingi 150,000 kwa ajili ya matibabu, jambo ambalo lilimsaidia kutatua changamoto hiyo.

‘’Kwa hakika mafanikio yetu makubwa ni kujiamini sasa na hatuna hofu kwa jambo la shilingi 100,000 hadi shilingi 500,000 kwangu sio kikwazo nikitokezewa na shida,’’alifafanua.

Moja ya changamoto wanazokumbana nazo kwa sasa, ni pamoja na masharti magumu ya upatikanaji mikopo jambo ambalo, linawarejesha nyuma kimaendeleo.



Sheha wa shehia ya Shungi Hamad Ramadhan Soud, alisema ushirika huo umekuwa mfano wa kuigwa ndani ya shehia yake, kutokana na kufanya vizuri, kuanzia uwekaji hisa hadi biashara.

‘’Naendelea kufautilia namna ambayo wanaweza kupata mikopo yenye masharti nafuu, ili kuona wanaendeleza biadhara zao na kuongeza mtaji wao hapo badae.

Ushirika huo wa ‘twaomba kheir’ wa kijiji cha Chanjamjawiri shehia ya Shungi, unao wanachama 15 wote wanawake, ulianza mwaka 2022, unaendesha uwekaji hisa, uuzaji wa sabuni na sukari na wanampango wa kununua nguo hapo baade.

                 Mwisho

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch