Skip to main content

WARIOBA: 'VYOMBO VYA HABARI VINAJUKUMU KUELIMISHA UMMA MASUALA YA UCHAGUZI, DEMOKRASIA'

 

 





NA MWANDISHI MAALUM, DODOMA@@@@

VYOMBO vya habari vina dhima na jukumu la kusaidia katika kuimarisha demokrasia hususan katika kuelimisha umma masuala ya uchaguzi ili waweze kushiriki kwa ukamilifu katika uchaguzi na kuimarisha demokrasia ya ushiriki wa wananchi kwa ukamilifu.

Akizungumza katika kongamano la wadau wa habari na uchaguzi Tanzania lillilofanyika leo April 30, 2024,  katika ukumbi wa hoteli ya Dodoma Waziri mkuu mstaafu Jaji Joseph Warioba alisema kuwa nguvu ya vyombo vya habari havina budi kutumika katika mchakato wa uchaguzi tokea kujiandikisha hadi kupiga kura ili kuimarisha shughuli hizo za uchaguzi.

Jaji warioba alisema kuwa bado vyombo vya habari havikufanya kazi zake kwa ukamilifu  katika chaguzi zilizopita hivyo kuna haja ya kubadilika katika vyombo vyetu vya habari ili viweze kufanya kazi zake kwa ufanisi.

“Vyombo vya habari vinatoa habari sio elimu na vinajikita zaidi katika matokeo na havifanyi utafiti”, alifafanua.

Jaji Warioba alisema kuwa enzi zile vyombo vya habari hususan katika maoni ya mhariri vilijikita katika utafiti wa kina na kufanya uchambuzi ambao ulisaidia kuizindua serikali na kuweka sera ambazo zinasaidia kataika kujenga na kuimarisha haki na demokrasia katika masuala mbali mbali.

Alisisitiza haja ya vyama vya siasa kuwa na mawanda mapana katika kuimarisha demokrasia hapa nchini hususan katika hatua za awali za uteuzi wa wagombea.

“Vyama vya siasa viimarishe demokrasia katika uteuzi wa wagombea tuwapelekee wananchi wagombea wanaokubalika kwa wananchi”, Aliongeza

Alitoa wito maalum kwa vyombo vya habari kusaidia kupunguza changamoto za uchaguzi katika hatua zote tokea kujiandikisha, kupiga kura pamoja na kuchagua wagombea ambao wamekubalika kwa wananchi.

Vurugu katika uchaguzi zinatokea kutokana na kwamba wananchi hawakuridhika na mchakato wa uchaguzi  na sauti na kero zao hawana pahala za kuzitoa hivyo ni muhimu kulitazama kwa kina suala hili la uchaguzi katika hatua zote ili usawa, haki na uwajibikaji uweze kupatikana katika hatua zote.

Katibu Mtendaji wa Baraza la habari Tanzania Ernest Sungura alisema kuwa Baraza la habari Tanzania limejikita katika kukuza maadili na weledi kwa waandishi wa habari ili waweze kutumia kalamu zao katika kujenga misingi ya haki , uwazi na uwajibikaji katika hatua zote za uchaguzi.



Alisema kuwa nguvu ya vyombo vya habari havina budi kutumika kujenga jamii iliyo bora na imara ili lengo la vyombo hivyo katika kuelimisha umma liweze kutekelezwa.

“Kuongeza elimu kwa wapiga kura itakayowasaidia kufanya maamuzi makini na sahihi katika sanduku la kupiga kura”, alifafanua.

Alisisitiza kuwa kwa kipindi vyombo vya habari Tanzania havikuwa na mshikamano na maandalizi ya pamoja na kuimarisha habari za uchaguzi katika hatua zote ili kuimarisha elimu kwa wapiga kura lakini pia wananchi waweze kupata taarifa ambazo zitawasaidia katika kufanya uamuzi wakati wa kupiga kura.

“Vyombo vya Habari vya Tanzania huwa havina maandalizi ya Pamoja ya namna ya kuandika na kutangaza Habari za uchaguzi katika kila hatua ya mchakato wa uchaguzi kuanzia uboreshaji wa daftari la wapiga kura, kujiandikisha kwa wapiga kura, uteuzi wa wagombea, elimu kwa mpiga kura, kampeni hadi siku ya kupiga kura”.Alifafanua

Hivyo alisema kuwa Baraza la habari linakusudia Kuviandaa vyombo vya Habari mapema kwa kuandaa Mpango Kazi wa Kitaifa unaolenga kuvisaidia vyombo vya Habari kufanya kazi ya kihabari ya kutoa taarifa sahihi kwa wakati sahihi kufichua uovu na kuwajibisha na kuibua masuala ili yajadiliwe.

Mwakilishi wa ubalozi wa Marekani Kalisha Holmes, alisema kuwa vyombo vya habari ni muhimili wa nne na hivyo vina wajibu wa kuelimisha umma katika masuala ya uchaguzi ili waweze kufanya maamuzi sahihi.

Katika kipindi hiki ni wakati muafaka wananchi kupata habari zilizo sahihi ili waweze kufuatilia kwa karibu hatua zote za kuimarisha demokrasia pamoja na kutumia vyombo vya habari kama njia muhimu ya kuimarisha demokrasia hususan katika kuelekea uchaguzi.

“Umuhimu wa uhuru wa vyombo vya habari unahitajika. Vyombo huru na vinavyojitegemea ni nguzo muhimu katika kukuza na kuimarisha demokrasia”, aliongeza.

Wakichangia katika kongamano hilo Usia Nkhoma Mtaalam wa mawasiliano kutoka UNICEF alisema kuwa Vyombo vya habari viwe na agenda ili viakisi maoni na matakwa ya wananchi ili tuwe na vyombo vya habari makini, tunalo jukumu kubwa la namna gani tunaweza kujenga vyombo vya habari imara ambao  tulazimishe wanasiasa waweke masuala ambayo yanayokidhi mahitaji ya vizazi vyetu.

Edda Sanga mwandishi mkongwe alisema wanawake hawana budi kupewa fursa ya kuchagua na kuchaguliwa kwa mujibu wa matakwa yao na kamwe wasitumike kama ngazi katika uchaguzi.  Sauti za walioko pembezoni pia ziweze kupewa nafasi katika uchaguzi na kero zao ziibuliwe na kujadiliwa na kupatiwa ufumbuzi.

Pili Mtambilike mtaalamu wa sekta ya habari amesema vyombo vya habari vina dhima kubwa ya kuondoa sumu iliyojengeka katika uchaguzi na hivyo  kuongeza elimu ya wapiga kura katika vyombo vya habari. Vyombo vya habari viwe mstari wa mbele katika kusaidia kueneza suala hilo la elimu kwa mpiga kura.

Aliongeza umuhimu wa makundi yote ya pembezoni kuwemo katika hatua zote za uchaguzi hususan makundi ya walemavu ili kuimarisha ushiriki wa watu wote katika masuala ya uchaguzi. Mchakato wa kuwapata wagombea katika makundi hayo uwe wa uwazi na uzingatie haki na usawa kwa wote.




Kongamano hilo la siku moja ambalo limefanyika leo katika ukumbi wa Dodoma Hotel likiwa na kauli mbiu ya uandishi wa habari za uchaguzi kwa weledi na kujenga usawa, haki na uwajibikaji limeandaliwa na Baraza la habari Tanzania na limewashirikisha wadau wa habari, wanasiasa, waandishi wa habari pamoja na asasi za kiraia.

Hii ni mara ya kwanza kwa kongamano la aina hiyo kufanyika hapa nchini likiwa na lengo la Kujadiliana na kuweka mikakati ya pamoja kuongeza UWAZI, HAKI na UWAJIBIKAJI tunapoelekea katika uchaguzi wa serikali za mitaa mwaka 2024 na uchaguzi mkuu mwaka 2025. Kongamano hilo limefadhiliwa na Ubalozi wa Marekani na IFES (The international and Foundation for Electoral system)

mwisho

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch