Skip to main content

'CITIZEN BRIGED' PEMBA WAONESHWA WALIPO WANAWAKE WA KUANDALIWA KIUONGOZI

 


NA ZUHURA JUMA, PEMBA@@@@

MWENYEKITI wa Bodi ya Jumuiya ya Utetezi wa Mazingira na Jinsia Pemba ‘PEGAO’ Alhajji-Amran Massoud Amran, amewashauri wahamasishaji jamii kudai haki zao za uongozi, demokrasia na siasa ‘Citizen bragged’ kisiwani Pemba, kuelekeza nguvu zao ngazi ya vyuo, ili kuwaibua wanawake wenye nia ya kugombea nafasi za uongozi.

Alisema, wanafunzi wanawake ambao wanajitayarisha kuja kuitumikia jamii, wako katika skuli za sekondari na vyuo vikuu, hivyo ni vyema kwa wahamasishaji hao, sasa kuhamia katika eneo hilo kufanya uhamasishaji.

Mwenyekiti huyo wa bodi, aliyasema hayo jana, alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi juu nafasi ya wahamasishaji jamii kutoka TAMWA, namna ya kuwaandaa wanawake kuwa viongozi katika nafasi mbali mbali.

Alisema, wanawake walioko ngazi ya elimu ya sekondari na vyuo vikuu, ndio tegemeo kubwa kwa jamii, hivyo ikiwa watawezeshwa mapema, kuingia katika nafasi za uongozi, itakuwa rahisi kwao, baada ya kumaliza masomo.

‘’Kwanza nipongeze kazi yenu kubwa ya kuzipitia shehia mbali mbali hata zile za visiwani, kwa lengo la kuihamasishaji jamii, kudai haki zao za uongozi, lakini msisahau kupitia na vyuoni,’’alipendekeza.



Katika hatua nyingine, Mwenyekiti huyo wa Bodi ya ‘PEGAO’ Alahajji-Amran Massoud Amran, alisema bado elimu zaidi inahitajika kwa jamii, ili imuamini mwanamke kwenye safu ya uongozi.

Hata hivyo alisema, juhudi zinazofanywa kwa pamoja kati ya PEGAO, ZAFELA na TAMWA zinafaa kuungwa mkono, kwani inakuja kuchapuza ukuaji wa demokrasia na uwazi nchini.

Mapema Mkurugenzi wa ‘PEGAO’ Hafidh Abdi Said, aliwasisitiza wahamasishaji hao, wanapoibua changamoto kwa jamii, wahakikishe wanaifuatilia hadi mwisho.

‘’Kwa mfano, wapo wanawake hata vitambulisho vya mzanzibari mmegundua hawana, au hawana huduma za kijamii kama maji safi na salama, sasa hapa lazima mzitafutilie ufumbuzi wake, ili wawaamini,’’alishauri.



Hata hivyo Mkurugenzi huyo, aliwakumbusha wahamasishaji hao, kuwamakini wanapoandika ripoti zao, ili zianishe changamoto, suluhisho na mkakati wa baadae.

Kwa upande wake Mratibu wa mradi wa kuihamasisha jamii kudai haki zao za kisiasa, uongozi na demokrasia ‘SWIL’ kutoka ‘PEGAO’ Dina Juma, alisema ni vyema kwa taasisi na mashirika, kuendelea kushirikiana na asasi za kiraia.

‘’Sisi asasi na zile taasisi za serikali, sote tunatengeneza jamii moja, sasa tunawapowafikia, kuwasilisha changamoto zao, waone kama tumewasaidia kazi,’’alieleza.





Mhamasishaji jamii kutoka Wete Salim Hamad Sharif, aliuomba uongozi wa ‘PEGAO’ kupanga timu maalum, kwa ajili ya kwenda kwa wananchi wa kisiwa cha Fundo, kutoa elimu kwa upana.

‘’Wananchi wa kisiwa cha Fundo baadhi yao hawajaelewa kwa upana, umuhimu wa elimu kwa watoto wao, ndio maana mtoto anaweza kutolewa darasani aende habarini, bila mzazi kujali jambo hilo,’’alieleza.

Nae Mohamed Maalim, alisema kama inakubalika popote mtu anapofanyia kazi kufikisha elimu, sasa atahakikisha kila eneo anafika, ili kuelezea haki jamii katika uongozi, siasa na demokrasia.

Wakiwasilisha ripoti zao hivi karibuni, viongozi wa wahamasishaji jamii kutoka wilaya nne za Pemba, walisema wamekuwa wakiibua changamoto zinazoikabili jamii, ingawa upatikanaji wa suluhisho ndio kikwazo.

Mradi wa kuihamasisha jamii kudai haki zao za uongozi, demokrasia na siasa ‘SWIL’ unatekelezwa na Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania, ‘TAMWA’ –Zanzibar, Jumuiya ya Wanasheria Wanawake Zanzibar ‘ZAFELA’ na Jumuiya ya Utetezi wa Mazingira na Jinsia Pemba ‘PEGAO’ kwa ufadhili wa Ubalozi wa Norway.

Mwisho wa utekelezaji wa mradi huo, huo wa ‘SWIL’ unatarajiwa wanawake wasiopungua 6,000 iwe wamesha wezeshwa kudai haki zao.

 Mradi huo uliozinduliwa Novemba, 2020, na ukitarajiwa kutia nanga mwaka 2024, watu 100 wakiwemo wanawake na wanaume, iwe tayari wameshajengewa uwezo, ili nao sasa kuwafikia wanawake 400, ambao nao wenyewe wanatarajiwa kuwafikia wanawake hao 6,000.

 Idadi hiyo wanawake 6,000 watakaofikiwa, ni sawa na PEGAO, TAMWA na ZAFELA kuwafikia wanawake 1,200 kwa kila mkoa mmoja, kati ya mitano ya Unguja na Pemba.

 Ambapo hapo ni sawa na wanawake 546 kutoka kila wilaya moja, kati ya wilaya 11, ambapo Pemba zipo nne na Unguja saba.

 Zanzibar yenye majimbo 50 ya uchaguzi, mradi huu wa ‘SWIL’ utawafikia wastani wa wanawake 120, kutoka kila jimbo moja la uchaguzi, sawa na kufikiwa wanawake 55 kwa kila wadi moja, kati wadi 110 za Unguja na Pemba.

                              Mwisho   

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch