Skip to main content

Waandishi Chipkizi Zanzibar wang’ara kwenye Mradi wa kuleta mabadiliko ya wanawake na Uongozi

 


Zanzibar: Nihifadhi Issa.

Chama Cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania -Zanzibar – TAMWA-Z kimekutana na waandishi wa Habari chipukizi,wahariri,wamiliki wa vyombo vya Habari na wadau wa Habari kwa kuwatunuku  na kuwatunza waandishi wa Habari 23 waliokuwa kwenye mradi wa Waandishi wahabari vijana.

Mahafahali hayo yamefanyika katika Ukumbi wa Bima uliopo Maisara Mkoa Mjini Magharib Unguja.

Khairat Haji ni  Kaimu Afisa Programmu TAMWA -Zanzibar amesema katika hatua za kumarisha uongozi kwa wanawake   mradi  huu ambao hii ni awamu ya pili ambapo kwa awamu ya kwanza uliwafunza na kuwasimamia waandishi vijana 18 kwa 2022  akieleza kuwa mwaka 2023 waandishi vijana 24 walipata fursa katika mradi huu wa Wamawake na Uongozi”Kupitia mradi huu  ulikuwa unahitaji kazi 348 na hadi kufikia leo kazi hizo ni 347,huku magazeti 47 ,Makala za radio 117 huku Makala za mitandamo 187 ambazo zinakamilisha kazi 347” Amesema Khairat

Shifaa Said ni Jaji Kiongozi wa Tuzo za Waandishi wa Habari Chipukizi kwenye kuhariri kazi za waandishi hao 24 zilizofika katika sehemu Majaji watatu,Ali Sultan , Husna Mohamed Khamis kwa muda wa siku nne na Makala zilizofika 175 ndio zilizowasilishwa magez 15,radio 85 na mitandao 75 =175

Amesema Vigezo muhimu walivyoangalia  ni weledi na umahiri katika sauti Pamoja zizosikika na umahiri wa lugha kwenye kazi hizi pamoja na upekee wa mada na matumizi ya radio.

“pia tumeangalia mafanikio na ukuwaji wa wanufaika wa waandishi na kufanya Makala na vipindi vyenye  mabadiliko kwenye jamii  ubunifu na weledi wa kuangali na sio Habari za matokeo ila ni Habari zinazoangalia masuala ya kuibua na kujumuisha makundi ya watu wenye mahitaji maalum”alisema Shifaa

Mkurugenzi chama cha waandishi wa habari wanawake    TAMWA Zanzibar Dkt Mzuri Issa amesema kuwa Makala na kazi hizo zimeleta mabadiliko na kazi hizo zimeleta   kwa kuwashawishi wanawake kuingia kwenye siasa na kupata nguvu ya kusaidia kuvunja dhana potofu kwenye wanawake kuwa kwenye uongozi.



“waandishi hawa wamefanya kazi kubwa ambazo zimepekelea mimi kupigiwa simu na wanawake wanataka nmwakani waingie kwenye mchakato wa kugombania nafasi niwape njia za kufanya nijambo la kufurahisha na kupendeza”alisema Mzuri

 

Mjumbe wa Bodi ya Tamwa Zanzibar   Bi  Hawra Shamte amesema kuwa uwepo kwa mahafali hayo   kwa waandishi hao 23 ni kukubali kujifunza na kuandika masuala ya  wanawake na hii ni Dhahiri kuona kwamba majukumu  kwenye kuandika masuala ya wanawake na uongozi yametamalaki 

“Ninachotaka kuwaambia waandishi hawa  tuendelea kaundika na kuihabarisha umma juu ya uwepo kwa Habari hizi katika kuleta mabadiliko katika jamii hii ambayo inategemea kuwa na viongozi wanawake na wanaume”alisemalizia Hawra

  Berema Suleiman Nassor  mwandishi wa Zenji Fm pia ni mnufaika wa Mradi huu. Amesema   kwenye suala hili ni takwimu na upatikanaji wa kuandika na kuwasaidia na kuwafikia jamii ilimuia vigumu

“ mwanzo nilikuwa naadika Habari   za kawaida na sasa nimekuwa na naandika Habari zenye kuleta mabadiliko  usawa wa kijinsia kwanza sikuweza ila kwa sasa   nimekuwa mzoefu hii ni kutokana na juhudi za TAMWA” alisema Berema

KHadija Rashid Nassor  mwandishi wa Radio jamii Mkoani Pemba ambae pia ni  mnufaika kwa mradi huo kwa miaka miwili  sasa amesema wamekuwa kwenye uandishi wa kuunganisha na kuwasaidia wanawake na waandishi wengine

“nimekuwa mzoefu sasa nawafundisha wenzangu namna bora ya kuandaa Makala zenye ubora kwa kuunganisha mikataba na sera mbalimbali”alisema Khadija

Nae mwandishi wa radio jamii Micheweni  Esau Simon   amesema mradi umemsaidia kufanya  kazi za kuleta mabadiliko na sasa kumukuwepo kwa usawa wa mazungumza hususan kwa upande wa watu wenye ulemavu .

 Mwandishi wa DW na Mhariri Salma  Said na amesema suala la kuona vijana wanakuwepo kwenye mradi hii ni kuonesha masuala ya uandishi wa Habari za viwango na wenye kuleta mabadiliko.

“Ikiwa haya yataendelea kuandikwa basi kutakuwepo kwa mabadiliko kwa jamii kwenye uleta uwajibikaji ,kubadilishwa kwa sheria na haki kutendeka”alisema Salma

 

Sambamba na hayo  Mwandishi wa Gazeti la Daily News  Issa   Yussuf amewasisita waandishi hao kuzingatia matumizi ya lugha kwani ni muhimu.

“kwenye masuala ya lugha hii ni jambo ambalo litawafikisha mbali na kuwasaidia zaidi kwenye uandishi kujifunza na kusoma masuala ya mikataba na sheria mbali mbali” alisema Issa

 

Katika mahafali hayo jumla ya washindi watatu wamepata zawadi ya cheti na kompyuta mpakato akiwemo Amina Masoud Jabir kutoka Radio Jamii Mkoani, Hassan Mselem Pemba Online Media na Asya Mwalim Haji kutoka Gazeti la Zanzibar Leo.

Mradi wa huo wa kuwawezesha waandishi wa habari vijana   YMF kuandika habari za wanawake na uongozi uliowashirikisha waandishi vijana 24   unguja na pemba umetekelezwa na TAMWA ZANZIBAR kwa kushirikiana na Shirika la National Endowment for Democracy (NED)

Mwisho.

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch