Skip to main content

MATAYARISHO WIKI YA MSAADA WA KISHERIA PEMBA YAANZA KWA KISHINDO

 



NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

LEO Mei 7, mwaka 2024, Idara ya Katiba na Msaada wa Kisheria Zanzibar ofisi ya Pemba, imekutana na wadau wake mbali mbali wakiwemo watoa msaada wa kisheria na wasaidizi wa sheria, ili kupanga mikakati ya kuelekea, wiki ya msaada wa kisheria hapa Zanzibar.

Kwenye kikao hicho kilichofanyika Gombani Chake chake, na kuongozwa na Afisa Mdhamini, Ofisi ya Rais, Katiba, Sheria, Utumishi na Utawala Bora Pemba, Halima Khamis Ali, kwanza kilipokea ripoti ya wiki ya msaada ya mwaka 2023, iliyotolewa na Mkuu wa Divisheni ya Katiba na Msaada wa Kisheria Pemba, Bakar Omar Ali.

Ambae kwenye ripoti hiyo, alielezea mafanikio yaliopatikana ikiwa ni pamoja na kuwafikia wananchi waliokuwa wakihitaji msaada wa kisheria katika makaazi yao.

Alisema jingine ni waendesha boda boda kutoa malalamiko yao, juu ya madai ya kunyanyaswa na askari wa usalama barabarani pamoja na faini kubwa wanazopigwa kwa makosa madogo.

Mkuu huyo wa Divisheni, alieleza kuwa jingine ni kuwakutanisha watoa msaada wa kisheria na wasaidizi wa sheria kuelezea changamoto wanazokumbana nazo wakati wanapokuwa katika shughuli mbali mbali.




‘Lakini pia katika wiki ya mwaka jana ya utoaji wa msaada wa kisheria, wapo wasaidizi wa sheria mbali mbali, pamoja na waandishi wa habari walionekana kufanyakazi vizuri na kupata tunzo,’’alifafanua.

Akizungumzia kuhusu wiki ya msaada ya mwaka huu, alisema walipanga kuvitembelea vyuo vya mafunzo pamoja na kukutana na wanananchi waliomo kwenye mpango wa kaya maskini.

Alieleza kuwa, shughuli hiyo haitofanywa tu na Idara ya Katiba na Msaada wa kisheria, bali kila jumuia ya wasaidizi wa sheria na taasisi nyingine, zinazojishughulisha na utoaji wa elimu ya sheria zitatakiwa kufanya shughuli yoyote.




Akifungua mkurtano huo, Afisa Mdhamini, Ofisi ya Rais, Katiba, Sheria, Utumishi na Utawala Bora Pemba, Halima Khamis Ali, alisema ni vyema kila taasisi, ikajipangia itafanya nini katika wiki ya msaada wa kisheria mara tu, itakapoanza mwezi ujao.

Alieleza kuwa, Idara ya Katiba na Msaada wa Kisheria, itaanza kupokea mpango kazi wa kila taasisi, iwe ni mahakama, ofisi ya mwanasheria mkuu na hata jumuiya za wasaidizi wa sheria, ili kuona wanawafikia wananchi.

Alieleza kuwa, bado kuna changamoto kadhaa zilizomo ndani ya jamii, ambazo zinahitajika kupatikana ufumbuzi wa kisheria, na jamii inawategemea wanasheria na wasaidizi hao wa sheria.

‘’Lakini sisi wizara, tunaridhishwa mno na kazi mnazozifanya, lakini msibweteke muendelee kukaza buti, kwani jamii inaendelea kukumbwa na majanga mbali mbali ya kisheria,’’alieleza.

Kwa upande wake mwakilishi wa Shirika la Msaada wa kisheria na Haki za Binaadamu ‘ZALHO’ Said Rashid Hassan, alisema yapo makundi kama ya wafanyakazi serikali, yanahitajika kufikiwa ili kuelezea changamoto zao.



Nae Mwanasheria kutoka baraza la mji wa Wete Hafidhi Sadra Hassan, aliiomba Idara hiyo kwa mwaka wa fedha ujao wa fedha, kupanga bajeti maalum ya shughuli hiyo, ili kuwatia moyo watendaji.

Hata hivyo Mkurugenzi wa Jumuiya ya Wasaidizi wa sheria wilaya ya Chake chake ‘CHAPO’ Nassor Bilali Ali, alipendekeza kuwa, kinachofanyika kisiwa kimoja na chingine kufanyike, ili kuweka usawa.

Hii itakuwa ni mara ya tano kufanyka kwa wiki ya msaada wa kisheria Zanzibar, kuanzia mwaka 2020, ambapo kwa mwaka huu, inatarajiwa kuzinduliwa Juni 24, na kuadhimishwa Juni 29 kisiwani Unguja.

                             Mwisho    

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kuta...