Skip to main content

KWA SHERIA HII UHURU WA HABARI ZANZIBAR NI NDOTO

 



NA NIHIFADHI ISSA, ZANZIBAR.@@@@

  WAANDISHI wa habari wanajukumu la kuendelea kufanya uchechemuzi wa mabadiliko ya sheria zenye mapungufu na ambazo sio rafiki kwa tasnia ya habari ili kutoa fursa ya upatikanaji wa sheria zilizo bora.

Yamebainishwa hayo na Mkurugenzi wa Chama Cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania TAMWA Zanzibar     Dkt. Mzuri Issa  nakusema kuwa   Sheria nambari 5 ya Wakala wa Habari, Magazeti na Vitabu ya mwaka 1988, ambayo imefanyiwa marekebisho sheria namba 8 mwaka 1997 sheria hii licha yakuwa ni kongwe imekuwa na mapungufu mengi yanayokwamisha haki na uhuru wa vyombo vya habari Zanzibar.

Akizungumza katika kikao cha kujadili   mapungufu ya sheria zinazokwamisha uhuru wa habari huko katika ukumbi wa TAMWA Tunguu amesema Demokrasia sahihi hutegemea uhuru wa vyombo vya habari unavyoweza kusimamia maslahi ya jamii,   ikiwemo  uhuru wa kutoa maoni na kujieleza bila ya kuingiliwa pamoja  kusambaza taarifa na mawazo ya aina mbalimbali kwa kufuata kanuni  zilizowekwa ni haki inayotambuliwa na sheria za kitaifa na  kimataifa.

“ikiwa Zanzibar imo ndani ya Tanzania na imeridhia mikataba mbalimbali ambayo inalinda tasnia ya habari ipo haja kufanyika marekebisho kwa sheria ambazo haziendi sambamba na uhuru  wa habari ikiwemo sheria hii” alisema Dkt Mzuri.



Kwa mujibu wa Sheria nambari 5 ya wakala wa habari, magazeti na vitabu ya mwaka 1988, yenye  marekebisho ya sheria namba 8 mwaka 1997 katika sheria hii vipo vifungu ambavyo havijatowa uhuru kwa waandishi pia kwa vyombo vya habari kikwemo kifungu cha 14 (1) kilichompa mamlaka mrajisi kumtaka mchapishaji gazeti kupeleka kopi mbili kila siku kwa gharama zake kwa madai ya kuweka kumbukumbu.

Afisa   mradi wa Uhuru wa Habari kutoka  TAMWA Zanzibar    Zaina Abdalla Mzee amesema uwepo wa sheria hiyo unakinza dhana ya demokrasia na utawala  “kwanza hii sheria ni kongwe imefikia wakati  irekebishwe ili kuchapuza uhuru wa habari ambao tunautaka,”   

Ameendelea kuwa “Sheria hizihaziwagusi waandishi tu bali hata wanachi wanaotumia vyombo vya habari kutoa malalamiko au shida zao zinapowakabili  huingiwa na woga  na hivyo kukosa uhuru wa kujieleza” ameeleza Zaina.





Waandishi wa habari ndio wahusika wakuu katika hili, Khatib Suleiman    ni mwandishi wa habari     wa Gazeti la Habari Leo  anasema vifungu hivyo vya sheria vinarudisha nyuma utendaji wa kazi wa mwandishi wa habari “kwa mfano chombo cha habari hakipati mapato kinapata wapi fedha za kupeleka nakala kila siku kupeleka kwa mrajis mimi mawazo yangu ofisi ya mrajis iwe na mtu maalum wa kufuatilia izo habari kama wanataka kuendelea na hiyo sheria” amesema Khatib.

Kwa upande wake mwandishi mwanandamizi Hawra Shamte amesema licha ya kuwa kuna sheria zinazosimamaia sekta ya habari lakini kiuhalisia zinaonekana hazifanyi kazi ipasavyo ya kulinda usalama wa waandishi wa habari hivyo zinahitaji kufanyiwa marekebisho.

“Tanzania ni moja kati ya nchi iliyoridhia mikataba mbalimbali ya kimataifa na kikanda ambayo inalinda tasnia ya habari, waandishi wa habari, watetezi wa haki za binadamu hivyo wajibu wa Serikali  kuendeleza uhuru wa habari kama ya;ivyo makubaliano hayo,” Hawra.

Salim Said Salim ni mwandishi mkongwe Zanzibar amesema waandishi wanakutana na vikwazo wakati wa kutekeleza majukumu yao”Vyombo vya habari hufikia wakati mwengine kufungiwa na kushindwa kuendelea na kazi zao za utangazaji kwa kipinmdi kadhaa  au kupigishwa faini hii inachukiza,”alisema Salim .    



Wananchi wanayo haki ya kupata habari  kupitia vyombo mbalimbali Mfaume Muhammed  anasema ikiwa vyombo vya habari vitaekewa vikwazo au  vizuizi ambavyo si vya lazima itawia vigumu kupata habari   “lazima vikwazo vingine vitatuliwe ambavyo vinaonekana havina ulazima sana izo nakala mbili ni nyingi wakishindwa kuchapisha na sisi wasomaji wa magezeti tutakosa kusoma  habari” alifafanua Mfaume.

Akitoa maoni Mwanasheria kutoka Tume ya kurekebisha Sheria Zanzibar Sabra Mahmoud Iddi amesema wanategemea mchakato Sheria ya habari utafanyiwa marekebisho ili kupata sheria bora zinazozingatia maslahi ya waandishi na uhuru wa vyombo vya habari.

“Hili jambo ni la muda mrefu na linapitia hatua kwa hatua lazima waandishi muwe na subra kwa lengo la kupata sheria bora zinazokwenda na wakati”amesema Sabra.

 mwisho

 

 

 

 

 

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch