Skip to main content

MaDC, MASHEHA, MADIWANI MKOANI WAPEWA DOZI KUHUSU MIPANGO MIJI

 


NA ASHA ABDALLA, PEMBA @@@@

WAKUU wa wilaya, Masheha na Madiwani  wametakiwa kushirikiana kwa pamoja katika kuwaelimisha wananchi kuhusiana na mipango miji, ambayo itaweza kuwasaidia wananchi wote kuwa na makaazi yenye hadhi kisiwani Pemba. 


Hayo yameelezwa na Salma Abdalla Ali kutoka Idara ya mipango miji na vijiji kamisheni ya Ardhi Pemba, kwanyakati tofauti, wakati walipokua wakitoa mafunzo ,huko wilayani  Mkoani Mkowa wa Kusini Pemba. 


Alisema kua Mipango miji imekuja kwa ajili  ya kuwapimia Wananchi maeneo ambayo hajawahi kupimwa hususani yale ambayo hayajafanyiwa ujenzi, ili waweze kupunguza migogoro mbalimbali ambayo inajitokeza ndani ya jamii.


Aidha alisema kuwa Idara ya Mipango miji wanakazi kubwa ya kuelimisha jamii, kupitia vipindi mbalimbali vya redio na tv, kwani wanachi bado wanauwelewa mdogo kuhusu mipango miji.




Hata hivyo alisema kuwa, wanatarajia kupanga eneo kwa kila wilaya, ambalo litaweza kuimarisha mji ambalo litaweza kutumika kwa matumizi mbalimbali ya wananchi  waliomo kwenye wilaya hizo.

"Tutajaribu kupima maeneo na kueka eneo ambalo wananchi wataweza kulifanyia shughuli mbalimbali za kijamii, ikiwemo kilimo, mifugo, masoko kwa lengo la kukuza uchumi wa nchi yetu," alifafanua.



Kwa upande wake Katibu Tawala wilaya ya Mkoani Miza Hassan Faki kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya hiyo, alisema kua nilazima mipango miji wawe karibu na wananchi, ili kuwapa elimu zaidi ili waweze kufahamu hiyo mipango miji nini na malengo yao ni yepi.

Nae Afisa usajili wa Ardhi kamisheni ya Ardhi Pemba Yussuf Hamad Kombo, alifahamisha  kua umilikishwaji  wa ardhi ndio njia pekee, ambayo inaweza kupunguza migogoro mbalimbali wananchi wanakumbana nayo katika jamiii.


"Tunapokuja mipango miji tukakupangia, upimaji, kukumilikisha na kukusajili, inakuwa ni umuhimu mkubwa kwani  eneo lako litakua tayari, lishawekwa kuzuizi na hakuwezi kutokea mgogoro wa aina yoyote hataka nieneo umerithi au kuzawadiwa , "alifafanu.



Kwaupande wake Afisa wa Ardhi kutoka kamisheni ya Ardhi Hamida Juma Hamad aliwaomba Masheha na Madiwani, kujitahidi katika kushirikiana kuwapa elimu  wananchi, ili waweze kulifanikisha kikamilifu zoezi zima  la upimaji wa ardhi.

Nae Mkurugenzi kutoka Baraza la mji la Mkoani Yussuf Kaiza Makame, alisema kuwa kuna umuhimu mkubwa wakuja  mpango miji kwani kwasasa Pemba mzima, itajengeka katika muonekano mzuri kulingana na ilivo kua hapo awali. 



Hatahivyo alisema kuwa Mipango Miji waweze kupima ardhi kwa kuweka alama na kutowa hatimiliki ili kuepusha udanganyifu ambao utasababisha mizozo kwa wananchi.



Nae Sheha wa Shehia ya Kengeja Mohamed Kassim Mohamed aliishukuru mipango miji kwa kuwapatia mafunzo hayo, waliowapa na kuahidi watayafanyia kazi kwa wananchi wao, na kuwaomba na wao mafunzo hayo kuwapitia  wanavijiji kuaelimisha zaidi ili wapate kuelewa kwaharaka. 



Kwa upande wake Diwani wa kuteuliwa  Wilaya ya Mkoani Arafa Mzee Amour, alitowa ushauri kwa Idara ya Mipango Miji wakati wanapotaka kupima Miji  ile wanayotaka kuekeza  wajaribu kupima maeneo yale ambayo hayajajengwa yapo karibu nabarabara ili kuuweza kupata miundombinu iliyo bora .


Mafunzo hayo yaliofanyika wilaya ya Mkoani yalijumuisha katibu tawala wa wilaya ya Mkoani kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya, Masheha wa Shehia 36 za Mkowa Kusini  na madiwani  ,na Mkurugenzi wa baraza la Mji Mkoani. 


MWISHO.

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch