Skip to main content

MWANI: ZAO LINALOWABEBA WANAWAKE KIUCHUMI, BIDHAA ZAKE ZAONGEZA MYORORO WA THAMANI

 


NA MUZNAT KHAMIS, ZANZIBAR@@@@

TOFAUTI na vilimo vyengine tulivyovizoea ambapo mkulima hulazimika kuchimba ardhi kwa kutumia jembe ama zana nyengine, kuweka mbegu, mmea huanza kuota na tofauti na mwani ambao hulimwa kwenye maji ya bahari.

 

Kilimo cha mwani kilianza mwishoni mwa mwaka miaka ya 1980 hapa Zanzibar, ambapo wanaume wakiwa kwenye hatari za uvuvi wanawake walizana kuingia kwenye kilimo hicho.

 

Hata hivyo, wanawake wengi hapo awali waliokuwa wakijishughulisha na kilimo cha mwani ni wale waliokuwa kwenye mazingira magumu wakiwemo wajane, ambao ndio waliokiona kilimo hicho kuwa mkombozi.

 

Umaarufu wa kilimo hicho zaidi unatokana na faida zake kiuchumi na kwa sababu wakulima wengi wa zao hilo hapa Zanzibar ni wanawake, ina maanisha kwamba zao hilo limekuwa moja ya nguzo ya kiuchumi katika maisha ya akina mama Zanzibar.

 

Makala haya yanalenga kuangalia japo kwa ufupi sana namna zao hilo linavyowanufaisha kiuchumi akina mama na namna zao hilo lilivyobadilisha maisha yao.

 

MWANI UNAVYOBADILISHA MAISHA YA WANAWAKE

Mariyam Mussa Haji mkaazi wa Fuoni Melitano, ambaye ni muanzilishi wa kikundi cha ‘Muzne products’ chenye watu watatu, alisema thamani ya zao la mwani imeongezeka ikilinganishwa na miaka iliyopita.

 


“Thamani ya zao la mwani imeongezeka kwa sababu sehemu ya mwani inayozalishwa hapa Zanzibar inasarifiwa na kuzalisha bidhaa mbalimbali”, alisema Mariyam.

 

Alisema tofauti na zamani mwali wote uliozalishwa Zanzibar ulisafirishwa nje, hivi sasa hatua ya mwani kuzalishwa bidhaa hapa nchini kumeongeza mnyororo wa tathamani kwa wajasirimali hasa wanawake.

 

Mariyam alisema tangu kukindi chao kuanza kuuza bidhaa zitokanazo na mwani wamekuwa wakipata faida kubwa ikiwemo kujikwamua kimaisha kutokana uuzaji wa bidhaa hizo.

 

Miongoni mwa bidhaa ambazo makala haya ilibatika kuziona zilizozalishwa na kikundi cha ‘Muzne products’, kilichopo Fuoni Meli tano ni pamoja na sabuni, mafuta, jam na unga wa lishe wa mwani.

 

“Kwa kiasi fulani fedha tunazopata zinatusaidia kimaisha na kuepukana na ukali wa umasikini, wengine wamepata ajira za kudumu kwa kuuza bidhaa”, alisema Mariyam.

 



Alisema kwa mwezi mmoja inategemea sana hali ya soko, hata hivyo katika kipindi hicho ana uhakika wa kuingiza kuanzia shilingi 300,000 kwenda juu.

 

“Kwa kawaida biashara inaenda na msimu kwa wastani tunaweza kuingiza 500,000, ikiwa biashara haiku vyema hatukosi shilingi 300,000”, alisema.

 

Mariyam alisema wanunuzi wa bidhaa za mwani mara nyingi hutoka Tanzania bara pamoja na wazungu wanaotembelea katika maduka yao.

 

Kwa upande wake, Mwanaisha Makame ambaye ni mmoja kati ya wachakataji wa zao la mwani kutoka Paje, alisema kazi hiyo imesaidia kuinuka kiuchumi kwani amefanikiwa kuwasomesha watoto wake wawili katika ngazi mbalimbali.

 

Safia Hashim mkaazi wa Muungoni wilaya ya Kusini Unguja, alisema yeye ni mmoja kati ya wanawake waliofaidika na kilimo cha mwani, ambapo amefikia hatua ya kumiliki nyumba.

 

Safia alisema alipata mafunzo ya miezi mitatu kutoka kwa mtaalamu kutoka Indonesia ambayo yamemuwezesha kuwa na ujuzi wa kusarifu zao la mwani.

 

"Kwa sasa naweza kutumia mwani kutengeneza vitu mbalimbali kama vyakula, juisi, chachandu, pilipili, kachumbali, chipsi, tambi, chauro, visheti, keki, pipi, jam ya matunda, sabuni, shampoo na mafuta ya kupaka na nywele”, alisema Safia.

 



Joyce John Denis, ofisa uvuvi kitengo cha mwani katika Idara ya Maendeleo ya Uvuvi na Mazao ya Baharini, alisema hatua ya wajasirimali kuzalisha bidhaa mbalimbali kumelipa heshima zana zao hilo kwa kiliongezea thamani.

 

Ofisa huyo alibainisha kuwa bidhaa zinazotokana na zao la mwani zinasaidia wanawake wajasirimali kuongeza mapato na kuchochea bei katika soko ikilinganishwa na mwani mbichi.

 

Aidha alisema bidhaa zitokanazo na mwani husaidia kuimarisha afya ya jamii, kwani bidhaa zitokanazo na zao hilo zinapo sarifiwa na kuwa chakula huasaidia mwili wa mwanadamu kupata virutubisho muhimu.

 

MWANI KUTOKA MALIGHAFI HADI KUZALISHWA BIDHAA

 

Kilimo cha mwani kimewapatia ajira za kudumu wanawake wengi katika sehemu za pwani za vijiji vya Zanzibar, ambapo baadhi ya akina mama waliozungumza na gazeti hili wamesema pamoja na kwamba kilimo hicho ni kigumu lakini kimebadilisha maisha yao.

 

Wanawake wengi wamejiajiri katika kilimo hicho, ingawa wengi wao wanasema kuwa licha ya kazi kubwa kipato ni kidogo wanachokipata, hata hivyo zipo faida wanazozipata.

 

Mwani umebadilisha mtazamo sio tu kiuchumi lakini hata kitamaduni visiwani Zanzibar kwani wanawake wengi wa Zanzibar wanategemea maisha kutokana na kipato cha mwani.

 

 

UZALISHAJI NA USAFIRISHAJI MWANI ZANZIBAR

 

Kwa mujibu wa wizara ya Uchumi wa Buluu na Uvuvi, uzalishaji wa zao hilo hapa visiwani umeongezeka kutoka, tani 10,531 kwa mwaka 2021, hadi tani 12,594 kwa mwaka 2022 sawa na ongezeko la asilimia 20.

 

Kwa mujibu wa taarifa za wizara hiyo, usafirishaji wa mwani nje ya nchi umeongezeka kutoka tani 12,124 kwa mwaka 2021 hadi tani 13,972 mwaka 2022, sawa na ongezeko la asilimia 15.

 

Zanzibar ni nchi ya nne 4 duniani kati ya nchi zinazozalisha mwani (Mwekundu) ikiongozwa na nchi ya Indonesia, Ufilipino na Malaysia, ambapo mwaka 2021 Zanzibar imezalisha zaidi ya tani 12,000.

  


SERIKALI YA AWAMU YA NANE INAVYOSAIDIA KILIMO CHA MWANI

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi, alisema Zanzibar ni nchi inayoongoza kwa uzalishaji wa mwani barani Afrika uzalishaji umeongezeka zaidi kwa tani 12,594 kwa mwaka 2021/22.

 

Alisema mafanikio yote yanatokana na utekelezaji wa sera na mikakati ya uchumi wa buluu ambapo serikali imeunda sera mpya ya uchumi wa buluu pamoja na mikakati ya uzalishaji wa mazao ya baharini ukiwemo mwani.

 

Alisema serikali imewekeza fedha nyingi katika kuwasaidia wakulima na wajasiriamali wa sekta ya mwani wapatao 5,000 Unguja na Pemba kwa kuwapatia boti maalumu za kuwawezesha kwenda katika maji ya kina kirefu zaidi kwa ajili ya ulimaji wa mbegu bora za mwani.

 

 

 

TAFITI ZA KITAALAMU KUHUSU MWANI

Kwa mujibu wa utafiti uliofanywa na Suleyum Talib Ali kutoka Chuo Kikuu cha Taifa cha Zanzibar ulioangazia mchango wa kilimo cha mwani katika uchumi wa buluu, ulieleza kuwa zao hilo limekuwa na nafasi ya pekee katika kusaidia maisha ya wakulima.

 

Kwa mujibu wa utafiti huo mkulima wa mwani kwa mwezi ana uhakika wa kupata kati ya shilingi 120,000 hadi 200,000, ambazo humsaidia katika kukabiliana na changamoto mbalimbali za kimaisha katika familia.

 

Mtafiti wa mwani Flower Msuya, yeye alisema kilimo cha mwani kinasaidia kwa kiasi kikubwa maisha ya wakulima na wajasirimali wanaouza bidhaa za zao hilo.

 

Mwani ni wa pili kuingiza fedha za kigeni Zanzibar, kilimo cha zao hilo kina manufaa makubwa sana kwa wanawake wa visiwa hivyo kwa kuwa kimeboresha maisha yao.

 



"Katika utafifi wetu tumebaini kuwa mwani unaoitwa cottonie unaweza kulimwa kwenye maji mengi na ndio mwani bora zaidi, hivyo tunatumia tuber note kulima mwani huo, njia hiyo inatumia neti na bomba kupanda mwani kwenye bahari badala ya vijiti”, alisema.

 

DIRA YA MAENDELEO ZANZIBAR

Kwa kutambua shughuli za wakulima wa mwani, Dira ya mpango wa maendeleo endelevu ya Zanzibar ya mwaka 2020-2050 imeeleza, kupitia matumizi sahihi ya bahari chini ya mikakati ya muelekeo wa uchumi wa buluu ni kupatikana faida ya ajira na kupunguza umasikini kwa watumiaji wa rasilimali hiyo.

 


Aidha dira imeiweka uchumi wa buluu kama sekta muhimu ya kiuchumi ambayo itaufanya uchumi wa Zanzibar kuwa endelevu.

 

Dira hiyo inakwenda sambamba na malengo ya 14 na 6 ya agaenda ya bara la Afrika 2063, ambayo inasisitiza matumizi mazuri na endelevu ya bahari katika kuleta maendeleo.

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch