Skip to main content

WANAOTUMIA BARA BARA MKOANI-CHAKE CHAKE WAIKUMBUSHA SERIKALI UJENZI

 

 NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

WANANCHI wanaotumia barabara ya Mkoan-Chake chake, wameikumbusha serikali kuanza ujenzi wa barabara hiyo kwa kiwango cha lami, ili waitumie kwa utulivu wanapokuwa katika harakati zao za maendeleo.

Walisema, kwa sasa barabara hiyo imekuwa kero kwao, kutokana na uwepo wa mashimo, misingi, na mipasuko mipana ambayo wakati mwingine husababisha ajali ambazo zinaweza kuepukika.

Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi, baada ya kutokezea ajali hivi karibuni eneo la Ngezi, walisema, mashimo ambayo huongezeka kila mvua zinaponyesha, ndio chanzo cha ajali.

Mmoja kati ya wananchi hao Anuwari Is-haka Omar wa Matuleni, alisema wakati umefika sasa kwa serikali kutimiza ahadi ya ujenzi wa barabara hiyo.

‘’Kwa muda mrefu tumekuwa tukiskia kuwa ujenzi wa barabara hii, utaanza wakati wowote, lakini hadi sasa imeshapita miaka hatuoni kinachofanyika,’’alisema.

Kwa upande wake Mwanaisha Omar Haji wa Kipapo, alisema katika eneo la Chanjamjawiri, limekuwa maarufu kwa vyombo hasa vya maringi mawili, kugongana na kuanguka, kunakosababishwa na uchakavu wa barabara.

‘’Barabara imepasuka na kutengeneza mashimo makubwa, ambayo husababisha madereva kutozingatia upande aliopaswa kupita, jambo ambalo husababisha ajali,’’alieleza.

Nae Hamida Mjaka Muhsin na mwenzake Aisha Makame Juma wa Mizingani, wamesema wamekuwa na gamu wanapotaka kwenda miji ya Chake chake au Mkoani, kutokana na uchakavu wa barabara yao.

Walisema, wanaamini serikali itaijenga barabara hiyo, ingawa hawajui ni lini, kutokana na kuwekewa ahadi kwa muda mrefu.

‘’Hata hivi karibuni Rais wa Zanzibar Dk. Hussein Ali Mwinyi, alitueleza ana nia ya kuijenga lakini, ahadi kama hiyo ilishawahi kutolewa na mtangulizi wake, sasa inaumiza matumbo,’’alifafanua Hamida.

Dereva mmoja wa garia ya abiria inayofanyakazi katika mji wa Wamba na Chake chake, alisema, kwa sasa hawapitii tena vijiji vya Ngwachani, Kuyuni, Ngezi, Mgagadu, Kimbuni na Mizingani kutokana na kuharibika kwa barabara ya Chake chake -Mkoani.

‘’Kwa sasa inatulazimu kupitia barabara ya Kipapo-Mgelema hadi Wambaa, maana barabara kwa kupitia Mizingani imeharibika vibaya,’’alisema dereva huyo.

Akijibu hoja za Mwakilishi wa Jimbo la Mkoani, juu ya hatma ya ujenzi wa barabara hiyo, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi, alisema tayari mkandarasi wa ujenzi wa barabara hiyo, ameshapatikana, ambapo ujenzi utakapoaanza mkandarasi huyo, atashirikiana na kampuni ya Mecco.

Alisema pamoja na kupatikana kwa mjenzi huyo, tayari mkataba umeshasainiwa na hata fedha za utangulizi zimeshatolewa, ikiwa ni miongoni mwa matayarisho ya ujenzi wa barabara hiyo.

Dk. Mwinyi alisema, baada ya matayarisho kukamilika, mkandarasi huyo anatarajiwa kuingia barabara wakati wowote kuanza ujenzi huo, ili kuona wananchi wanaitumia.

Alieleza kuwa, katika kufanikisha hilo, kazi kubwa ya serikali ni kuangalia uwezekano wa kulipa fidia, kwa ajili ya majengo na vipando vya wananchi, ambavyo vimeshaonekana kuathirika wakati wa ujenzi huo.

Dk. Mwinyi alieleza kuwa, hana shaka kuwa barabara za Chake chake – Mkoani na Chake chake -Wete, mara zitakapomalizika ujenzi wake, itakuwa ni sehmu ya kukifungua kisiwa cha Pemba, kiuchumi.

‘’Wananchi wawe wastahamilivu, kwa kuwepo kwa kero ya barabara ya Mkoani- Chake chake, na taarifa tulizonazo ni njema, maana mjenzi ameshapatikana ni Propav atashirikiana na kampuni ya Mecco na hata fedha za utangulizi tayari,’’alieleza.

Aidha Rais huyo wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi, alisema hata fidia kwa upande wa ujenzi wa uwanja wa ndege kwa sehemu kubwa zimeshatolewa kwa wananchi na zilizobakia mchakato unaendelea.

                           Mwisho

 

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

Vikausha damu vya mjamzito hivi hapa, umo mchele, udongo, mkaa, chaki Uwezekano wa kuzaliwa watoto wenye udumavu, utapiamlo ni mkubwa

  NA ZUHURA JUMA, PEMBA@@@@ ‘’KILA ninapobeba mimba nimezoea kula mchele kwa wingi naweza kusamehe pilau au biriani,’’ ndio maneno ya mwanzao ya Bahati Mohamed Ali (sio jina lake halisi). Nilimfuma akiwa barazani kwake, mjini Ole wilaya ya Chake chake, pembeni yake akiwa na kibakuli cha mwazi, kwa umbali utaona amejaza chakula aina ya pepe, kumbe ni mchele wa Mbeya. Hujichotea kidogo kidogo na kuushindilia mdomoni mwake, huku akiendela kupiga storia na wenzake, bila ya kujali kuwa ujauzito alionayo na mchele huo hauna mwisho mwema. Kawaida yake akiwa mjamzito, kila anapoamka asubuhi anaroweka mchele upatao robo kilo hivi…na baada ya kumaliza kupika, yeye huchukua mchele wake kutafuna (kula). Wakati mwenza wake na watoto wao, wanakula chakula cha mchana, Bahati yeye hukaa pembeni na kibakuli chake cha mchele akiendelea kubahatisha afya yake. ‘’Mimba nyengine hupenda sana kutafuna mchele wa Mbea na nyengine hupenda mchele wa mapembe, kwa kweli huwa nina hamu (kileo), kwan...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...