Skip to main content

WAISLAM MTEMANI WAWI WAKUMBUSHWA JAMBO BAADA YA RAMADHAN


NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

WAUMINI wa dini ya kiislamu kijiji cha Mtemani, shehia ya Wawi wilaya ya Chake chake Pemba, wamekumbushwa kuyaendeleza mema yote waliyokuwa wakiyatenda katika mwezi mtukufu wa Ramadhan, kwani amri na makatazo hayo waliyokuwa wakiyatii, bado yanaendelea kuwepo.

Hayo yameleezwa na khatibu wa msikiti wa Mtemani Wawi wilaya ya Chake chake Salim Nassor, wakati akitoa hutuba mbili za swala ya Edi-l Fitir, mara baada ya kukamilika kwa swala hiyo, iliyofanyika msikitini hapo leo April 10, 2024.

Alisema, hipendezi na haingii akilini kuona waumini wa dini ya kiislamu waliokuwa wakifuata maamrisho ya Muumba, katika mwezi mtukufu wa Ramadhan na kisha sasa amri hizo, kuzipindua na kufanya watakavyo.

Alieleza kuwa, Muumba aliyekuwepo katika mwezi uliomalizika, ndio yule yule aliyepo katika miezi mingine, hivyo ni wajibu wa waumini hao kuendelea kumtii, ili kupata radhi zake.

Khatib huyo alifafanua kuwa, katika kipindi cha mfungo, kila mmoja alikuwa laini mbele ya mwenzake, na kutoonekana kwa walevi, wizi, zinaa, ngoma, kutukanana ambapo amri zote hizo, bado zinatakiwa kutekelezwa katika miezi mingine.

‘’Mimi niwausie waislamu wa Wawi na wingine duniani kote, katika mataifa mingine, bado amri za Muumba, ndio zile zile zilizokuwepo katika kipindi cha mwezi wa Ramadhan, na sasa zinaendelea hivyo ni wajibu wa kuzitii,’’aliwakumbusha.



Katika hatua nyingine Khatib huyo, aliwakumbusha waumini wa dini ya kiislamu, kwa siku ya leo ya sherehe ya sikukuu ni kula, kunywa, kuvaa na kutembelea maeneo yaliohalali, ili kuzitakasa nyoyo zao.

‘’Kwa mfano siku ya leo, unaweza kuwatembelea wagonjwa, wenye hali ngumu za maisha, mayatima kwa ajili ya kuwafariji kama sehemu ya sherehe na sio kufanya maasi,’’alifafanua.

Hata hivyo, amewakumbusha wazazi na walezi, kuwavisha mavazi ya staha watoto wao hasa wa kike, na kuacha kuwafunganisha na watoto wenzao wingi, ili kuepusha majanga.

‘’Kila mmoja ni shahidi kuwa, kwa siku hizi vyombo vya usafiri hasa vya maringi mawili ni vingi, lazima kwa mtoto mmoja asizidi mtoto mmoja, ambapo kufanya hivyo, itakuwa rahisi kwenye udhibiti,’’alieleza.



Baadhi ya waumini wa dini ya kiislamu, waliozungumza na mwandishi wa habari hii, wamewashauri waumini wenzao, kuyaacha kwa vitendo makatazo ya Muumba, ili iwe ni nusra katika maisha yao ya leo na baadae.

Omar Faki Hamdan wa Wawi, alisema hata mfano wa hutuba iliyotolewa katika msikiti uliopo Mtemanani, ni aina ya ukumbusho mzuri kwa waumini.

Nae Ridhiwan Othman Hamdu alisisitiza, haja kwa wazazi na walezi kuwasomesha watoto dini yao ya kiislamu, ili wajue namna bora na iliyoridhiwa na Muumba ya usherehekeaji wa sikuu za kiislamu.

Waumini wa dini ya kiislamu wa shehia ya Wawi na vijiji jirani, wameungana na waumini wingine dunini kote, leo Arpili10, 2024 katika sherehe ya sikuu ya Edi-lfitir, ambayo huja baada ya kufunga aidha siku 29 au 30 za mwezi mtukufu wa Ramadhan.

                                Mwisho

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch