Skip to main content

WATU WENYE ULEMAVU MAKOMBENI WATAKA ELIMU KUANZISHA USHIRIKA





NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

WATU wenye ulemavu shehia ya Makombeni wilaya ya Mkoani Pemba, wamesema wana hamu ya kutaka kuanzisha vikundi vya ushirika, ingawa changamoto ni taaluma ndogo ya kuendesha vikundi hivyo.

Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi shehiani hapo, walisema wamekuwa na hamu ya kutaka kujikusanya, ili kufikia ndoto zao kupitia vikundi vya ushirika, ingawa changamoto ni elimu ndogo ya uanzishwaji wa vikundi.

Walisema, wamekuwa wakigubikwa na umaskini wa kipato, ambao wanaamini kama wengekuwa na uwezo kielimu wa kuanzisha vikundi, wengekuwa na hali nzuri kimaisha.

Mmoja kati ya watu hao wenye ulemavu wa ualibino Mbuke Ramadhan Mussa, alisema wamekuwa hawajui wapi pakuanzia ili hadi kufikia kuwa na kikundi cha ushirika.

Alieleza kuwa, hawaelewi kuwa sheha anaweza kuwa chanzo cha wao kuanzisha vikundi vya ushirika, bali wapo kwenye makaazi wakiwa hawajui la kufanya.

‘’Ni kweli sisi watu wenye ulemavu wa shehia ya Mkoambeni, tunahitaji kupata uwelewa wa kuanzisha vikundi vya ushirika, ili tuwe kama wenzetu katika kukuza pato lao,’’alieleza.

Kwa upande wake Mayasa Makame Chumu mwenye ulemavu wa viungo, alisema inawezekana hali ngumu waliyonayo inatokana na kukosa elimu ya kutojikusanya pamoja.

‘’Naamini kama tutapewa mtaalamu wa kutupatia elimu ya uanzishwaji wa vikundi, umaskini wa kipato kwetu utakuwa ndoto,’’alieleza.

Hata hivyo Mwajuma Khamis Juma na mwenzake Omar Kombo Kheir, waliziomba taasisi za watu wenye ulemavu kuwafikia shehia kwao, ili kukaa nao na kuwaelekeza.

‘’Tunaambiwa kuwa kuna haki zetu kupitia sheria na mikataba mbali mbali, sasa zitekelezwe kwa wahusika kufika shehiani kwetu ili watupe elimu,’’walishauri.

Mapema sheha wa shehia ya Makombeni Mwashum Makame Haji, aliwataka watu hao wenye ulemavu kujikusanya pamoja, na kisha kuwasili ofisini kwake.







Alieleza kuwa, kama wameshakuwa tayari kwa ajili ya kuanzisha vikundi vya ushirika wa aina yoyote, wafike kwake ili kisha kuwatafutia mtaalamu husika.

‘’Hata hapa Makombeni wapo watu ambao wana uwezo mzuri wa kuwaelimisha, sasa wajipange na kisha waje ili tuwakabidhi na kuwaelekeza aina ya ushirika na jumuia zilivyo,’’alieleza.

Katika hatua nyingine sheha huyo aliwataka viongozi wa jumuiya na vyama vya ushirika vilivyomo shehiani mwake, kuwashirikiana kwa karibu na watu wenye ulemavu.

Afisa wa watu wenye ulemavu mkoa wa kusini Pemba, ambae anakimu wilaya ya Mkoani, Mussa Seif Mussa amekiri kuwepo kwa shida hiyo, na kuahidi kufika shehiani humo.

Alieleza, hawakuwa na taarifa hiyo kwa siku zote, ingawa sasa baada ya kupokea malalamiko hayo, watajipanga ili kwenda Makombeni kukutana na watu hao.

‘’Hili ni jukumu letu la msingi la kuwapitia wenzetu wenye ulemavu ili kujua changamoto na utendaji wa shughuli zao mbali mbali,’’alieleza.

Hata hivyo Afisa huyo aliwataka watu hao wenye ulemavu wa shehia ya Makombeni, kuendelea kufuatilia vyombo vya habari, ili kujua namna ya kuanzisha vikundi hivyo.

Mratibu wa baraza la taifa la watu wenye ulemavu Mashavu Juma Mabrouk, alisema atafuatilia kwa karibu watu hao, ili kujua changamoto zao.


Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, ilipata mkopo wa shilingi bilioni 230, ambapo wizara ya Uwezeshaji ilipata shilingi bilioni 31, kwa ajili ya wajasiriamali.

Katibu Mtendaji wa baraza la taifa la watu wenye ulemavu Zanzibar Ussi Khamis Debe, alisema fedha za mikopo zimekuwa na changamoto kuombwa na vikundi vya watu wenye ulemavu.

‘’Kwa mfano tumefanikiwa kuanzisha vikundi 90 vya watu wenye ulemavu kwa Unguja na Pemba, lakini ni vikundi 12 pekee vilivyopata na vyengine vilishindwa njiani,’’alieleza.

                    Mwisho       

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch