Skip to main content

VIFO VYA BODA BODA, WAHANGA, AMADEREVA, POLISI WATAJA MADHARA KWA JAMII

 




   

                    

NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

MOJA ya madhara ya vifo vya ajali za Boda boda ni kukatisha uhai wa abiria, madereva au waenda kwa miguu.

Wahanga wanasema, licha ya magonjwa kama Corona, maleria, kipindu pindu kuwa yanapoteza wapendwa wao, lakini ajali za Boda boda zinachangia.

Wanaainisha kuwa, boda boda zimekuwa zikikatisha uhai wa wapenzi wao, wakuu wao wa familia au wazazi wao, na kuwaacha wakiwa hawana uhakika wa maisha.

Hassan Haji Mohamed wa Vitongoji wilaya ya Chake chake, anasema, kwa sasa anaishi na mguu mmoja kwa miaka saba, baada ya kupata ajali ya boda boda.

‘’Nilikuwa nimepakiwa nakwenda msibani kwa mdogo wangu, lakini kisha dereva alichanganya mwendo, na kuingia pembezoni mwa gari ya mzigi iliyokuwa imeegeshwa na kupata kilema cha kudumu,’’anakumbuka.

Mohamed Othman Juma wa Mkoani mjini, anasema alipoteza vidole viwili vya mkono wa kulia, baada ya boda boda aliyokuwa amepanda kugongana na gari ya abiria.

‘’Mwendo ulikuwa mzuri kisa, lakini dereva alitaka kulipita gari la mazigo, lakini sukani ilimshinda na kulivamia kwa mbavuni na mimi kuumia,’’anasimulia.

Khadija Ussi Haji wa Wete ambae kwa sasa ni kuzuka na kuachiwa watoto watatu, anasema muume wake alifariki kwa ajili ya boda boda.

Anasimulia kuwa, kwa sasa anaishia maisha ya kubahatisha hasa kwa vile hakuna msaada wa familia hata moja, jambo linalompa wasi wasi wa kila siku.

Khadija Chande Hamad wa Kojani Wete, anasema kwa sasa anaishi na wajukuu zake watatu wote ni mayatima wa ajali za boda boda, ambao baba yao alifariki eneo la Mchanga mdogo.

‘’Ilikuwa ni kama saa 7:00 imeelezwa wakifukuzana wao kwa wao kutoka Konde hadi Ole, ingawa kufika Mchanga mdogo, walivamiana,’’anaeleza.

Kwa sasa bibi huyo na wajukuu zake, anasema anaishi kwa maisha ya kuomba omba, kutoka kwa ndugu na jamaa zake, kwani familia ya upande mmoja imesusia kutoa huduma.

 

POLISI LINATAJA MADHARA YA AJALI HIZO

Kamishna wa Polisi Zanzibar ‘CP’ Hamad Khamis Hamad, anasema moja ni kupunguza nguvu kazi ya taifa, kwani wengi wa madereva wa boda boda ni vijana.

‘’Kuzipa gharama za mazishi au matibabu familia ambazo, pengine hawakujipangia kwa wakati huo, ni miongoni mwa madgara ya ajali za boda boda,’’anasema.

Mkuu wa kikosi cha usalama barabarani ‘TRO’ mkoa wa Mjini magharibi Unguja Khamis Mwakanolo, anaona madhara ni abiria, dereva au mpatwa na ajali kupata madhara ya mwilini mwake.

Nae Mkuu wa usalama barabarani Mkoa wa kusini Pemba ‘RTO’ Shawal Abdalla Ali, anaona madhara ni kujidhoofisha kiuchumi kwa mmiliki wa boda boda,

‘’Lakini pia kusababisha vifo, vilema, vizuka na kuongeza kwa mayatima, huwa ni madhara makubwa yatokanayo na ajali za boda boda,’’anaaninisha Shawal.

MADEREVA WA BODA BODA

Omar Khamis Haji ‘Kiomi’ anasema madhara ni kupoteza uhai wao, jambo ambalo linaweza kuwaweka wengine kwenye umaskini.

‘’Maana inawezekana familia tayari inakutegemea, lakini kama ukipata ajali na kisha kuwa kilema ama kupoteza uhai, tayari umeshawasababishia wengine kuishi kwenye umaskini,’’anasema.

 chanzoa cha ajali hizo ni usimamizi hatarishi wa askari wa usalama barabarani.

Maulid Himid Haji wa Ole, anasema madhara anayoyaona ni kuwapotezea imani jamii, juu waenesha boda boda kuwa wamekuwa chanzo cha ajali za barabarani.

Ussi Haji Said na mwenzake Bakar Juma Ibrahimu, wanasema pamoja na kupata vilema vya kudumu, lakini wamekuwa wakiitia hasara serikali kwa matitabu.

‘’Mwaka 2020 mwenztu eneo la Chake chake alijigonga na ukuta na kuvurugika vibaya, ilibidi asafirishwe na kutumika gharama zaidi ya shilingi 800,000 na hadi leo ni mlemavu,’’anasema Ussi.

Mwenyekiti wa Jumuia ya waendesha boda boda mkoa wa kusini Pemba Kassim Khamis Juma, anaona amdhara ni vijana kuondoka duniani kila siku.

‘’Ni kweli ajali za boda boda zimekuwa nyingi mno, jambo linapunguza idadi ya vijana na kuongezeka wazee, ambao wanaelekea kukosa wasaidizi,’’anasema.

Mmiliki wa Boda Boda Fatma Haji Said wa Msingi Chake chake, anasema kwake ni kupotezea kwa mali yake (boda boda), ambayo aliamini ndio kitega uchumi chake.

‘’Tumetakiwa tujiajiri, sasa kama umenunua chombo baada ya siku nne, kijana anakwambia ameiongesha na mti, ni kukurejesha nyuma kimaisha,’’anasema.

TAKWIMU ZA AJALI
Uchunguuzi uliofanywa na mwandishi wa habari hizi, umebaini kuwa, kwa mfano kwa mwaka 2019 hadi mwaka 2020 kwa Tanzania, kulikuwa na ajali za piki piki 1,133 zilizosababisha vifo 674, sawa na majeruhi 948.

Imebainika kuwa, kati ya ajali hizo, Tanzania bara kuliripotiwa ajali 964, zilizosababisha vifo 573 na majeruhi 767 kwa miaka hiyo miwili.

Wakati kwa Zanzibar, kuliripotiwa ajali 169 sawa na vifo 101 huku idadi ya majeruhi wakiwa ni 181.

Katika kipindi cha Januari hadi Disemba pekee kwa mwaka 2020 kwa Tanzania, kulikuwa na matukio 505 ya ajali za pikipiki, ikilinganishwa na matukio 628 katika kipindi kama hicho mwaka 2019.

Kwa upande wa Zanzibar, mikoa iliyoongoza kwa ajali za piki piki katika mwaka 2020, ni mkoa wa Mjini magharibi ulioripoti ajali 1,774, ukihusisha vifo 25.

Ingawa kati ya hao, wanaume waliongoza kwa kuwa 24, huku wanawake akiripotiwa mmoja aliyefariki, kutokana na ajali za piki piki.

Mkoa mwengine ni wa Kusini Unguja kwa ajali 469, sawa na vifo watu 10, huku wanaume wakiwa wanane (8), na wanawake wawili.

Mkoa wa kusini Pemba, uliripoti matukio 604, yakihusisha vifo 10, wakiwemo wanawake wawili (2) na wanaume wanane (8).

Uchunguzi ukabaini kuwa, kwa mwaka huo wa 2020, mkoa wa Kaskazini Unguja ulikuwa na ajali 311, ambazo zilihusisha vifo vya wanaume wanane (8) na mwanamke mmoja, ambapo mkoa wa Kaskazini Pemba, ulikuwa na ajali 858, sawa na vifo vya watu watano (5) wote wakiwa wanaume. 

 


 

ATHARI ZA AJALI ZA PIKI PIKI

Kassim Haji Ali abiria ambae kwa sasa ana mkono mmoja, anasema kwanza ni kupata ulemavu wa kudumu ambao haukutarajiwa.

Mayasa Hassan Hemed ambae mume wake alipoteza maisha mwaka 2022 kwa ajili ya pili pili, anasema ni vifo na kuwaacha watoto wakiwa na mlezi mmoja.

Baba ambae mtoto wake alifariki kwa ajili, anasema ni kukosa nguvu kazi ya familia, kwani kila familia inawategemea wengine kwenya kazi.

Mkuu wa kikosi cha usalama barabarani mkoa wa Mjini magharibi Unguja ‘RTO’ Khamis Mwakanolo, athari ni kuongeza umaskini ndani ya familia, kwa matibabu makubwa.

Mmiliki wa piki piki (boda boda) Michakaini Chake chake Pemba Kombo Haji Kombo, anasema kwanza ni kuwarejesha nyuma wao walioekeza kwenye vyombo hivyo.

Doktari Khamis Haji Khamis anasema, ni matumizi ya dawa yasiyotarajiwa, kwa waendesha piki piki, ambao kwa mwezi hujitokeza katia ya watatu hadi watano.

NINI KIFANYIKE KUPUNGUZA AJALI?

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi, wakati akikabidhi piki piki za mkopo mkoa wa kusini Pemba, aliwataka madereva kukomaa katika utii wa sheria za barabarani.

‘’Sitofurahishwa kusikia siku moja muendesha boda boda amekuwa chanzo cha ajali barabarani, kwani tunawakabidhi vyombo hivi vikakuze uchumi na sio kuongeza ajali, majeruhi, vilema na vifo,’’aliwakumbusha.  

Kamisha wa Polisi Zanzibar ‘CP’ Hamad Khamis Hamad, anasema kwanza ni elimu kwa waendesha piki piki, juu ya matumizi sahihi ya barabara.

Mwenyekiti wa Jumuiya ya boda boda mkoa wa kusini Pemba, Kassim Khamis Juma, anasema kuimarishwa kwa miundo mbinu ya barabara, hasa kutokana na ongezeko la vyombo vya moto.

Dereva wa piki piki Othman Issa Yakoub anasema utaratibu wa kukagua piki piki kila wakati uondoke, na badala yake kuwe na mifupo ya kisasa.

Mwananchi Zuhra Juma Mmanga wa Ngwachani Mkoani anasema, ni uwepo wa adhabu kali kwa dereva wa piki piki, atakaetiwa hatiani kwa kosa hilo.

Afisa Sheria kutoka Idara ya Katiba na Msaada wa Kisheria Zanzibar Bakar Omar Ali, anasema kamera zilizopo mjini zitumike kuwatia hatiani wanaokiuka sheria.

MITANDAO YA KIJAMII IMERIPOTI NINI?

Ajali za barabarani zinatajwa kuwa ndio zinasababisha vifo vingi vya watu duniani kulimo magonjwa yoyote, Shirika la Afya Duniani WHO linasema.

 

WHO kwenye ripoti yake ya mwaka 2018, limeanisha licha ya bara la Afrika kuwa na idadi ndogo ya vyombo vya usafiri, lakini ndilo lenye ajali nyingi za barabarani duniani, kuliko mataifa ya Ulaya.

 

Katika ripoti hiyo ‘WHO’ linasema kuwa kuna vifo 27 kwa kila watu 1000, huku likifafanua kuwa, kuna vifo vya barabarani katika nchi za Afrika ni mara tatu zaidi ya ajali zinazotokea Ulaya.

 

Ripoti ikafafanua kuwa, karibu nusu ya mataifa 54 ya Afrika hayana sheria za mwendo kasi katika nchi zao, huku nchi kama Botswana, Ivory Coast na Cameroon, ni miongoni mwa nchi ambazo zimeona kiwango cha vifo vikiongezeka.

 

Kwa mujibu wa taarifa za hivi karibuni , zinasema kuwa watu milioni 1.35 waliuwawa katika ajali za barabarani duniani kwa mwaka 2016, kiwango ambacho kiko tofauti kidogo na mwaka uliopita.

 

Upande mwengine katika ripoti iliyotolewa na Benki ya Dunia, imeelezwa kuwa hadi kufikia mwaka 2020, idadi ya vifo vinavyosababishwa na ajali za barabarani katika nchi za Afrika Kusini mwa jangwa la Sahara, itaongezeka kwa asilimia 80.

 

                     Mwisho

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch