Skip to main content

WANAWAKE MAKOMBENI ""HATUNA UWELEWA MPANA DHANA UCHUMI WA BULUU"

 

 


NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

WANAWAKE wa shehia wa Makombeni wilaya ya Mkoani Pemba, wameomba kuongezewa ufahamu juu ya dhana ya uchumi wa buluu, ili waifahamu kwa kina malengo ya serikali kuu.

Walisema, wamekuwa wakisikia juu juu ya dhana hiyo, ingawa bado wamekuwa hawana uwelewa wa ndani, na kusababisha kubakia na uwelewa wa wao zamani.

Wakizungumza na waandishi wa habari wa Shirika la Magazeti ya serikali Zanzibar ofisi ya Pemba waliofika kusikiliza changamoto zao, walisema bado dhana hiyo haiku vyema kwenye akili yao.

Walisema kua, wanahitaji mamla husika kufika Makombeni kuwaeleza kwa kina juu ya dhana ya uchumi wa buluu, ili waende samba mba na kaluli ya rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi.

Mmoja kati ya wanawake hao Mayasa Makame Chumu, alisema bado baadhi yao wamekuwa wakisikiliza vyombo vya habari, ingawa dhana hiyo bado hawajaipata vyema.

‘’Dhana ya uchumi wa buluu tunaiskia kwenye vyombo ya habari, lakini hasa kuipata kwa upana bado, baada hatujawahi kuwapa wataalamu kutueleza,’’alieleza.

Nae Mwajuma Khamis Juma, alieleza kuwa ni wakati sasa kwa wataalamu kutoa Idara ya Uchumi wa buluu kufika Makombeni ili kukutana nao ana kwa ana.

Naeo Faida Faki Kombo, Zuhura Haji Kheir na Semeni Juma Kheir, wamesema vipindi vya kwenye redio na tv wanavisikia, ingawa hawapati kuuliza maswali.

Walieleza kuwa, wamekuwa wakisikiliza vipindi vya kwenye redio, lakini changamoto wanayokumbana nayo ni kukosa kuuliza juu dhana ya uchumi wa buluu.

‘’Vipindi vya redio ni kweli vinatoka kwenye redio, lakini hatupati kuuliza sasa tunaomba wataalamu husika wafikie shehiani kwetu,’’wamependekeza.

Sheha wa shehia wa Makombeni Mwashum Haji Makame, alikiri kuwa ipo haja kwa wataalamu kutoka Idara ya Uchumi wa buluu kufika shehiani mwake.

Alieleza kuwa wananchi wamekuwa na hamu kubwa ya kukutana na wataalamu ili kuelezea namna ambavyo dhana hiyo inaweza kuwakomboa.

‘’Wananchi wa shehia yangu wengi wanaitegemea bahari kwa shughuli zao mbali mbali za maendeleo, ikiwemo suala la uchumi wa buluu, lakini bado hawana uwelewa mpana,’’alieleza.

Hata hivyo sheha huyo amewataka wananchi wake, kuendelea kufuatilia kwa karibu vyombo vya habari, ambapo wanaweza kupata uwelewa japo mdogo, ili kujua vipi habari inaweza kuwasaidia.

Kaimu Afisa Mdhamini wizara ya Uchumi wa Buluu na Uvuvi Pemba, Abdull-malik Mohamed Bakar, alisema tayari shehi zote za Pemba, wameshazifikia kutoa ufafanuzi wa dhana ya uchumui wa buluu.

Alieleza kuwa, inawezekana wapo wananchi ambao hawakubahatika kuhudhuria kwenye mikutano wakati maafisa wa Idara ya Uchumi wa buluu walipopita kwenye shehia zao.

‘’Kama wananchi hao wa shehia ya Makombeni wanahitaji tena elimu, tutawasiliana na uongozi wa shehia, ili kutupangia mkutano mwengine,’’alieleza.

Hata hivyo aliwasisitiza wananchi hao, kuendelea kufuatilia vyombo vya habari, kwani kumekuwa na vipindi kadhaa vinavyoendeshwa juu ya dhana ya uchumi wa buluu.

Rais wa Zanzibar Dk. Hussein Ali Mwinyi tayari ameshakabidhi vifaa vya uvuvi, ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa dhana hiyo kwa vitendo.

                           Mwisho   

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch